< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
HE AQUÍ que todas estas cosas han visto mis ojos, y oído y entendido de por sí mis oídos.
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
Como vosotros lo sabéis, lo sé yo; no soy menos que vosotros.
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
Mas yo hablaría con el Todopoderoso, y querría razonar con Dios.
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
Que ciertamente vosotros sois fraguadores de mentira; sois todos vosotros médicos nulos.
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
Ojalá callarais del todo, porque os fuera sabiduría.
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
Oid ahora mi razonamiento, y estad atentos á los argumentos de mis labios.
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
¿Habéis de hablar iniquidad por Dios? ¿habéis de hablar por él engaño?
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
¿Habéis de hacer acepción de su persona? ¿habéis de pleitear vosotros por Dios?
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
¿Sería bueno que él os escudriñase? ¿os burlaréis de él como quien se burla de algún hombre?
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
El os reprochará de seguro, si solapadamente hacéis acepción de personas.
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
De cierto su alteza os había de espantar, y su pavor había de caer sobre vosotros.
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
Vuestras memorias serán comparadas á la ceniza, y vuestros cuerpos como cuerpos de lodo.
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
Escuchadme, y hablaré yo, y véngame después lo que viniere.
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
¿Por qué quitaré yo mi carne con mis dientes, y pondré mi alma en mi mano?
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
He aquí, aunque me matare, en él esperaré; empero defenderé delante de él mis caminos.
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
Y él mismo me será salud, porque no entrará en su presencia el hipócrita.
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
Oid con atención mi razonamiento, y mi denunciación con vuestros oídos.
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
He aquí ahora, si yo me apercibiere á juicio, sé que seré justificado.
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
¿Quién es el que pleiteará conmigo? porque si ahora yo callara, fenecería.
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
A lo menos dos cosas no hagas conmigo; entonces no me esconderé de tu rostro:
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
Aparta de mí tu mano, y no me asombre tu terror.
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
Llama luego, y yo responderé; ó yo hablaré, y respóndeme tú.
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
¿Cuántas iniquidades y pecados tengo yo? hazme entender mi prevaricación y mi pecado.
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
¿Por qué escondes tu rostro, y me cuentas por tu enemigo?
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
¿A la hoja arrebatada has de quebrantar? ¿y á una arista seca has de perseguir?
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
¿Por qué escribes contra mí amarguras, y me haces cargo de los pecados de mi mocedad?
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
Pones además mis pies en el cepo, y guardas todos mis caminos, imprimiéndolo á las raíces de mis pies.
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
Y el [cuerpo mío] se va gastando como de carcoma, como vestido que se come de polilla.

< Ayubu 13 >