< Yeremia 9 >

1 Kama kichwa changu kingetoa maji, na macho yangu kuwa chemichemi ya machozi! kwa kuwa natamani kulia usiku na mchana kwa ajili yao waliokuwa binti za watu wangu ambao wameuawa.
I wish that my head was [like] [MET] a spring of water, and that my eyes were [like] a fountain of tears. Then I would cry night and day for all of my people who have been killed [by our enemies].
2 Kama mtu anganipatia mahali pa wasafiri nyikani ili nikae, mahali ambapo ningeenda kuwatelekeza watu wangu. Kama ningewaacha, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la wenye hiana!
I wish that I could leave my people and forget them, and go and live in a shack/shelter in the desert, because they have not remained faithful [MET] [to Yahweh]; they are a mob of people who deceive others.
3 asema BWANA, “Huupinda ulimi wao kana kwamba ni upinde ili wapate kuongea uongo, lakini si kwa uamiinifu wao kwamba wanapata nguvu duniani. Wanatoka uovu mmoja hadi mwiingine. Hawanijui mimi.”
[Yahweh replied to me], “They use their tongues [to tell] [MET] lies like people shoot [arrows] with bows. It is because they tell lies that they have become more powerful in this land, and they do not know me.
4 Kila mmoja wenu, awe mlinzi wa jirani yake na usimwamini hata ndugu yako yeyote. kwa kuwa kila ndugu ni mwongo,
Do not trust your neighbors and [even] your brothers! They all are as deceitful [as Jacob was]. They slander [each other] and tell lies [about each other].
5 kila jirani anatembea akilaghai. Kila mwanamume anakejeli jirani yake na haongei ukweli. Ndimi zao hufundisha vitu vya uongo. Hujidhofisha ili kusema uongo.
They deceive their friends and never tell the truth. They lie continually and, because of that, they have become skilled liars; they do one oppressive thing after another, and are unable to stop doing it.
6 Makazi yenu yako kati ya udanganyifu; kwa uongo wao wanakataa kunitambua mimi. Asema BWANA.”
They habitually lie and deceive [each other], and no one will admit/say that I am God.
7 Kwa hiyo BWANA wa majeshi asema hivi, “Tazama, Niko tayari kuwajaribu. Nitawajaribu nione. Jinsi gani niwezavyo kufanya kwa binti za watu wangu?
Therefore [I], the Commander of the armies of angels, say this: Listen carefully to what I say: I will [cause my people to experience great afflictions, ] [like a metalworker puts metal in a hot fire] [MET] to completely burn out the impure bits. Because of all [the evil things] that my people have done, there is absolutely nothing else [RHQ] that I can do.
8 Ndimi zao ni mishale iliyochongoka; huongea vitu vya uasi. Kwa midomo yao wanatangaza amani pamoja na jirani zao, lakini katika mioyo yao wanadanganya wakati wa kusubri.
What they say [MTY] [injures people like] [MET] poisoned arrows do. They say to their neighbors, ‘I hope things will go well for you,’ while they are planning to kill them.
9 Kwa nini nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya - asema BWANA na kwa nini nisijilipizie kisasi kwa taifa ambalo liko kama hili?
Should I not punish them for doing that [RHQ]? Yes, I should certainly (get revenge on/give what they deserve to) [the people of] a nation that does things like that!”
10 Nitaimba wimbo wa kuomboleza na kulia kwa ajili ya milima, na wimbo wa mazishi utaimbwa nyikani. Kwa kuwa wameteketezwa kwa hiyo hakuna anAyeweza kupita kati kati yao. Hawatasikia sauti ya ng'ombe yeyote. Ndege wa angani na wanyama wote wamekimbia.
So, I will weep and wail for [the people who live in] the mountains and in the (pastures/places where the livestock eat the grass), because those areas will be desolate, and no one will live there. There will be no cattle there to call to each other, and all the birds and wild animals will have fled [to other places].
11 Kwa hiyo nitaigeuza Yerusalemu kuwa vifusi vya ukiwa, maficho ya mbweha. Nitaifanya miji ya Yuda kuwa miji iliyoharibiwa isiyokaliwa na watu.
[Yahweh also says], “I will cause Jerusalem to become a heap of ruins, and [only] jackals/wolves will live there. I will destroy the towns of Judah, with the result that they will be completely deserted; no one will live there.”
12 Ni nani mwenye hekima anayeyaelewa haya? Je, kinywa cha BWANA kinatangaza nini kwake ili aweze kuyasema? Kwa nini nchi imepotea? Imeharibiwa kama jangwa, ambapo hakuna apitaye kati kati yake.
[I said], “Only people who are very wise [RHQ] can understand these things. Only those who have been taught by Yahweh can [RHQ] explain these things to others. The wise people are [RHQ] the only ones who can explain why the land will be completely ruined with the result that everyone [RHQ] will be afraid to travel through it.”
13 BWANA asema, “Ni kwa sababu wameziacha sheria zake ambazo niliwatengenezea, kwa sababu hawaisikilizi sauti yangu au kuishi kwa kuifuta.
Yahweh replied, “[These things will happen] because my people have rejected my laws which I gave to them; they have not obeyed me or my instructions.
14 Ni kwa sababu wameishi kwa ushupavu wa mioyo yao na wamewafuata Mabaali kama baba zao walivyowafundisha kufanya.
Instead, they have stubbornly done the things that they wanted to do. They have worshiped the idols that represent the god Baal, which is what their ancestors did.
15 Kwa hiyo BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Tazama, Ninataka kuwafanya hawa watu wale pakanga na kunywa maji ya sumu.
So now listen to what [I], the Commander of the armies of angels, the God of the Israelis, say: [What I will do will be like] [MET] giving these people bitter things to eat and poison to drink:
16 Ndipo nitakapowasambaza kati ya mataifa ambayo hawajayajua, wao wala mababu zao. Nitatuma upanga kwa ajili yao mpaka nimewaangamiza wote kabisa.'”
I will scatter them to many nations which neither they nor their ancestors have known [anything about]; I will [enable their enemies to] strike them with swords until I have destroyed them.”
17 BWANA wa majeshi asema hivi, “Yafikirini haya: Waiteni waliaji; waje. Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza, waje.
This is also what the Commander of the armies of angels says: “Think [about what is happening], [then] summon those women who mourn [when someone has died].
18 Waje haraka waimbe wimbo wa maombolezo juu yetu, ili macho yetu yatokwe na machozi na kope zetu zibubujikwe na maji.
Tell them to come quickly and start to wail, with the result that tears will stream down from your(pl) eyes.
19 Kwa kuwa sauti ya kilio imesikika Sayuni, 'Jinsi tulivyoharibiwa. Tumeaibishwa sana, kwa kuwa tumeitelekeza nchi tangu walIpoangusha nyumba zetu.'
Listen to [the people of] Jerusalem crying/lamenting, saying, ‘We have been ruined/destroyed! We have experienced a terrible disaster! Now we are very ashamed, because our houses have been destroyed [by our enemies], and we [are being forced to] leave our land.’”
20 Kwa hiyo ninyi wanawake, sikieni neno la BWANA; zingatieni ujumbe unaokuja toka kinywani mwake. Kisha wafundisheni binti zenu wimbo wa maombolezo, na kila mwanamke wa jirani wimbo wa kilio.
You women, listen to what Yahweh says [MTY]. Pay attention to his words [DOU]. Teach your daughters to wail. Teach each other how to sing funeral songs,
21 Kwa kuwa vifo vimekuja kupitia dirishani; vinaelekea mahali petu. Vinawaharibu watoto kutoka nje na vijana kwenye viwanja vya miji.
because people will be dying [PRS] in your houses and in palaces. There will be no more children playing in the streets, there will be no more young men [gathering] in the city squares/marketplaces.
22 Uyatangaze haya, 'Asema BWANA - mizoga ya wanaume itaanguka kama mavi kwenye mashamba na kama mabua baada ya mvunaji, na hapatakuwa na mtu wa kuyakusanya.'”
There will be corpses scattered across the fields like dung; their dead bodies will lie there like [SIM] grain that has been cut by reapers/farmers, and there will be no one [still alive] to bury them.
23 BWANA asema hivi, “Usimwache mtu mwenye busara ajivune kwa ajili ya hekima yake, au shujaa kwa sababu ya uwezo wake. Usimwache mtu tajiri ajivunie utajiri wake.
Yahweh says this: “Wise men should not boast about their being wise, strong men should not boast about their being strong; and rich people should not boast about their being rich.
24 Kwa kuwa kama mtu atajivunia chochote kile, acha iwe hivi, yeye awe na busra na kunijua mimi. Kwa kuwa mimi ni BWANA, atendaye katika agano la wema, haki, na hukumu duniani. Ni katika hili kwamba ninafurahia- asema BWANA.
Instead, those who want to boast should boast about their knowing me and about understanding that I am Yahweh, that I am kind and just and righteous, that I faithfully love [people], and that I am delighted with [people who act] that way.
25 Tazama, siku zaja - asema BWANA wakati nitakapowaadhibu wote ambao hawajatahiriwa ambao wako hivyo hivyo katika miili yao.
There will be a time when I will punish all those people of Egypt and of the Moab people-group and of the Edom [people-group] and of the Ammon [people-group], all those people who live close to desert areas (OR, who cut their hair short [to please their gods]) far from Judah, all those people who have [changed their bodies by] circumcising them [MET] but who have not [changed] their inner beings. I will punish the people of Judah also, because they have not changed their inner beings, [either].”
26 Nitaiadhibu Misri na Yuda, Edomu, watu wa Amoni, Moabu, na watu wote wanaonyoa denge. Kwani mataifa yote haya hayajatahiriwa, na nyumba yote ya Israeli ina moyo ambao haujatahiriwa.”

< Yeremia 9 >