< Ayubu 11 >
1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
and to answer Zophar [the] Naamathite and to say
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
abundance word not to answer and if: surely no man lip: words to justify
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
bluster your man be quiet and to mock and nothing be humiliated
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
and to say pure teaching my and pure to be in/on/with eye your
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
and but who? to give: if only! god to speak: speak and to open lips his with you
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
and to tell to/for you secret wisdom for double to/for wisdom and to know for to forget to/for you god from iniquity: guilt your
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
search god to find if: surely no till limit Almighty to find
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
height heaven what? to work deep from hell: Sheol what? to know (Sheol )
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
long from land: country/planet garment her and broad: wide from sea
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
if to pass and to shut and to gather and who? to return: return him
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
for he/she/it to know man vanity: false and to see: see evil: wickedness and not to understand
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
and man be hollow to encourage and colt wild donkey man to beget
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
if you(m. s.) to establish: prepare heart your and to spread to(wards) him palm your
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
if evil: wickedness in/on/with hand your to remove him and not to dwell in/on/with tent your injustice
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
for then to lift: kindness face: kindness your from blemish and to be to pour: firm and not to fear
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
for you(m. s.) trouble to forget like/as water to pass to remember
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
and from midday to arise: establish lifetime/world gloom like/as morning to be
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
and to trust for there hope and to search to/for security to lie down: sleep
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
and to stretch and nothing to tremble and to beg face of your many
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
and eye wicked to end: expend and refuge to perish from them and hope their exhalation soul: life