< Ayubu 11 >

1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
Then Zophar the Naamathite answered and said,
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
“Should not such a multitude of words be answered? Should this man, so full of talk, be believed?
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
Should your boasting make others remain silent? When you mock, will no one make you feel ashamed?
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
For you say to God, 'My beliefs are pure, I am blameless in your eyes.'
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
But, oh, that God would speak and open his lips against you;
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
that he would show you the secrets of wisdom! For he is great in understanding. Know then that God demands from you less than your iniquity deserves.
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
Can you understand God by searching for him? Can you comprehend the Almighty perfectly?
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
The matter is as high as heaven; what can you do? It is deeper than Sheol; what can you know? (Sheol h7585)
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
Its measure is longer than the earth, and wider than the sea.
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
If he passes through and shuts anyone up, if he calls anyone to judgment, then who can stop him?
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
For he knows false people; when he sees iniquity, does he not notice it?
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
But foolish people have no understanding; they will get it when a wild donkey gives birth to a man.
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
But suppose that you had set your heart right and had reached out with your hands toward God;
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
suppose that iniquity were in your hand, but that then you put it far away from you, and did not let unrighteousness live in your tents.
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
Then you would certainly lift up your face without a sign of shame; indeed, you would be steadfast and would not fear.
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
You would forget your misery; you would remember it only like waters that have flowed away.
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
Your life would be brighter than the noonday; though there were darkness, it would become like the morning.
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
You would be secure because there is hope; indeed, you would find safety about you and would take your rest in safety.
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
Also you would lie down in rest, and none would make you afraid; indeed, many would seek your favor.
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
But the eyes of wicked people will fail; they will have no way to flee; their only hope will be a last gasp of life.”

< Ayubu 11 >