< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
Man, that is born of woman, Is of few days, and full of trouble.
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
He cometh forth as a flower, and is cut down; He fleeth also as a shadow, and continueth not.
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
And dost thou fix thine eyes upon such a one? And dost thou bring me into judgment with thee?
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
Who can produce a clean thing from an unclean? Not one.
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
Seeing that his days are determined, And the number of his months, with thee, And that thou hast appointed him bounds which he cannot pass,
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
O turn thine eyes from him, and let him rest, That he may enjoy, as a hireling, his day!
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
For there is hope for a tree, If it be cut down, that it will sprout again, And that its tender branches will not fail;
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
Though its root may have grown old in the earth, And though its trunk be dead upon the ground,
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
Through the scent of water it will bud, And put forth boughs, like a young plant.
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
But man dieth, and he is gone! Man expireth, and where is he?
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
The waters fail from the lake; And the stream wasteth and drieth up;
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
So man lieth down, and riseth not; Till the heavens be no more, he shall not awake, Nor be roused from his sleep.
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
O that thou wouldst hide me in the under-world! That thou wouldst conceal me till thy wrath be past! That thou wouldst appoint me a time, and then remember me! (Sheol h7585)
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
If a man die, can he live again? All the days of my war-service would I wait, Till my change should come.
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
Thou wilt call, and I will answer thee; Thou wilt have compassion upon the work of thy hands!
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
But now thou numberest my steps; Thou watchest over my sins.
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
My transgression is sealed up in a bag; Yea, thou addest unto my iniquity.
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
As the mountain falling cometh to nought, And the rock is removed from its place;
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
As the waters wear away the stones, And the floods wash away the dust of the earth, So thou destroyest the hope of man.
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
Thou prevailest against him continually, and he perisheth; Thou changest his countenance, and sendest him away.
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
His sons come to honor, but he knoweth it not; Or they are brought low, but he perceiveth it not.
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
But his flesh shall have pain for itself alone; For itself alone shall his soul mourn.

< Ayubu 14 >