< Yeremia 1 >

1 Hili ndilo neno la Yeremia mwana wa Hilikia; yeye alikuwa mmoja wa makuhani kule Anatothi katika nchi ya Benjamini.
Paroles de Jérémie, fils de Hilkija, l'un des prêtres qui étaient à Anathoth, dans le pays de Benjamin.
2 Neno la BWANA lilimjia katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wake.
La parole de Yahvé lui fut adressée au temps de Josias, fils d'Amon, roi de Juda, la treizième année de son règne.
3 Lakini pia lilimjia katika wakati wa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka mwezi wa tano wa mwaka wa kumi na moja wa Zedekia mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, wakati watu wa Yerusalemu walipochukuliwa kuwa watumwa.
Elle arriva aussi aux jours de Jojakim, fils de Josias, roi de Juda, à la fin de la onzième année de Sédécias, fils de Josias, roi de Juda, jusqu'à la déportation de Jérusalem au cinquième mois.
4 Neno la BWANA lilinijia, likisema,
Or la parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes,
5 “kabla sijakuumba tumboni, Nilikuchagua; kabla hujazailiwa toka tumboni Nilikutenga; Nilikufanya kuwa nabii kwa mataifa.”
« Avant de te former dans le ventre de ta mère, je te connaissais. Avant ta naissance, je t'ai sanctifié. Je t'ai établi prophète des nations. »
6 “Ahaa, BWANA!” Nilisema, “mimi sijui kusema, kwa kuwa mimi ni mtoto.”
Et je dis: « Ah! Seigneur Yahvé! Voici, je ne sais pas comment parler, car je suis un enfant. »
7 Lakini BWANA akaniambia, “Usiseme, 'mimi ni mtoto.' Utaenda kila mahali ninapokutuma, na utasema kila kitu ninachokuamuru!
Mais Yahvé me dit: « Ne dis pas: « Je suis un enfant », car tu iras vers celui que je t'enverrai, et tu diras tout ce que je te commanderai.
8 Usiwaogpe hao, kwa kuwa Mimi niko pamoja na wewe kukuokoa- asema BWANA.”
N'aie pas peur à cause d'eux, car je suis avec toi pour te sauver, dit l'Éternel.
9 Kisha BWANA akanyosh mkono wake, akagusa kinywa changu, na akaniambia, “Nimeweka maneno yangu kinywani mwako.
Alors Yahvé étendit sa main et toucha ma bouche. Et Yahvé me dit: « Voici, j'ai mis mes paroles dans ta bouche.
10 Nimekuchagua leo juu ya mataifa na juu ya mataifa, ili kung'oa na kuvunja, kuharibu na kutupa, kujenga na kupanda.”
Voici, je t'ai établi aujourd'hui sur les nations et sur les royaumes, pour arracher et démolir, pour détruire et renverser, pour bâtir et planter. »
11 Neno la BWANA lilinijia, likisema, “Yeremia, unaona nini?” Nikasema, “Ninaona tawi la mlozi.”
La parole de Yahvé me fut adressée en ces termes: « Jérémie, que vois-tu? » J'ai dit: « Je vois une branche d'amandier. »
12 BWANA akaniambia, “umeona vyema, kwa kuwa ninaliangalia neno langu ili nilitimize.”
Et Yahvé me dit: « Tu as bien vu, car je veille sur ma parole pour l'accomplir. »
13 Neno la BWANA likaniji mara ya pili likisema, “Unaona nini? “Nikasema, “Ninaona chungu kikichemuka, ambacho mdomo wake unaelekea toka upande wa kaskazini,”
La parole de Yahvé me fut adressée pour la seconde fois, en disant: « Que vois-tu? » J'ai dit: « Je vois un chaudron en ébullition, et il bascule vers le nord. »
14 BWANA akaniambia, “Janga litatokea kaskazini juu ya wote wanaoishi katika nchi hii.
Alors Yahvé me dit: « Du nord, le mal se répandra sur tous les habitants du pays.
15 Kwa kuwa ninayaita makabila yote ya falme za kaskazini, asema BWANA. Yatakuja, na kila mmoja atasimika enzi yake katika malango ya Yerusalemu, dhidi ya kuta zote zinazoizunguka, na dhidi ya miji ya Yuda.
Car voici, j'appellerai toutes les familles des royaumes du nord, dit l'Éternel. « Ils viendront, et ils placeront chacun leur trône à l'entrée des portes de Jérusalem, et contre toutes ses murailles tout autour, et contre toutes les villes de Juda.
16 Nitatamka hukumu dhidi yao juu ya uovu wao wa kuniacha, kwa kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kwa kuabudu kile walichotengeneza kwa mikono yao.
Je prononcerai contre eux mes jugements sur toute leur méchanceté, en ce qu'ils m'ont abandonné, et ont brûlé de l'encens à d'autres dieux, et adoraient les œuvres de leurs propres mains.
17 Jiandae! Simama ukawaambie kila kitu ninachokuamuru. Usifdhaike mbele zao nisije nikakufadhaisha wewe mbele zao!
« Mets donc ta ceinture à ta taille, lève-toi, et dis-leur tout ce que je t'ordonne. Ne t'effraie pas devant eux, de peur que je ne t'effraie devant eux.
18 Tazama! Leo nimekufanya kuwa mji ulio na ngome, kuwa ngome ya chuma, na ukata wa shaba dhidi ya nchi yote - dhidi ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wote wa nchi.
Car voici, je fais de toi aujourd'hui une ville fortifiée, une colonne de fer et des murs de bronze contre tout le pays, contre les rois de Juda, contre ses princes, contre ses prêtres et contre le peuple du pays.
19 Watapigana na wewe, lakinai hawatakushinda, kwa kuwa nitakuwa pamoja na wewe ili kukuokoa- asema BWANA.”
Ils te combattront, mais ils ne te vaincront pas, car je suis avec toi, dit l'Éternel, pour te secourir. »

< Yeremia 1 >