< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
わが心生命を厭ふ 然ば我わが憂愁を包まず言あらはし わが魂神の苦きによりて語はん
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
われ神に申さん 我を罪ありしとしたまふ勿れ 何故に我とあらそふかを我に示したまへ
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
なんぢ虐遇を爲し 汝の手の作を打棄て惡き者の謀計を照すことを善としたまふや
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
汝は肉眼を有たまふや 汝の觀たまふ所は人の觀るがごとくなるや
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
なんぢの日は人間の日のごとく 汝の年は人の日のごとくなるや
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
何とて汝わが愆を尋ねわが罪をしらべたまふや
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
されども汝はすでに我の罪なきを知たまふ また汝の手より救ひいだし得る者なし
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
汝の手われをいとなみ我をことごとく作れり 然るに汝今われを滅ぼしたまふなり
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
請ふ記念たまへ 汝は土塊をもてすてるがごとくに我を作りたまへり 然るに復われを塵に歸さんとしたまふや
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
汝は我を乳のごとく斟ぎ牛酪のごとくに凝しめたまひしに非ずや
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
汝は皮と肉とを我に着せ骨と筋とをもて我を編み
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
生命と恩惠とをわれに授け我を眷顧てわが魂神を守りたまへり
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
然はあれど汝これらの事を御心に藏しおきたまへり 我この事汝の心にあるを知る
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
我もし罪を犯さば汝われをみとめてわが罪を赦したまはじ
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
我もし行状あしからば禍あらん 假令われ義かるとも我頭を擧じ 其は我は衷に羞耻充ち 眼にわが患難を見ればなり
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
もし頭を擧なば獅子のごとくに汝われを追打ち 我身の上に復なんぢの奇しき能力をあらはしたまはん
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
汝はしばしば證する者を入かへて我を攻め 我にむかひて汝の震怒を増し新手に新手を加へて我を攻めたまふ
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
何とて汝われを胎より出したまひしや 然らずば我は息絶え目に見らるること無く
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
曾て有ざりし如くならん 即ち我は胎より墓に持ゆかれん
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
わが日は幾時も无きに非ずや 願くは彼姑らく息て我を離れ我をして少しく安んぜしめんことを
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
我が往て復返ることなきその先に斯あらしめよ 我は暗き地死の蔭の地に往ん
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
この地は暗くして晦冥に等しく死の蔭にして區分なし 彼處にては光明も黑暗のごとし