< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
Yt anoieth my soule of my lijf; Y schal lete my speche ayens me, Y schal speke in the bitternesse of my soule.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
Y schal seie to God, Nyle thou condempne me; schewe thou to me, whi thou demest me so.
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Whether it semeth good to thee, if thou `falsli chalengist and oppressist me, the werk of thin hondis; and if thou helpist the counsel of wickid men?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Whethir fleischli iyen ben to thee, ethir, as a man seeth, also thou schalt se?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Whether thi daies ben as the daies of man, and `thi yeeris ben as mannus tymes;
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
that thou enquere my wickidnesse, and enserche my synne?
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
And wite, that Y haue do no `wickid thing; sithen no man is, that may delyuere fro thin hond?
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Thin hondis han maad me, and han formed me al in cumpas; and thou castist me doun so sodeynli.
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Y preye, haue thou mynde, that thou madist me as cley, and schalt brynge me ayen in to dust.
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Whether thou hast not mylkid me as mylk, and hast cruddid me togidere as cheese?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
Thou clothidist me with skyn and fleisch; thou hast ioyned me togidere with boonys and senewis.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
Thou hast youe lijf and mercy to me, and thi visiting hath kept my spirit.
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
Thouy thou helist these thingis in thin herte, netheles Y woot, that thou hast mynde of alle thingis.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
If Y dide synne, and thou sparidist me at an our; whi suffrist thou not me to be cleene of my wickidnesse?
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
And if Y was wickid, wo is to me; and if Y was iust, Y fillid with turment and wretchidnesse `schal not reise the heed.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
And if Y reise `the heed for pride, thou schalt take me as a lionesse; and thou turnest ayen, and turmentist me wondirli.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
Thou gaderist in store thi witnessis ayens me, and thou multipliest thin yre, `that is, veniaunce, ayens me; and peynes holden knyythod in me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Whi hast thou led me out of the wombe? `And Y wolde, that Y were wastid, lest an iye `schulde se me.
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
That Y hadde be, as if Y were not, and `were translatid, ethir borun ouer, fro the wombe to the sepulcre.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Whether the fewnesse of my daies schal not be endid in schort? Therfor suffre thou me, that Y biweile `a litil my sorewe,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
bifor that Y go, and turne not ayen, to the derk lond, and hilid with the derknesse of deth, to the lond of wrecchidnesse and of derknessis;
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
where is schadewe of deeth, and noon ordre, but euerlastynge hidousnesse dwellith.