< Ayubu 10 >

1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
Weary in my soul, I will pour my words with groans upon him: I will speak being straitened in the bitterness of my soul.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
And I will say to the Lord, Do not teach me to be impious; and therefore have you thus judged me?
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Is it good before you if I be unrighteous? for you have disowned the work of your hands, and attended to the counsel of the ungodly.
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Or do you see as a mortal sees? or will you look as a man sees?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Or is your life human, or your years [the years] of a man,
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
that you have enquired into mine iniquity, and searched out my sins?
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
For you know that I have not committed iniquity: but who is he that can deliver out of your hands?
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Your hands have formed me and made me; afterwards you did change [your mind], and strike me.
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Remember that you have made me [as] clay, and you do turn me again to earth.
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Hast you not poured me out like milk, and curdled me like cheese?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
And you did clothe me with skin and flesh, and frame me with bones and sinews.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
And you did bestow upon me life and mercy, and your oversight has preserved my spirit.
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
Having these things in yourself, I know that you can do all things; for nothing is impossible with you.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
And if I should sin, you watch me; and you have not cleared me from iniquity.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
Or if I should be ungodly, woe is me: and if I should be righteous, I can’t lift myself up, for I am full of dishonor.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
For I am hunted like a lion for slaughter; for again you have changed and are terribly destroying me;
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
renewing against me my torture: and you have dealt with me in great anger, and you have brought trials upon me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Why then did you bring me out of the womb? and why did I not die, and no eye see me,
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
and I become as if I had not been? for why was I not carried from the womb to the grave?
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Is not the time of my life short? suffer me to rest a little,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
before I go whence I shall not return, to a land of darkness and gloominess;
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
to a land of perpetual darkness, where there is no light, neither [can any one] see the life of mortals.

< Ayubu 10 >