< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
homo natus de muliere brevi vivens tempore repletus multis miseriis
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
quasi flos egreditur et conteritur et fugit velut umbra et numquam in eodem statu permanet
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
et dignum ducis super huiuscemodi aperire oculos tuos et adducere eum tecum in iudicium
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
quis potest facere mundum de inmundo conceptum semine nonne tu qui solus es
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
breves dies hominis sunt numerus mensuum eius apud te est constituisti terminos eius qui praeterire non poterunt
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
recede paululum ab eo ut quiescat donec optata veniat sicut mercennarii dies eius
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
lignum habet spem si praecisum fuerit rursum virescit et rami eius pullulant
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
si senuerit in terra radix eius et in pulvere emortuus fuerit truncus illius
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
ad odorem aquae germinabit et faciet comam quasi cum primum plantatum est
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
homo vero cum mortuus fuerit et nudatus atque consumptus ubi quaeso est
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
quomodo si recedant aquae de mari et fluvius vacuefactus arescat
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
sic homo cum dormierit non resurget donec adteratur caelum non evigilabit nec consurget de somno suo
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
quis mihi hoc tribuat ut in inferno protegas me ut abscondas me donec pertranseat furor tuus et constituas mihi tempus in quo recorderis mei (Sheol h7585)
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
putasne mortuus homo rursum vivet cunctis diebus quibus nunc milito expecto donec veniat inmutatio mea
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
vocabis et ego respondebo tibi operi manuum tuarum porriges dexteram
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
tu quidem gressus meos dinumerasti sed parces peccatis meis
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
signasti quasi in sacculo delicta mea sed curasti iniquitatem meam
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
mons cadens defluet et saxum transfertur de loco suo
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
lapides excavant aquae et adluvione paulatim terra consumitur et homines ergo similiter perdes
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
roborasti eum paululum ut in perpetuum pertransiret inmutabis faciem eius et emittes eum
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
sive nobiles fuerint filii eius sive ignobiles non intelleget
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
attamen caro eius dum vivet dolebit et anima illius super semet ipso lugebit

< Ayubu 14 >