< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
婦の産む人はその日少なくして艱難多し
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
その來ること花のごとくにして散り 其馳ること影のごとくにして止まらず
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
なんぢ是のごとき者に汝の目を啓きたまふや 汝われを汝の前にひきて審判したまふや
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
誰か清き物を汚れたる物の中より出し得る物あらん 一人も無し
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
その日既に定まり その月の數なんぢに由り 汝これが區域を立て越ざらしめたまふなれば
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
是に目を離して安息を得させ 之をして傭人のその日を樂しむがごとくならしめたまへ
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
それ木には望あり 假令砍るるとも復芽を出してその枝絶ず
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
たとひ其根地の中に老い 幹土に枯るとも
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
水の潤霑にあへば即ち芽をふき枝を出して若樹に異ならず
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
然ど人は死れば消うす 人氣絶えなば安に在んや
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
水は海に竭き河は涸てかわく
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
是のごとく人も寢臥てまた興ず 天の盡るまで目覺ず睡眠を醒さざるなり
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
願はくは汝われを陰府に藏し 汝の震怒の息むまで我を掩ひ 我ために期を定め而して我を念ひたまへ (Sheol h7585)
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
人もし死ばまた生んや 我はわが征戰の諸日の間望みをりて我が變更の來るを待ん
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
なんぢ我を呼びたまはん 而して我こたへん 汝かならず汝の手の作を顧みたまはん
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
今なんぢは我に歩履を數へたまふ 我罪を汝うかがひたまはざらんや
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
わが愆は凡て嚢の中に封じてあり汝わが罪を縫こめたまふ
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
それ山も倒れて終に崩れ巖石も移りてその處を離る
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
水は石を鑿ち 浪は地の塵を押流す 汝は人の望を斷たまふ
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
なんぢは彼を永く攻なやまして去ゆかしめ 彼の面容の變らせて逐やりたまふ
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
その子尊貴なるも彼は之を知ず 卑賤なるもまた之を曉らざるなり
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
只己みづからその肉に痛苦を覺え己みづからその心に哀く而已

< Ayubu 14 >