< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
“My soul has been weary of my life, I leave off my talking to myself, I speak in the bitterness of my soul.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
I say to God, Do not condemn me, Let me know why You strive [with] me.
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Is it good for You that You oppress? That You despise the labor of Your hands, And shine on the counsel of the wicked?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Do you have eyes of flesh? Do You see as man sees?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
[Are] Your days as the days of man? Your years as the days of a man?
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
That You inquire for my iniquity, And seek for my sin?
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
For You know that I am not wicked, And there is no deliverer from Your hand.
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Your hands have taken pains about me, And they make me together all around, And You swallow me up!
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Please remember That You have made me as clay, And You bring me back to dust.
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Do You not pour me out as milk? And curdle me as cheese?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
Skin and flesh You put on me, And fence me with bones and sinews.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
Life and kindness You have done with me. And Your inspection has preserved my spirit.
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
And these You have laid up in Your heart, I have known that this [is] with You.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
If I sinned, then You have observed me, And do not acquit me from my iniquity,
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
If I have done wickedly—woe to me, And righteously—I do not lift up my head, Full of shame—then see my affliction,
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
And it rises—as a lion You hunt me. And You turn back—You show Yourself wonderful in me.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
You renew Your witnesses against me, and multiply Your anger with me, Changes and warfare [are] with me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
And why from the womb Have You brought me forth? I expire, and the eye does not see me.
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
I am as [if] I had not been, I am brought from the belly to the grave,
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Are my days not few? Cease then, and put from me, And I brighten up a little,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
Before I go, and do not return, To a land of darkness and death-shade,
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
A land of obscurity as thick darkness, Death-shade—and no order, And the shining [is] as thick darkness.”