< Yeremia 51 >

1 Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
This is what Yahweh says: “I will inspire/motivate [an army] to destroy Babylon [like a powerful] wind [MET], and [also] to destroy the people of Babylonia.
2 Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
I will send a foreign army to come to get rid of Babylonia [like a strong wind] that blows away chaff. They will attack from every direction on that day of disaster.
3 Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
[I will tell them, ] ‘Do not allow the archers [of Babylon] to [have time to] put on their armor or draw their bows. Do not spare the young men of Babylon. Completely destroy their army.’
4 Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
Their soldiers will fall dead in Babylonia; [they will die after being] wounded in the streets.
5 Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
[I, ] the Commander of the armies of angels, the Israelis’ God, have not abandoned Israel and Judah. [Even though] their land was full of people who sinned against [me], the Holy God of Israel, I am still their God.
6 Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
[You people of Israel and Judah, ] flee from Babylon! Run away from there! Do not stay there and be killed when I punish [the people of Babylon]! It will be the time when I will get revenge; I will do to them what they deserve.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
Babylon has been [like] [MET] a gold cup in my hand, [a cup that is full of wine] that caused people all over the earth [who drank some of it to become] drunk. [It is as though] the [rulers of] the nations drank the wine from Babylon, and it caused them to become crazy.
8 Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
But suddenly Babylon will be conquered. [You foreigners who live in Babylon, ] weep for its people. Give them medicine for their wounds; perhaps they can be healed.”
9 Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
We [foreigners] would have [tried to] heal them, but [now] they cannot be healed. [So we will not try to help them; ] we will abandon them, and return to our own lands, because [it is as though] the punishment they are receiving is so great that it reaches up to the clouds in sky, [so great that no one can measure it].
10 Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
Yahweh has (vindicated us/shown that we were right); [so] let’s proclaim in Jerusalem everything that Yahweh our God has done [for us].
11 Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
[You enemy soldiers, ] sharpen your arrows! Lift up your shields, [because] Yahweh has incited your kings of Media [and Persia to march with their armies] to Babylon and to destroy it. That is how Yahweh will get revenge on [those foreigners who entered] his temple [in Jerusalem] and defiled it.
12 Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
Lift up a battle flag close to the walls of Babylon! (Reinforce the/Appoint more) guards, and tell the watchmen to stand [in their positions]! Prepare an ambush, because Yahweh is about to accomplish all that he has planned to do to the people of Babylon.
13 Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
Babylon is [a city] near the great [Euphrates] River, a city in which there are many rich people, but it is time for Babylon to be finished; the time [for the city] to exist is ended.
14 Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
The Commander of the armies of angels has solemnly promised, using his own name, “Your cities will be filled with your enemies; I will cause them to be like [SIM] a swarm of locusts; and they will shout triumphantly [when they conquer your city].”
15 Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
Yahweh created the earth by his power; he established it by his wisdom, and he stretched out the sky by his understanding.
16 Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
When he speaks loudly, there is thunder in the sky; he causes clouds to form in every part of the earth. He sends lightning with the rain and releases the winds from his storehouses.
17 Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
People are senseless, and they know very little [HYP]; those who make idols are [always] disappointed, because their idols [do nothing for them]. The images/statues that they make are not real [gods]; they are lifeless.
18 Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
Idols are worthless; they deserve to be ridiculed; there will be a time when they will [all] be destroyed.
19 Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
But the God whom [we] Israelis [worship] is not like those [idols]; he is the one who created everything [that exists]; [we], the people of Israel, belong to him; his name is ‘the Commander of the armies of angels’.
20 Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
Yahweh says [about the army of Babylonia] (OR, [about a nation that will attack Babylonia)], “You have been [like] [MET] my battle-axe and war-club; with your [power] I have shattered nations and destroyed [many] kingdoms.
21 Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
With your [power] I have shattered armies [of other nations]: I destroyed [their] horses and their riders, [their] chariots and [their] chariot-drivers.
22 Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
With your [power] I shattered men and women, old people and children, young men and young women.
23 Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
With your [power] I shattered shepherds and their flocks [of sheep], farmers and their oxen, governors and [their] officials.”
24 Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
But, Yahweh [also] says, “[Soon] I will repay/punish [you] people in Babylon and in the rest of Babylonia for all the evil things that you have done in Jerusalem.
25 Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
[Babylonia is] [APO] like [MET] a great mountain [from which bandits descend] to (plunder/steal things from) people all over the earth. But I, Yahweh, am the enemy of you [people of Babylonia]. I will raise my fist to strike you. I will knock you down from the cliffs and cause you to be [only] a huge pile of burned rubble.
26 Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
Your [city] will be abandoned forever; [even] the stones in your [city] will never [again] be used for buildings. [Your city will be completely destroyed].”
27 Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
[Tell] the nations to lift up a battle flag! [Tell them to] shout the battle-cry! Gather all their armies to fight against Babylon! Prepare the nations to attack Babylon. Summon [the armies of] the kingdoms [north of Babylonia]—from Ararat, Minni, and Ashkenaz. Appoint a commander for them, and bring [a great number of] horses; [there must be a huge number of horses]; that [huge number] will resemble [SIM] a swarm of locusts.
28 Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
Prepare the [armies of other nations], armies that will be led by the kings of Media [and Persia], their governors and [their] officials.
29 Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
[When they attack Babylon, it will be as though] the earth will shake and writhe [in pain], because [those armies] will accomplish everything that Yahweh has planned to do to Babylon; they will destroy it completely, [with the result that] no one will live there [again].
30 Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
[When their enemies attack], the strongest warriors in Babylon will not fight. They will remain in their barracks, without any strength. They will be as timid/weak as [SIM] women. [The enemy soldiers] will burn the buildings in the city and pull down the bars [of the city gates].
31 Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
Messengers will go quickly, one after another, to tell the king that his city has been captured.
32 Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
The places at which people can cross the river [to escape from the city] will be blocked. The dry reeds in the marshes/swamps will be set on fire, and the soldiers of Babylon will be terrified.
33 Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
This is what the Commander of the armies of angels, the God whom [we] Israelis [worship], says; “Babylon is like [SIM] wheat on the ground where it is about to be threshed by [animals] tramping on it. Very soon [their enemies] will trample on [the city of] Babylon [MET].”
34 Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
[The army of] Nebuchadnezzar, the King of Babylon, has attacked and crushed us [Israeli people], and we have no strength [left]. [It is as though] they have swallowed us like a [great] monster that filled its belly with all our tasty parts, and then has spit out [what it did not like].
35 Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
[So] the people of [PRS] Jerusalem say [to Yahweh], “Cause the people of Babylon to suffer like they caused us to suffer! Cause the people of Babylonia to be punished for killing [MTY] our people!”
36 Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
And this is what Yahweh replies to the people of Jerusalem: “I will [be like your lawyer to] defend you, and I will avenge you. I will dry up the river in Babylon and [all] the springs of water.
37 Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
Babylon will become a heap of ruins, a place where jackals/wolves live. It will become a place that people are horrified about and will ridicule; it will be a place where no one lives.
38 Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
The people of Babylon will [all] roar like young lions; they will growl like baby lions.
39 wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
But while they are extremely hungry, I will prepare a [different kind of] feast for them. [It is as though] I will cause them to drink wine until they are very drunk, [with the result that] they will fall asleep. But they will never wake up from that sleep!
40 nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
I will bring them down to a place where they will be slaughtered, like [SIM] [someone who takes] lambs or rams or goats [to where they will be slaughtered for sacrifices].
41 Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
People all over the earth [now] (honor/praise) Babylon; they say that it is a great city. But I will cause it to become a [place about which people of all] nations are horrified.
42 Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
The [enemies of Babylon] will cover the city [like] huge waves of the sea [DOU].
43 Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
The towns in Babylonia will become ruins, Babylonia will become a dry desert area. It will be a land in which no one lives and which no one walks through.
44 Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
And I will punish Bel, [the god that the people] of Babylon [worship], and I will cause the people to give back what they have stolen [MET]. [People of other] nations will no longer come to [worship] Bel. And the walls of Babylon will collapse.”
45 Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
[Yahweh also says, ] “My people, come out of Babylon! Run away from there! Run, because [I], Yahweh, am extremely angry [MTY] [with the people of Babylon, and I will get rid of them]!
46 Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
Do not be discouraged/worried [IDM] or afraid when you hear reports [about what is happening in Babylon]. People will report rumors like that every year, rumors about violent things being done in the land, and rumors about leaders fighting against each other.
47 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
But it will soon be the time for me to get rid of the idols in Babylon. [People all over] the land will be ashamed [because of being defeated]; and the corpses of their [soldiers] will lie in the streets.
48 Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
Then all [the angels in] heaven and all the [people on] [PRS] the earth will rejoice, because from the north will come [armies] that will destroy Babylon.
49 “Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
Like [the soldiers of Babylon] killed the people of Israel and [also] killed others all over the world [HYP], [the people of] Babylon must also be killed.
50 Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
You [Israeli people] who have not been killed [MTY], get out of Babylon! Do not wait! [Even though you are in a land] far away [from Israel], think about Yahweh, and think about Jerusalem!”
51 Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
[The Israeli people say], “We are ashamed. We are completely disgraced [DOU], because foreigners have entered Yahweh’s temple [and (defiled it/caused it to become unfit for worship)].”
52 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
Yahweh replies, “[That is true], but there will soon be a time when I will destroy the idols in Babylon, and throughout Babylonia there will be wounded people who will groan.
53 Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
Even if [the walls around] Babylon could extend up to the sky, and if its walls/fortifications were extremely strong, I will send [armies] that will destroy the city. [That will surely happen because I, ] Yahweh, have said it.”
54 Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
Listen to [the people of] Babylon crying [for help]! And listen to the sounds of things being destroyed all over Babylonia!
55 Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
Yahweh will be destroying Babylon. He will cause the loud noises in the city to cease.
56 Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
Enemy troops will surge against the city like [SIM] a great wave. They will capture the city’s mighty soldiers and break their weapons. [That will happen] because Yahweh is a God who punishes [his enemies] justly; he will punish them as they deserve.
57 Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
The king, the Commander of the armies of angels says, “I will cause the city officials and wise men, the army captains and soldiers [in Babylon] to become drunk. They will fall asleep, but they will never wake up [again]!”
58 Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
Yahweh also says, “The thick walls around Babylon will be flattened to the ground. The city gates will be burned. People [from other countries] will work hard [to save the city], but it will be (in vain/useless), because everything [that they have built] will be destroyed by fire.”
59 Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
Seraiah was the man who made arrangements for the King of Babylon [whenever he traveled]. He was the son of Neraiah and grandson of Mahseiah. When he was about to go to Babylon with King Zedekiah, after Zedekiah had been ruling Judah for almost four years, the prophet Jeremiah gave him a message.
60 Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
Jeremiah had written on a scroll a list of all the disasters that he had written about, disasters that would soon occur in Babylon.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
He said to Seraiah, “When you arrive in Babylon, read [aloud] everything that I have written [on this scroll].
62 Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
Then pray, ‘Yahweh, you said that you will thoroughly destroy Babylon, with the result that people and animals will no [longer] live there. You said that it will be desolate forever.’
63 Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
[Then], when you have finished reading [what I have written on] the scroll, tie it to a [heavy] stone and throw it into the Euphrates [River].
64 Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Then say, ‘In the same way, Babylon [and its people] will disappear and never exist again, because of the disasters that Yahweh will cause to occur there’” That is the end of Jeremiah’s messages.

< Yeremia 51 >