< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
taedet animam meam vitae meae dimittam adversum me eloquium meum loquar in amaritudine animae meae
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
dicam Deo noli me condemnare indica mihi cur me ita iudices
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
numquid bonum tibi videtur si calumnieris et opprimas me opus manuum tuarum et consilium impiorum adiuves
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
numquid oculi carnei tibi sunt aut sicut videt homo et tu videbis
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
numquid sicut dies hominis dies tui et anni tui sicut humana sunt tempora
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
ut quaeras iniquitatem meam et peccatum meum scruteris
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
et scias quia nihil impium fecerim cum sit nemo qui de manu tua possit eruere
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
manus tuae plasmaverunt me et fecerunt me totum in circuitu et sic repente praecipitas me
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
memento quaeso quod sicut lutum feceris me et in pulverem reduces me
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
nonne sicut lac mulsisti me et sicut caseum me coagulasti
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
pelle et carnibus vestisti me et ossibus et nervis conpegisti me
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
vitam et misericordiam tribuisti mihi et visitatio tua custodivit spiritum meum
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
licet haec celes in corde tuo tamen scio quia universorum memineris
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
si peccavi et ad horam pepercisti mihi cur ab iniquitate mea mundum me esse non pateris
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
et si impius fuero vae mihi est et si iustus non levabo caput saturatus adflictione et miseria
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
et propter superbiam quasi leaenam capies me reversusque mirabiliter me crucias
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
instauras testes tuos contra me et multiplicas iram tuam adversum me et poenae militant in me
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
quare de vulva eduxisti me qui utinam consumptus essem ne oculus me videret
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
fuissem quasi qui non essem de utero translatus ad tumulum
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
numquid non paucitas dierum meorum finietur brevi dimitte ergo me ut plangam paululum dolorem meum
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
antequam vadam et non revertar ad terram tenebrosam et opertam mortis caligine
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
terram miseriae et tenebrarum ubi umbra mortis et nullus ordo et sempiternus horror inhabitans