< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
視よわが目これを盡く觀 わが耳これを聞て通逹れり
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
汝らが知るところは我もこれを知る 我は汝らに劣らず
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
然りと雖ども我は全能者に物言ん 我は神と論ぜんことをのぞむ
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
汝らは只謊言を造り設くる者 汝らは皆無用の醫師なり
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
願くは汝ら全く默せよ 然するは汝らの智慧なるべし
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
請ふわが論ずる所を聽き 我が唇にて辨爭ふ所を善く聽け
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
神のために汝ら惡き事を言や 又かれのために虚僞を述るや
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
汝ら神の爲に偏るや またかれのために爭はんとするや
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
神もし汝らを鑒察たまはば豈善らんや 汝等人を欺むくごとくに彼を欺むき得んや
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
汝等もし密に私しするあらば彼かならず汝らを責ん
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
その威光なんぢらを懼れしめざらんや 彼を懼るる畏懼なんぢらに臨まざらんや
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
なんぢらの諭言は灰に譬ふべし なんぢらの城は土の城となる
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
默して我にかかはらざれ 我言語んとす 何事にもあれ我に來らば來れ
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
我なんぞ我肉をわが齒の間に置き わが生命をわが手に置かんや
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
彼われを殺すとも我は彼に依賴まん 唯われは吾道を彼の前に明かにせんとす
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
彼また終に我救拯とならん 邪曲なる者は彼の前にいたること能はざればなり
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
なんぢら聽よ 我言を聽け我が述る所をなんぢらの耳に入しめよ
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
視よ我すでに吾事を言竝べたり 必ず義しとせられんと自ら知る
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
誰か能われと辨論ふ者あらん 若あらば我は口を緘て死ん
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
惟われに二の事を爲たまはざれ 然ば我なんぢの面をさけて隱れじ
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
なんぢの手を我より離したまへ 汝の威嚴をもて我を懼れしめたまはざれ
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
而して汝われを召たまへ 我こたへん 又われにも言はしめて汝われに答へたまへ
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
我の愆われの罪いくばくなるや 我の背反と罪とを我に知しめたまへ
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
何とて御顏を隱し我をもて汝の敵となしたまふや
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
なんぢは吹廻さるる木の葉を威し 干あがりたる籾殼を追たまふや
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
汝は我につきて苦き事等を書しるし 我をして我が幼稚時の罪を身に負しめ
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
わが足を足械にはめ 我すべての道を伺ひ 我足の周圍に限界をつけたまふ
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
我は腐れたる者のごとくに朽ゆき 蠹に食るる衣服に等し

< Ayubu 13 >