< Ayubu 10 >

1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
“I am tired of living. And I will not be silent and stop saying what I am complaining about. Instead, being very unhappy, I will speak [IDM].
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
I will say to God, ‘Do not say that I must be punished; instead, tell me what wrong you are saying that I have done.
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Does it seem to be good for you to oppress me, to abandon me, whom you created, and instead, to help wicked people to do the things that they plan to do?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Do you understand things the way that we humans do?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
(Do you live for only a few years, like we do?/You certainly do not live for only a few years, like we do.) [RHQ]
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
So, why do you [RHQ] continue to search for my faults? Why do you hunt for my sins?
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
You know that I am not guilty, and that no one can rescue me from your power [MTY].
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
“'With your hands you created me and shaped/formed my body; but now you are [deciding that you should not have done that, and you are] destroying me.
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Do not forget that you made me from [a piece of] clay; are you going to cause me to become dirt again [RHQ]?
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
You certainly [RHQ] directed/controlled it when I was conceived, and you formed me inside my mother’s womb [MET].
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
You fastened my bones together with sinews, and [then] you covered them with flesh inside my skin.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
You have caused me to be alive, and you have faithfully loved me, and you have carefully (preserved me/kept me alive).
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
“'But you (kept secret/did not reveal) what [you were planning to do to me]; I am certain that you were planning [to do] these [things to me].
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
You were watching to see if I would sin, in order that [if I sinned, ] you would refuse to forgive me.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
If I am a wicked man, I hope/wish that terrible things will happen to me. But even if I am righteous, I still must bow my head [and feel ashamed], because I am very disgraced and feel miserable.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
And if I am proud, you hunt me like [SIM] a lion hunts [for some animal to kill], and you act powerfully to injure me.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
You constantly find more witnesses [to testify that I have done what is wrong], and you continually become more angry/perturbed with me. [It is as though] you are always bringing new troops to attack me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
“'God, why did you allow me to be born? I wish/desire that I had died before anyone [SYN] saw me.
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
[I consider that] it would have been better if I had been carried directly from my mother’s womb to the grave than for me to live.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
[I think that] [RHQ] there are only a few days for me to remain alive; so (allow me to be alone/stop attacking me), in order that I may be a little cheerful
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
before I go to the place from which I will never return, where it is always gloomy and very dark [DOU],
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
a place of darkness and dark shadows, where [everything] is confused/disordered, where [even a small amount of] light there is like darkness (OR, there is no light, only darkness).’”

< Ayubu 10 >