< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
Ecco, l'occhio mio ha vedute tutte [queste cose], L'orecchio mio le ha udite, e le ha intese.
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
Quanto sapete voi, so anch'io; Io non son da men di voi.
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
E pure io parlerò all'Onnipotente; Io avrò a grado di venire a ragione con lui.
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
Ma certo, quant'è a voi, voi siete rappezzatori di menzogna; Voi [siete] medici da nulla tutti quanti.
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
Oh! vi taceste pur del tutto, Ciò vi sarebbe [reputato] in saviezza!
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
Deh! ascoltate la difesa della mia ragione, Ed attendete agli argomenti delle mie labbra.
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
Convienvisi in favor di Dio parlar perversamente, E per rispetto suo parlar frodolentemente?
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
Convienvisi aver riguardo alla qualità sua? Convienvisi litigar per Iddio?
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
[Sarebbe egli] ben [per voi] ch'egli vi esaminasse? Gabberestelo voi come si gabba un uomo?
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
Egli del certo vi arguirà, Se di nascosto avete riguardo alla qualità delle persone.
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
La sua altezza non vi sgomenterà ella? Lo spavento di lui non vi caderà egli addosso?
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
I vostri [detti] memorandi [son] simili a cenere; [Ed] i vostri sublimi [ragionamenti] a mucchi di fango.
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
Tacetevi, e lasciatemi stare, ed io parlerò; E passimi addosso che che sia.
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
Perchè mi strappo io la carne co' denti, E [perchè] tengo l'anima mia nella palma della mia mano?
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
Ecco, uccidami egli pure; sì spererò in lui; Ma tuttavia difenderò le mie vie nel suo cospetto.
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
Ed egli stesso mi [sarà] in salvazione; Perciocchè l'ipocrita non gli verrà davanti.
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
Ascoltate attentamente il mio ragionamento; Ed [entrivi] negli orecchi la mia dichiarazione.
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
Ecco ora, [quando] io avrò esposta per ordine la mia ragione, Io so che sarò trovato giusto.
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
Chi è colui che voglia litigar meco? Conciossiachè di presente mi tacerò, e spirerò.
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
Sol non farmi due cose, [Ed] allora io non mi nasconderò dal tuo cospetto.
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
Allontana la tua mano d'addosso a me, E non mi spaventi il tuo terrore.
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
E poi chiama, ed io risponderò; Ovvero, io parlerò, e tu rispondimi.
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
Quante iniquità e peccati ho io? Mostrami il mio misfatto, e il mio peccato.
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
Perchè nascondi la tua faccia, E mi reputi tuo nemico?
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
Stritolerai tu una fronda sospinta? O perseguiterai tu della stoppia secca?
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
Che tu mi sentenzii a pene amare, E mi faccia eredar l'iniquità della mia fanciullezza!
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
E metta i miei piedi ne' ceppi, E spii tutti i miei sentieri, [E] stampi le tue pedate in su le radici de' miei piedi!
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
Onde costui si disfa come del legno intarlato, Come un vestimento roso dalle tignuole.

< Ayubu 13 >