< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
“He aquí que mi ojo ha visto todo esto. Mi oído lo ha escuchado y comprendido.
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
Lo que tú sabes, yo también lo sé. No soy inferior a ti.
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
“Seguramente hablaré con el Todopoderoso. Deseo razonar con Dios.
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
Pero ustedes son forjadores de mentiras. Todos ustedes son médicos sin valor.
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
¡Oh, que te calles por completo! Entonces serías sabio.
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
Escucha ahora mi razonamiento. Escucha las súplicas de mis labios.
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
¿Hablarás injustamente por Dios, y hablar con engaño por él?
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
¿Mostrarás parcialidad hacia él? ¿Contenderás por Dios?
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
¿Es bueno que te busque? O como se engaña a un hombre, ¿lo engañarás tú?
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
Seguramente te reprenderá si secretamente muestra parcialidad.
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
Su majestad no te hará temer y que su temor caiga sobre ti?
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
Tus dichos memorables son proverbios de ceniza. Sus defensas son defensas de arcilla.
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
“¡Cállate! Dejadme en paz, para que pueda hablar. Que venga sobre mí lo que quiera.
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
¿Por qué debo tomar mi carne entre los dientes, ¿y poner mi vida en mi mano?
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
He aquí que él me matará. No tengo ninguna esperanza. Sin embargo, mantendré mis caminos ante él.
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
Esta también será mi salvación, que un hombre sin Dios no se presentará ante él.
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
Escucha atentamente mi discurso. Que mi declaración esté en tus oídos.
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
Mira ahora, he puesto mi causa en orden. Sé que soy justo.
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
¿Quién es el que va a contender conmigo? Porque entonces callaría y dejaría el espíritu.
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
“Sólo no me hagas dos cosas, entonces no me esconderé de tu rostro:
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
retira tu mano lejos de mí, y no dejes que tu terror me haga temer.
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
Entonces llama, y yo responderé, o déjame hablar, y tú me respondes.
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
¿Cuántas son mis iniquidades y pecados? Hazme conocer mi desobediencia y mi pecado.
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
¿Por qué ocultas tu rostro? ¿y me consideras tu enemigo?
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
¿Acosarías a una hoja manejada? ¿Perseguirás el rastrojo seco?
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
Porque escribes cosas amargas contra mí, y hazme heredar las iniquidades de mi juventud.
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
También pusiste mis pies en el cepo, y marca todos mis caminos. Me has atado a las plantas de los pies,
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
aunque me estoy descomponiendo como una cosa podrida, como una prenda apolillada.

< Ayubu 13 >