< Yeremia 51 >

1 Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
Ainsi parle l’Eternel: "Voici, je vais susciter contre Babel et contre les habitants de la Chaldée un vent destructeur.
2 Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
Je lancerai sur Babel des barbares pour la secouer comme dans un van et faire le vide dans son territoire. Oui, au jour du malheur, ils la cerneront de toutes parts.
3 Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
Que l’archer ne bande pas son arc, qu’il ne revête pas sa cuirasse! Quant-à vous, n’épargnez pas ses jeunes gens, exterminez toute son armée.
4 Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
Qu’ils tombent sur la terre des Chaldéens, frappés à mort, et dans ses rues, transpercés par l’épée!
5 Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
Certes, Israël non plus que Juda n’est veuf de son Dieu, l’Eternel-Cebaot, tandis que le pays des Chaldéens déborde de crimes à l’égard du Saint d’Israël.
6 Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
Fuyez, sortez de Babel, sauvez-vous tous, afin de ne pas périr pour son crime, car c’est un temps de représailles pour l’Eternel, qui lui paie le prix de ses actes.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
Babel était entre les mains du Seigneur une coupe d’or, destinée à donner l’ivresse à toute la terre; les nations buvaient de son vin et pour cela entraient en délire.
8 Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
Soudain Babel est tombée, et elle s’est brisée. Pleurez sur elle, cherchez du baume pour ses maux, peut-être guérira-t-elle.
9 Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
Nous avons voulu guérir Babel, mais elle est inguérissable. Abandonnez-la! Que chacun de nous retourne en son pays, puisque son châtiment atteint jusqu’au ciel et s’élève jusqu’à la voûte du firmament!
10 Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
Le Seigneur a fait éclater notre droit: Allons raconter dans Sion l’oeuvre de l’Eternel, notre Dieu.
11 Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
Fourbissez les flèches, emplissez les carquois! Le Seigneur a stimulé le courage des rois de Médie, car sa pensée est dirigée contre Babel, dont il veut la destruction: ce sont les représailles de l’Eternel, la revanche de son sanctuaire.
12 Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
Arborez une bannière près des remparts de Babel, renforcez le poste d’observation, placez des sentinelles, disposez des embuscades, car l’Eternel, il a conçu un dessein et il va exécuter ce qu’il a annoncé contre les habitants de Babel.
13 Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
O toi, qui es assise le long des eaux abondantes, si riche en trésors, ta fin est venue, la mesure de tes rapines est comble.
14 Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
L’Eternel-Cebaot l’a juré par lui-même: Certes, je t’inonderai d’hommes nombreux comme les sauterelles, et ils pousseront contre toi le cri de victoire."
15 Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
Il a créé la terre par sa puissance, affermi le monde par sa sagesse, déployé les cieux par son intelligence.
16 Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
Lorsqu’il fait entendre le bruit du tonnerre, des torrents d’eau s’amassent au ciel; il élève les nuées du bout de la terre, il accompagne d’éclairs la pluie et fait s’échapper le vent de ses réservoirs.
17 Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
Tout être humain est éperdu, incapable de comprendre; tout orfèvre a honte de son idole, car sa statue de fonte est un mensonge, nul souffle de vie en tous ces dieux.
18 Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
Ce sont des néants, des oeuvres d’aberration; au jour du règlement des comptes, ils périront.
19 Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
Tel n’est point Celui qui est le lot de Jacob; c’est le créateur de l’univers, et Israël est la tribu qui lui appartient en propre: Eternel-Cebaot est son nom.
20 Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
Tu étais pour moi une massue, une arme de guerre; avec toi je broyais les nations, avec toi je détruisais les royaumes.
21 Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
Avec toi j’écrasais le cheval et son cavalier; avec toi j’écrasais le char et celui qui le montait.
22 Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
Avec toi j’écrasais hommes et femmes, avec toi j’écrasais vieillards et enfants, avec toi j’écrasais jeune homme et vierge.
23 Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
Avec toi j’écrasais le berger et son troupeau, avec toi j’écrasais le laboureur et son attelage, avec toi j’écrasais satrapes et gouverneurs.
24 Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
Mais je rendrai à Babel et à tous les habitants de la Chaldée tout le mal qu’ils ont fait à Sion, je le leur rendrai sous vos yeux, dit le Seigneur.
25 Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
Voici, c’est à toi que j’en ai, ô montagne de destruction, dit le Seigneur, toi qui as causé la ruine de toute la terre. J’Étendrai ma main contre toi, je te ferai rouler du haut des rochers et te changerai en un mont calciné.
26 Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
On ne tirera de toi ni pierre d’angle ni pierre de fondation; mais tu seras réduite à l’état de ruine éternelle, dit le Seigneur.
27 Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
Dressez un signal dans le pays, faites résonner le clairon parmi les nations; contre elle, convoquez des peuples, rassemblez les royaumes d’Ararat, de Minni et d’Achkenaz, recrutez des officiers, amenez des chevaux comme une volée de sauterelles aux ailes hérissées.
28 Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
Convoquez contre elle des peuples, les rois de Médie, Ses gouverneurs et tous ses chefs, et tout le territoire de sa suzeraineté.
29 Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
La terre a frémi et tremblé, car ils s’accomplissent sur Babel, les desseins de l’Eternel, qui veut faire de Babel une solitude inhabitée.
30 Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
Les guerriers de Babel renoncent à combattre, se tiennent cois dans les forts; leur courage s’est évanoui, ils ressemblent à des femmes. On a mis le feu à ses demeures, ses verrous sont brisés.
31 Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
Courrier sur courrier, messager sur messager se précipitent pour annoncer au roi de Babel que sa ville est envahie de toutes parts,
32 Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
que les passages sont occupés, que les fascines sont consumées par le feu, et que les gens de guerre sont dans l’épouvante.
33 Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
Oui, ainsi parle l’Eternel-Cebaot, Dieu d’Israël: "Babel ressemble à une aire, au temps où elle est piétinée; encore un peu et l’heure de la moisson arrivera pour elle.
34 Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
"II m’avait dépouillée dit Sion, il m’avait affolée, Nabuchodonosor, roi de Babel; il m’avait laissée là comme un vase vidé, après m’avoir avalée comme un dragon et s’être bourré le ventre de mes délices; il m’avait pourchassée.
35 Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
Que les violences que j’ai subies dans ma chair soient imputées à Babel! s’écrie l’habitante de Sion; que mon sang retombe sur les gens de Chaldée! s’écrie Jérusalem.
36 Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
C’Est pourquoi, ainsi parle le Seigneur, je vais épouser ta querelle et assouvir ta vengeance; je vais dessécher ses eaux et tarir sa source.
37 Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
Et Babel deviendra un monceau de ruines, un repaire de chacals, un objet de stupeur et de raillerie, un lieu inhabité.
38 Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
Ensemble, ils hurleront comme des léopards, ils grinceront comme de jeunes lionceaux.
39 wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
Au plus fort de leur ardeur, je leur présenterai un festin et leur donnerai l’ivresse, pour qu’ils entrent en délire et s’endorment d’un sommeil éternel, pour ne plus se réveiller, dit le Seigneur.
40 nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
Je les traînerai à la boucherie comme des brebis, comme des béliers et des boucs.
41 Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
Ah! comme Sésac est emportée de force! Comme elle est prise, elle, l’ornement de toute la terre! Comme Babel est devenue une solitude parmi les nations!
42 Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
La mer s’est élancée sur Babel, de la masse de ses flots elle est recouverte.
43 Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
Ses villes se sont changées en solitude, en une région aride et déserte, où nul homme ne s’établira, que ne traversera nul mortel.
44 Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
Je sévirai sur Bel à Babel, je lui arracherai de la bouche le morceau déjà avalé. Les nations n’y afflueront plus et les murs même. de Babel vont s’écrouler.
45 Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
Partez de là, mon peuple; que chacun sauve sa vie devant l’ardente colère de l’Eternel!
46 Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
Que votre coeur ne défaille pas! Ne vous effrayez pas des bruits qui se répandent sur la terre cette année, c’est un bruit, l’année prochaine, ce sera un autre bruit. La violence règne sur la terre, potentats contre potentats.
47 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
Oui, des jours vont venir, où je sévirai contre les idoles de Babel, et tout ce pays sera dans la confusion, et tous ses morts seront couchés sur son sol.
48 Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
Ciel et terre, et tout ce qu’ils renferment, célèbreront la chute de Babel, car c’est du Nord que l’assailleront les dévastateurs, dit l’Eternel.
49 “Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
II faut que Babel tombe à son tour, ô victimes d’Israël! puisqu’aussi bien à cause de. Babel sont tombées les victimes de toute la terre.
50 Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
Vous qui avez échappé au glaive, partez, ne vous arrêtez point! Songez de loin à l’Eternel; que Jérusalem soit présente à votre pensée!
51 Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
"Nous rougissions des outrages que nous étions obligés d’entendre, la honte couvrait notre visage, puisque des étrangers ont envahi les sanctuaires de la maison du Seigneur."
52 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
Aussi des jours viendront, dit l’Eternel, où je sévirai sur ses idoles, et où, sur tout son territoire, geindront des. hommes blessés à mort.
53 Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
Dût Babel monter jusqu’au ciel, ériger dans les hauteurs ses puissantes forteresses, il lui viendrait des dévastateurs suscités par moi, dit l’Eternel.
54 Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
Des cris retentissants montent de Babel, le fracas d’une grande chute du pays des Chaldéens.
55 Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
Car l’Eternel ravage Babel, il y fait taire cette vaste rumeur qui s’élève lorsque mugissent ses vagues comme des eaux profondes, lorsque se répandent les éclats de sa voix.
56 Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
Oui, le dévastateur se jette sur cette ville, sur Babel, ses guerriers sont pris, leurs arcs sont brisés, car l’Eternel est un Dieu de représailles, il paie sans faute.
57 Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
Je verserai l’ivresse à ses princes et à ses sages, à ses gouverneurs, à ses officiers et à ses guerriers: ils s’endormiront d’un sommeil éternel, pour ne plus se réveiller, dit le Roi, dont le nom est Eternel-Cebaot.
58 Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
Ainsi parle l’Eternel-Cebaot: "Les murs de la grande Babel s’écrouleront de fond en comble, ses portes, si hautes, deviendront la proie des flammes. Voilà comme les peuples travaillent pour le néant et les nations s’exténuent au profit du feu!"
59 Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
Recommandation que fit le prophète Jérémie à Seraïa, fils de Nêria, fils de Mahséia, lorsqu’il se rendit à Babylone sur l’ordre de Sédécias, roi de Juda, dans la quatrième année de son règne; Seraïa était commandant des étapes.
60 Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
Jérémie avait consigné dans un livre toutes les calamités qui devaient atteindre Babylone, tous ces discours qui avaient été rédigés au sujet de cette ville.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
Jérémie dit donc à Seraïa: "Quand tu arriveras à Babylone, tu auras soin de donner lecture de tous ces discours.
62 Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
Ensuite tu diras: "Eternel! C’Est toi qui as décrété contre cette ville sa complète destruction, au point que nul n’y habitera plus, ni hommes, ni bêtes, et qu’elle se trouvera réduite à l’état de ruine éternelle!"
63 Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
Et lorsque tu auras fini de donner lecture de ce livre, tu y attacheras une pierre et tu le lanceras en plein Euphrate,
64 Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
tout en disant ces mots: "Ainsi s’effondrera Babel, pour ne plus se relever, par l’effet de la calamité que je fais fondre sur elle: ils périront d’épuisement!" Ici se terminent les discours de Jérémie.

< Yeremia 51 >