< Ayubu 11 >
1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
Alors Tsophar, de Naama, prit la parole, et dit:
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
Ne répondra-t-on point à tant de discours, et suffira-t-il d'être un grand parleur pour être justifié?
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
Tes vains propos feront-ils taire les gens? Te moqueras-tu, sans que personne te confonde?
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
Tu as dit: Ma doctrine est pure, je suis sans tache devant tes yeux.
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
Mais je voudrais que Dieu parlât, et qu'il ouvrît sa bouche pour te répondre;
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
Qu'il te montrât les secrets de sa sagesse, de son immense sagesse; et tu reconnaîtrais que Dieu oublie une partie de ton iniquité.
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
Trouveras-tu le fond de Dieu? Trouveras-tu la limite du Tout-Puissant?
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
Ce sont les hauteurs des cieux: qu'y feras-tu? C'est plus profond que les enfers: qu'y connaîtras-tu? (Sheol )
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
Son étendue est plus longue que la terre, et plus large que la mer.
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
S'il saisit, s'il emprisonne, s'il assemble le tribunal, qui l'en empêchera?
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
Car il connaît, lui, les hommes de rien; il voit l'iniquité, sans qu'elle s'en doute;
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
Mais l'homme vide de sens de-viendra intelligent, quand l'ânon sauvage naîtra comme un homme!
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
Si tu disposes bien ton cœur, et si tu étends tes mains vers Dieu,
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
(Si l'iniquité est en tes mains, éloigne-la, et que le crime n'habite point dans tes tentes! )
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
Alors certainement tu lèveras ton front sans tache; tu seras raffermi et tu ne craindras rien;
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
Tu oublieras tes peines, tu t'en souviendras comme des eaux écoulées.
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
La vie se lèvera pour toi plus brillante que le midi, et l'obscurité même sera comme le matin.
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
Tu seras plein de confiance, parce que tu auras lieu d'espérer; tu exploreras autour de toi, et tu te coucheras en sécurité;
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
Tu t'étendras à ton aise, et nul ne t'effraiera; et bien des gens te feront la cour.
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
Mais les yeux des méchants seront consumés; tout refuge leur sera ôté, et toute leur espérance sera de rendre l'âme.