< Ayubu 12 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
約伯回答說:
2 “Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
的確,只有你們是有知識的子民;那麼,你們一死,智慧也與你們一同喪亡!
3 Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
其實,我和你們有同樣的心理,我並不亞於你們! 誰不知道這些事﹖
4 Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
我這呼籲天主而蒙應允的人,卻被他的友人所嘲笑,無辜的義人卻成了笑柄。
5 Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
幸運的人心想:遭難的人應受蔑視,失足的人應再予以打擊。
6 Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
但是,強盜的帳幕竟能安全,觸怒天主的人,以勢力為神的人卻享平安。
7 Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
請你詢問走獸,牠們也會開導你;詢問天上的飛鳥,牠們也會告訴你;
8 Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
地上的爬蟲也會教訓你,海中的魚族也會給你說明。
9 Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
牠們中有誰不知道:是天主的手創造了這一切﹖
10 Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
因為一切活物的生魂,一切血肉之人的靈魂,都握在他手中。
11 Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
耳朵不是為明辨言語,口腔不是為辨嘗食物嗎﹖
12 Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
白髮老人是有智慧的,年紀大者是有見識的;
13 Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
但智慧和能力同在天主內,智慧與見識是天主所有。
14 Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
他若拆毀,人不能再建;他若拘禁,人不得開釋。
15 Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
他若制水,水便乾涸;他若放水,水便沖毀大地。
16 Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
力量與才能,為他所有;受騙者與騙人者,都屬於他。
17 Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
他使謀士糊塗,使判官愚蠢;
18 Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
他解除君王所繫的玉帶,將繩索捆在他們的腰間;
19 Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
他使司祭赤足而行,推倒掌握大權者;
20 Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
奪去忠貞者的辯才,剝去年老者的理智:
21 Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
使貴人備受侮辱,使勇士的腰帶鬆弛;
22 Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
使隱秘的事由暗處彰顯,使黑暗進入光明;
23 Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
使邦國興起而又滅亡,使民族強大而又消散;
24 Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
剝去國君的理智,使他們漂泊於無路的荒野中,
25 Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.
在無光的黑暗中摸索,踉蹌猶如醉漢。

< Ayubu 12 >