< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Alors Job répondit,
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
« Sans doute, mais c'est vous qui êtes le peuple, et la sagesse mourra avec vous.
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
Mais j'ai de l'intelligence aussi bien que vous; Je ne suis pas inférieur à vous. Oui, qui ne connaît pas ce genre de choses?
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
Je suis comme celui qui se moque de son prochain, Moi, qui ai invoqué Dieu, et il m'a répondu. Le juste, l'homme irréprochable est une blague.
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
Dans la pensée de celui qui est à l'aise, il y a du mépris pour le malheur. Il est prêt pour ceux dont le pied glisse.
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
Les tentes des brigands prospèrent. Ceux qui provoquent Dieu sont en sécurité, qui portent leur dieu dans leurs mains.
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
« Mais demande maintenant aux animaux, et ils t'apprendront; les oiseaux du ciel, et ils vous le diront.
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
Ou bien parle à la terre, et elle t'enseignera. Les poissons de la mer te déclareront.
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
Qui ne sait pas que dans tout cela, La main de Yahvé a fait cela,
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
dans la main duquel se trouve la vie de tout être vivant, et le souffle de toute l'humanité?
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
L'oreille n'essaie pas les mots, même lorsque le palais goûte sa nourriture?
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
Avec les hommes âgés se trouve la sagesse, dans la compréhension de la durée des jours.
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
« La sagesse et la puissance sont auprès de Dieu. Il a le conseil et la compréhension.
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
Voici qu'il s'écroule, et il ne peut plus être reconstruit. Il emprisonne un homme, et il ne peut pas être libéré.
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
Voici, il retient les eaux, et elles tarissent. Encore une fois, il les envoie, et ils renversent la terre.
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
Avec lui, il y a la force et la sagesse. Le trompé et le trompeur sont à lui.
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
Il conduit les conseillers à l'écart, dépouillés. Il fait des juges des imbéciles.
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
Il délie les liens des rois. Il leur attache la taille avec une ceinture.
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
Il emmène les prêtres dépouillés, et renverse les puissants.
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
Il supprime la parole de ceux à qui l'on fait confiance, et enlève l'intelligence des anciens.
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
Il répand le mépris sur les princes, et détache la ceinture des forts.
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
Il découvre des choses profondes dans les ténèbres, et fait apparaître à la lumière l'ombre de la mort.
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
Il augmente les nations, et il les détruit. Il agrandit les nations, et il les conduit en captivité.
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
Il enlève l'intelligence aux chefs des peuples de la terre, et les fait errer dans un désert où il n'y a pas de chemin.
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
Ils tâtonnent dans l'obscurité, sans lumière. Il les fait tituber comme un homme ivre.

< Ayubu 12 >