< Yeremia 51 >
1 Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
Yahvé dice: “He aquí que yo me levantaré contra Babilonia, y contra los que habitan en Lebkamai, un viento destructor.
2 Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
Enviaré a Babilonia extraños que la aventarán. Vaciarán su tierra; porque en el día de la angustia estarán contra ella todos.
3 Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
Contra el que se dobla, que el arquero doble su arco, también contra el que se levanta con su cota de malla. ¡No le perdonen los jóvenes! ¡Destruyan por completo a todo su ejército!
4 Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
Caerán muertos en la tierra de los caldeos, y se empuja a través de sus calles.
5 Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
Porque Israel no está abandonado, ni Judá, por su Dios, por Yahvé de los Ejércitos; aunque su tierra está llena de culpa contra el Santo de Israel.
6 Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
“¡Huye de en medio de Babilonia! ¡Todo el mundo salva su propia vida! No seas cortado en su iniquidad, porque es el tiempo de la venganza de Yahvé. Él le dará una recompensa.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
Babilonia ha sido una copa de oro en la mano de Yahvé, que emborrachó a toda la tierra. Las naciones han bebido de su vino; por eso las naciones se han vuelto locas.
8 Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
¡Babilonia ha caído repentinamente y ha sido destruida! ¡Llora por ella! Toma un bálsamo para su dolor. Tal vez pueda curarse.
9 Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
“Habríamos curado a Babilonia, pero no está curada. Abandónala, y que cada uno se vaya a su país; pues su juicio llega hasta el cielo, y se eleva hasta los cielos.
10 Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
‘Yahvé ha producido nuestra justicia. Venid y anunciemos en Sión la obra de Yahvé, nuestro Dios’.
11 Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
“¡Que las flechas estén afiladas! ¡Sujeta los escudos con firmeza! Yahvé ha agitado el espíritu de los reyes de los medos, porque su propósito es contra Babilonia, para destruirla; porque es la venganza de Yahvé, la venganza de su templo.
12 Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
¡Levanten un estandarte contra los muros de Babilonia! ¡Haz que el reloj sea fuerte! Poner a los vigilantes, y preparar las emboscadas; porque Yahvé se ha propuesto y ha hecho lo que dijo sobre los habitantes de Babilonia.
13 Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
Tú que habitas sobre muchas aguas, abundante en tesoros, ha llegado tu fin, la medida de tu codicia.
14 Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
Yahvé de los Ejércitos ha jurado por sí mismo, diciendo, ‘Seguramente te llenaré de hombres, como con las langostas, y levantarán un grito contra ti’.
15 Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
“Él ha hecho la tierra con su poder. Él ha establecido el mundo por su sabiduría. Con su entendimiento ha extendido los cielos.
16 Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
Cuando él emite su voz, hay un rugido de aguas en los cielos, y hace que los vapores asciendan desde los confines de la tierra. Hace relámpagos para la lluvia, y saca el viento de sus arcas.
17 Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
“Todo hombre se ha vuelto estúpido y sin conocimiento. Todo orfebre se siente decepcionado por su imagen, porque sus imágenes fundidas son falsas, y no hay aliento en ellos.
18 Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
Son vanidad, una obra de ilusión. En el tiempo de su visita, perecerán.
19 Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
La porción de Jacob no es como éstas, porque él formó todas las cosas, incluyendo la tribu de su herencia. Yahvé de los Ejércitos es su nombre.
20 Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
“Vosotros sois mi hacha de combate y mis armas de guerra. Contigo romperé las naciones en pedazos. Con ustedes destruiré reinos.
21 Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
Contigo romperé en pedazos el caballo y su jinete.
22 Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
Contigo romperé en pedazos el carro y el que va en él. Contigo me romperé en pedazos hombre y mujer. Contigo me romperé en pedazos el viejo y el joven. Contigo me romperé en pedazos el joven y la virgen.
23 Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
Contigo romperé en pedazos el pastor y su rebaño. Contigo me romperé en pedazos el agricultor y su yugo. Contigo me romperé en pedazos gobernadores y diputados.
24 Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
“Le devolveré a Babilonia y a todos los habitantes de Caldea todo el mal que han hecho en Sión a tus ojos”, dice el Señor.
25 Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
“He aquí que estoy contra ti, montaña destructora”, dice Yahvé, “que destruye toda la tierra. Extiendo mi mano sobre ti, te bajan de las rocas, y te convertirá en una montaña quemada.
26 Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
No te quitarán una piedra angular, ni una piedra para los cimientos; pero tú estarás desolado para siempre”, dice Yahvé.
27 Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
“¡Poned un estandarte en la tierra! ¡Toca la trompeta entre las naciones! ¡Preparen a las naciones contra ella! ¡Convoca contra ella a los reinos de Ararat, Minni y Ashkenaz! ¡Nombrar a un mariscal contra ella! ¡Haz que los caballos suban como las langostas enjambre!
28 Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
Prepara contra ella a las naciones, ¡los reyes de los medos, sus gobernadores, y todos sus diputados, y toda la tierra de su dominio!
29 Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
La tierra tiembla y sufre; para los propósitos de Yahvé contra Babilonia se mantienen, para convertir la tierra de Babilonia en una desolación, sin habitantes.
30 Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
Los poderosos de Babilonia han dejado de luchar, permanecen en sus fortalezas. Su poderío ha fracasado. Se han convertido en mujeres. Sus moradas son incendiadas. Sus barras están rotas.
31 Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
Un corredor correrá al encuentro de otro, y un mensajero para encontrarse con otro, para mostrar al rey de Babilonia que su ciudad está tomada por todos los lados.
32 Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
Así que los pasajes se apoderan. Han quemado las cañas con fuego. Los hombres de guerra están asustados”.
33 Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
Porque Yahvé de los Ejércitos, el Dios de Israel dice: “La hija de Babilonia es como una era en el momento en que se pisa. Todavía un poco, y el tiempo de la cosecha viene para ella”.
34 Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
“Nabucodonosor, rey de Babilonia, me ha devorado. Me ha aplastado. Me ha convertido en un recipiente vacío. Él, como un monstruo, me ha tragado. Se ha llenado la boca con mis delicias. Me ha expulsado.
35 Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
¡Que la violencia hecha a mí y a mi carne sea sobre Babilonia!” el habitante de Sion dirá; y, “¡Que mi sangre sea sobre los habitantes de Caldea!” dirá Jerusalén.
36 Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
Por eso dice Yahvé: “He aquí que yo defenderé tu causa, y me vengaré por ti. Secaré su mar, y hacer que su fuente se seque.
37 Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
Babilonia se convertirá en un montón, una morada para los chacales, un asombro, y un silbido, sin habitante.
38 Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
Rugirán juntos como leones jóvenes. Gruñirán como cachorros de león.
39 wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
Cuando se inflamen, haré su fiesta, y los emborracharé, para que se alegren, y dormir un sueño perpetuo, y no despertar”, dice Yahvé.
40 nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
“Los haré caer como corderos al matadero, como los carneros con los machos cabríos.
41 Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
“¡Cómo se lleva a Sheshach! ¡Cómo se apodera la alabanza de toda la tierra! ¡Cómo se ha convertido Babilonia en una desolación entre las naciones!
42 Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
El mar ha subido sobre Babilonia. Está cubierta por la multitud de sus olas.
43 Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
Sus ciudades se han convertido en una desolación, una tierra seca, y un desierto, una tierra en la que no habita ningún hombre. Ningún hijo de hombre pasa por ella.
44 Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
Ejecutaré el juicio sobre Bel en Babilonia, y sacaré de su boca lo que se ha tragado. Las naciones no fluirán más hacia él. Sí, el muro de Babilonia caerá.
45 Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
“Pueblo mío, aléjate de en medio de ella, y cada uno de ustedes se salve de la feroz ira de Yahvé.
46 Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
No dejes que tu corazón desfallezca. No temas por las noticias que se escucharán en la tierra. Para las noticias vendrá un año, y después de eso en otro año vendrán las noticias, y la violencia en la tierra, gobernante contra gobernante.
47 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
Por tanto, he aquí que vienen días en que ejecutaré el juicio sobre las imágenes grabadas de Babilonia; y toda su tierra será confundida. Todos sus muertos caerán en medio de ella.
48 Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
Entonces los cielos y la tierra, y todo lo que hay en ella, cantará de alegría sobre Babilonia; porque los destructores vendrán a ella desde el norte”, dice Yahvé.
49 “Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
“Como Babilonia ha hecho caer a los muertos de Israel, así que los muertos de toda la tierra caerán en Babilonia.
50 Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
Tú que has escapado de la espada, ¡ve! ¡No te quedes quieto! Recuerda a Yahvé desde lejos, y deja que Jerusalén entre en tu mente”.
51 Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
“Estamos confundidos porque hemos escuchado reproches. La confusión ha cubierto nuestros rostros, porque han entrado extraños en los santuarios de la casa de Yahvé”.
52 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
“Por lo tanto, he aquí que vienen los días”, dice Yahvé, “que ejecutaré el juicio sobre sus imágenes grabadas; y por toda su tierra gemirán los heridos.
53 Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
Aunque Babilonia se eleve hasta el cielo, y aunque deba fortificar la altura de su fuerza, pero vendrán a ella destructores de mi parte”, dice Yahvé.
54 Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
“El sonido de un grito viene de Babilonia, ¡y de gran destrucción de la tierra de los caldeos!
55 Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
Porque Yahvé arrasa con Babilonia, ¡y destruye de ella la gran voz! Sus olas rugen como muchas aguas. El ruido de su voz es pronunciado.
56 Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
Porque el destructor ha venido sobre ella, incluso en Babilonia. Sus poderosos hombres han sido tomados. Sus arcos están rotos en pedazos, porque Yahvé es un Dios de retribución. Seguramente lo pagará.
57 Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
Haré de ella príncipes y sabios, sus gobernantes, sus diputados y sus poderosos hombres borrachos. Dormirán un sueño perpetuo, y no despertar,” dice el Rey, cuyo nombre es Yahvé de los Ejércitos.
58 Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
El Señor de los Ejércitos dice: “Los anchos muros de Babilonia serán completamente derribados. Sus altas puertas serán quemadas con fuego. Los pueblos trabajarán por la vanidad, y las naciones para el fuego; y se cansarán”.
59 Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
Palabra que el profeta Jeremías ordenó a Seraías, hijo de Nerías, hijo de Maseías, cuando fue con Sedequías, rey de Judá, a Babilonia, en el cuarto año de su reinado. Seraías era jefe de intendencia.
60 Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
Jeremías escribió en un libro todos los males que vendrían sobre Babilonia, y todas estas palabras que están escritas sobre Babilonia.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
Jeremías dijo a Seraías: “Cuando llegues a Babilonia, procura leer todas estas palabras,
62 Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
y di: ‘Señor, tú has hablado sobre este lugar, para cortarlo, para que nadie habite en él, ni hombre ni animal, sino que sea desolado para siempre’.
63 Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
Cuando termines de leer este libro, atarás una piedra y la arrojarás en medio del Éufrates.
64 Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Entonces dirás: ‘Así se hundirá Babilonia y no volverá a levantarse a causa del mal que le haré pasar; y se cansarán’.” Hasta aquí las palabras de Jeremías.