< Ayubu 11 >
1 Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
Then answered Zophar the Naamathite, and sayde,
2 “Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
Should not the multitude of wordes be answered? or should a great talker be iustified?
3 Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
Should men holde their peace at thy lyes? and when thou mockest others, shall none make thee ashamed?
4 Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
For thou hast sayde, My doctrine is pure, and I am cleane in thine eyes.
5 Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
But, oh that God would speake and open his lippes against thee!
6 hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
That he might shewe thee the secretes of wisedome, howe thou hast deserued double, according to right: know therefore that God hath forgotten thee for thine iniquitie.
7 Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
Canst thou by searching finde out God? canst thou finde out ye Almighty to his perfection?
8 Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
The heauens are hie, what canst thou doe? it is deeper then the hell, how canst thou know it? (Sheol )
9 Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
The measure thereof is longer then the earth, and it is broader then the sea.
10 kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
If hee cut off and shut vp, or gather together, who can turne him backe?
11 Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
For hee knoweth vaine men, and seeth iniquitie, and him that vnderstandeth nothing.
12 Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
Yet vaine man would be wise, though man new borne is like a wilde asse colte.
13 Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
If thou prepare thine heart, and stretch out thine hands toward him:
14 ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
If iniquitie be in thine hand, put it farre away, and let no wickednesse dwell in thy Tabernacle.
15 Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
The truely shalt thou lift vp thy face without spot, and shalt be stable, and shalt not feare.
16 Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
But thou shalt forget thy miserie, and remember it as waters that are past.
17 Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
Thine age also shall appeare more cleare then the noone day: thou shalt shine and bee as the morning.
18 Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
And thou shalt bee bolde, because there is hope: and thou shalt digge pittes, and shalt lye downe safely.
19 Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
For when thou takest thy rest, none shall make thee afraide: yea, many shall make sute vnto thee.
20 Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.
But the eyes of the wicked shall faile, and their refuge shall perish, and their hope shalbe sorow of minde.