< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
I am weary of my life; I will let loose within me my complaint; I will speak in the bitterness of my soul.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
I will say unto God, Do not condemn me! Show me wherefore thou contendest with me!
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Is it a pleasure to thee to oppress, And to despise the work of thy hands, And to shine upon the plans of the wicked?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Hast thou eyes of flesh, Or seest thou as man seeth?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Are thy days as the days of a man, Are thy years as the days of a mortal,
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
That thou seekest after my iniquity, And searchest after my sin,
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
Though thou knowest that I am not guilty, And that none can deliver from thy hand?
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Have thy hands completely fashioned and made me In every part, that thou mightst destroy me?
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
O remember that thou hast moulded me as clay! And wilt thou bring me again to dust?
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Thou didst pour me out as milk, And curdle me as cheese;
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
With skin and flesh didst thou clothe me, And strengthen me with bones and sinews;
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
Thou didst grant me life and favor, And thy protection preserved my breath:
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
Yet these things thou didst lay up in thy heart! I know that this was in thy mind.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
If I sin, then thou markest me, And wilt not acquit me of mine iniquity.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
If I am wicked, —then woe unto me! Yet if righteous, I dare not lift up my head; I am full of confusion, beholding my affliction.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
If I lift it up, like a lion thou huntest me, And again showest thyself terrible unto me.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
Thou renewest thy witnesses against me, And increasest thine anger toward me; New hosts continually rise up against me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Why then didst thou bring me forth from the womb? I should have perished, and no eye had seen me;
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
I should be as though I had not been; I should have been borne from the womb to the grave.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Are not my days few? O spare then, And let me alone, that I may be at ease a little while,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
Before I go— whence I shall not return—To the land of darkness and death-shade,
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
The land of darkness like the blackness of death-shade, Where is no order, and where the light is as darkness.