< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
אדם ילוד אשה קצר ימים ושבע רגז׃
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
כציץ יצא וימל ויברח כצל ולא יעמוד׃
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
אף על זה פקחת עינך ואתי תביא במשפט עמך׃
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
מי יתן טהור מטמא לא אחד׃
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
אם חרוצים ימיו מספר חדשיו אתך חקו עשית ולא יעבור׃
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
שעה מעליו ויחדל עד ירצה כשכיר יומו׃
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
כי יש לעץ תקוה אם יכרת ועוד יחליף וינקתו לא תחדל׃
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
אם יזקין בארץ שרשו ובעפר ימות גזעו׃
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
מריח מים יפרח ועשה קציר כמו נטע׃
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
וגבר ימות ויחלש ויגוע אדם ואיו׃
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
אזלו מים מני ים ונהר יחרב ויבש׃
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
ואיש שכב ולא יקום עד בלתי שמים לא יקיצו ולא יערו משנתם׃
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
מי יתן בשאול תצפנני תסתירני עד שוב אפך תשית לי חק ותזכרני׃ (Sheol h7585)
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
אם ימות גבר היחיה כל ימי צבאי איחל עד בוא חליפתי׃
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
תקרא ואנכי אענך למעשה ידיך תכסף׃
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
כי עתה צעדי תספור לא תשמור על חטאתי׃
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
חתם בצרור פשעי ותטפל על עוני׃
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
ואולם הר נופל יבול וצור יעתק ממקמו׃
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
אבנים שחקו מים תשטף ספיחיה עפר ארץ ותקות אנוש האבדת׃
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
תתקפהו לנצח ויהלך משנה פניו ותשלחהו׃
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
יכבדו בניו ולא ידע ויצערו ולא יבין למו׃
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
אך בשרו עליו יכאב ונפשו עליו תאבל׃

< Ayubu 14 >