< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Et Job, répondant, dit:
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
Ainsi vous, vous êtes les seuls hommes, et avec vous mourra la sagesse?
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
J’ai cependant un cœur comme vous, et je ne vous suis pas inférieur; qui, en effet, ignore ce que vous savez?
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
Celui qui est raillé par son ami comme moi invoquera Dieu, et Dieu l’exaucera; car la simplicité du juste est tournée en dérision.
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
C’est une lampe méprisée dans les pensées des riches, mais préparée pour un temps marqué.
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
Les tentes des voleurs sont dans l’abondance, et ils provoquent audacieusement Dieu, quoique ce soit lui qui ait mis toutes choses en leurs mains.
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
Certes, interroge les bêtes, et elles te l’enseigneront; et les volatiles du ciel, et ils te l’indiqueront.
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
Parle à la terre, et elle te répondra; et les poissons de la mer te le raconteront.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
Qui ignore que la main du Seigneur a fait toutes ces choses?
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
C’est dans sa main qu’est l’âme de tout vivant, et l’esprit de toute chair d’homme.
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
Est-ce que l’oreille ne discerne pas les paroles, et le palais de celui qui mange la saveur des aliments?
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
Dans les vieillards est la sagesse, et dans une longue vie la prudence.
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
En Dieu sont la sagesse et la force; c’est lui qui possède le conseil et la prudence.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
S’il détruit, il n’y a personne pour édifier; s’il enferme un homme, nul ne pourra lui ouvrir.
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
S’il retient les eaux, tout se desséchera; et, s’il les lâche, elles ravageront la terre.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
En lui sont la force et la sagesse: il connaît et celui qui trompe et celui qui est trompé.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
Il amène les conseillers à une fin insensée, et les juges à l’étourdissement.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
Il délie le baudrier des rois, et ceint leurs reins d’une corde.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
Il fait que les prêtres vont sans gloire, et il renverse les grands;
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
Changeant le langage des hommes véridiques, et enlevant la science des vieillards.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
Il verse le mépris sur les princes, en relevant ceux qui avaient été opprimés.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
C’est lui qui découvre les profondeurs des ténèbres, et produit à la lumière l’ombre de la mort.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
C’est lui qui multiplie les nations et les perd, et qui, après les avoir renversées, les rétablit entièrement.
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
C’est lui qui change le cœur des princes du peuple de la terre; qui les trompe, afin qu’ils marchent par où il n’y a point de voie.
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
Ils tâtonneront comme dans les ténèbres, et ils ne marcheront pas à la lumière, et il les fera chanceler comme des hommes ivres.

< Ayubu 12 >