< Ayubu 10 >

1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
Ma vie donne à mon cœur du dégoût: je veux me soulager, donner cours à mes plaintes, et parler dans l'amertume de mon âme.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
Je dis à Dieu: Ne me condamne pas! Déclare-moi sur quoi tu me prends à partie!
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Est-ce un bonheur pour toi de me maltraiter, de rejeter l'ouvrage de tes mains, et de prêter la lumière aux complots des impies?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
As-tu des yeux de chair? vois-tu, comme voient les mortels?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Tes jours sont-ils comme les jours des mortels. et tes années, comme celles des humains,
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
que tu fais une enquête de ma faute, et une perquisition de mon péché,
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
sachant bien que je ne suis pas coupable, et que nul ne peut sauver de ta main?
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Tes mains m'ont façonné, m'ont fait, en entier; et tu veux me détruire!
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Ah! souviens-toi que tu m'as modelé comme l'argile! et dans la poudre tu veux me faire rentrer!
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Ne m'as-tu pas versé comme du lait? comme le caillé ne m'as-tu pas fait prendre?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
De peau et de chair tu m'as revêtu, d'os et de nerfs tu m'as tissé,
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
tu m'as donné la vie et la grâce, tes soins ont protégé ma respiration:
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
et tu me réservais ces maux dans ton cœur! Je sais qu'ils étaient dans ta pensée.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
Au cas que je péchasse, tu voulais m'épier, et ne point m'absoudre de ma faute.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
Suis-je coupable? malheur à moi! innocent? je n'ose lever la tête, rassasié d'opprobre, et voyant ma misère;
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
qu'elle se lève, tu vas, tel qu'un lion, me donner la chasse, et renouveler sur moi tes miracles,
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
m'opposer de nouveaux témoins, redoubler ta fureur contre moi, et faire contre moi se succéder les bataillons.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Ah! pourquoi me tiras-tu du sein de ma mère? Je serais expiré, et aucun œil ne m'eût vu;
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
je serais comme n'ayant pas été; du ventre au tombeau j'aurais été porté.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Qu'ai-je, sinon quelques jours? Qu'Il cesse! se retire de moi, pour que je me rassérène un peu,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
avant que je m'en aille, pour ne plus revenir, dans la région des ténèbres et de l'ombre de mort,
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
région sombre comme la nuit, d'ombre de mort et de désordre, où la clarté ressemble aux ténèbres!

< Ayubu 10 >