< Yeremia 51 >
1 Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
This is what the Lord says: Look! I'm going to stir up a destructive wind against Babylon and against the people of Babylonia.
2 Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
I will send foreign soldiers to attack Babylon to winnow her and turn her country into a wasteland—they will attack her from all directions when her time of trouble comes.
3 Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
The archer doesn't need to use his bow; the infantryman doesn't need to put on his armor. Don't spare her young soldiers; set apart her whole army for destruction!
4 Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
They will fall down wounded in her streets, killed in the country of Babylonia.
5 Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
Israel and Judah have not been deserted by their God, the Lord Almighty, even though they sinned against the Holy One of Israel everywhere in their country.
6 Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
Escape from Babylon! Run for your lives! Don't get caught up in her punishment and die, for this is the time when the Lord pays her back for her sins.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
Once Babylon was a golden cup the Lord held in his hand. She made the whole earth drunk. The nations drank her wine which is why they went mad.
8 Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
Now, all of a sudden, Babylon has fallen. She has been smashed to pieces. Weep for her; get her some treatment for her pain. Maybe she can be healed.
9 Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
“We tried to heal her, but she couldn't be helped. So give up on her! All of us should go home to where we came from. The news of her punishment has reached everywhere, all the way to heaven.
10 Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
The Lord has encouraged and supported us. Come on, let's tell people here in Jerusalem what the Lord has done for us!”
11 Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
Sharpen the arrows! Pick up the shields! The Lord has encouraged the kings of the Medes, because his plan is directed at the destruction of Babylon. The Lord is paying them back for what happened to his Temple.
12 Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
Raise the signal flag to attack the walls of Babylon; strengthen the guard; have the watchmen take their places; get the ambush ready. The Lord planned and carried out his threats against the people of Babylon.
13 Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
You people who live beside by many waters, and have so much wealth, this is the time of your end—your life will be cut short.
14 Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
The Lord Almighty vowed by his own life, saying, I'm going to make sure to fill you with so many enemy soldiers they'll be like locusts. They will shout as they celebrate their victory over you.
15 Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
It was God who made the earth by his power. He created the world by his wisdom and by his understanding he put the heavens in place.
16 Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
The waters of the heavens rain down with a roar at his command. He makes the clouds to rise all over the earth. He makes lightning to accompany rain, and sends the wind from his storehouses.
17 Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
Everyone is stupid; they don't know anything. Every metalworker is embarrassed by the idols they make. For their images made of molten metal are fraudulent—they're not alive!
18 Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
They are useless, an object to be laughed at. They will be destroyed at the time of their punishment.
19 Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
The God of Jacob is not like these idols, for he is the creator of everything, including his own people that are special to him. The Lord Almighty is his name.
20 Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
You are my war club, the weapon I use in battle. I use you to destroy nations; I use you to destroy kingdoms.
21 Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
I use you to destroy horses and their riders; I use you to destroy chariots and their drivers.
22 Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
I use you to destroy men and women; I use you to destroy old men and youths; I use you to destroy young men and girls.
23 Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
I use you to destroy shepherds and their flocks; I use you to destroy farmers and their cattle; I use you to destroy rulers and state officials.
24 Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
Right in front of you I'm going to pay back Babylon and everyone who live in Babylonia for all the evil they did to Jerusalem, declares the Lord.
25 Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
Watch out, because I am against you, you destructive monster who devastates the whole world, declares the Lord. I will reach out to attack you; I will roll you down the cliffs; I will turn you into a mountain of ash.
26 Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
Nobody will be even able to find themselves a cornerstone or a foundation stone among your ruins, because you will be so utterly destroyed, declares the Lord.
27 Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
Raise a signal flag in the country! Blow the trumpet call to war among the nations! Get the nations ready to attack her; Summon the kingdoms to march against her: Ararat, Minni, and Ashkenaz. Choose a commander to lead the armies to attack her; send into battle cavalry like a swarm of locusts.
28 Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
Have the armies of the nations prepare for battle against her. This applies to the kings of the Medes, their leaders and all their officers, and every country they rule.
29 Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
The earth quakes and trembles because the Lord is determined to carry out what he threatened against Babylon—to turn Babylonia into a wasteland where no one lives.
30 Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
Babylon's defenders have given up fighting—they're just sitting in their fortresses. They're worn out; they've become like frightened women. Babylon's houses are burning; the bars securing her gates have been smashed.
31 Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
A runner hands his message over to another to carry; one messenger follows another messenger, all of them alerting the king of Babylon to the news that his city has been completely conquered,
32 Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
the river crossings have been captured, the marshlands set on fire and his soldiers are panicking.
33 Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: The people of Babylon are like a threshing floor when the grain is trampled out. Her time of harvest will come very soon.
34 Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
Nebuchadnezzar king of Babylon chewed me up and sucked me dry, making me as empty as a jar with nothing in it. He swallowed me down as if he were some monster, filling himself with the tastiest parts of me and throwing the rest away.
35 Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
“Babylon must bear the responsibility for the violent attacks on us,” say the inhabitants of Zion. “The people of Babylonia must bear the responsibility for the blood shed in my city,” says Jerusalem.
36 Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
This is what the Lord says: Watch as I present your case for you and make your enemies pay for what they did to you. I'm going to dry up her river and her springs.
37 Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
Babylon will be turned into a pile of rubble, a home for jackals, a place that horrifies people, a place they jeer at, a place where no one lives.
38 Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
The Babylonians will roar together like powerful lions and growl like lion cubs.
39 wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
But while their passions are aroused, I will serve them a banquet and get them drunk. They'll celebrate so much that they'll pass out and won't ever wake up, declares the Lord.
40 nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
I will take them down like lambs to be slaughtered, like rams and goats.
41 Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
How could it be? Babylon has fallen! The most famous city in the world has been conquered! What a horrible sight Babylon has become to everyone watching!
42 Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
It's as if the sea has flooded over Babylon, covering her in crashing waves.
43 Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
The towns of Babylonia are in ruins, turned into a dry desert wasteland where no one lives—no one even passes by.
44 Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
I will punish Bel in Babylon. I will force him to spit out what he swallowed. People of other nations won't run to worship him anymore. Even Babylon's wall has fallen.
45 Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
My people, come out of her! Each one of you, save yourselves from the Lord's furious anger.
46 Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
Don't lose courage, and don't be afraid when you hear different rumors going around the country. There'll be one rumor one year, and another one the next, talking about violent revolution, of one ruler fighting against another.
47 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
Look, the time is coming when I will punish Babylon's idols. The whole country will be humiliated; it will be full of the dead bodies of those who have been killed.
48 Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
Then everyone in heaven and on earth will celebrate with shouts of joy at what's happened to Babylon, because the destroyers from the north will come and attack her, declares the Lord.
49 “Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
Babylon has to fall because of the Israelites and people of other nations she killed.
50 Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
Those of you who have managed to escape being killed, leave now! Don't delay! Remember the Lord in this far away place; think about Jerusalem.
51 Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
“We are embarrassed because we've been mocked, and we held our heads in shame because foreigners went into the holy places of the Lord's Temple,”
52 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
So keep watching, declares the Lord, because the time is coming when I will punish her for worshiping idols, and the sound of wounded people moaning will be heard throughout the country.
53 Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
Even if Babylon could climb up into the sky to strengthen her high fortresses, those I send to attack her will destroy her, declares the Lord.
54 Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
A cry comes from Babylon; the noise of terrible destruction comes from the country of Babylonia.
55 Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
For the Lord is going to destroy Babylon; he will put an end to her boastful talk. The waves of attacking army will roar like the crashing sea; the noise of their shouts will echo all around.
56 Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
A destroyer is coming to attack Babylon. Her soldiers will be taken prisoner, and their bows will be smashed, for the Lord is a God who punishes fairly; he will definitely pay them back.
57 Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
I will make her leaders and wise men drunk, along with her commanders, officers, and soldiers. Then they will pass out, and won't ever wake up, declares the King, whose name is the Lord Almighty.
58 Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
This is what the Lord Almighty says: Babylon's massive walls will be knocked down to the ground and her high gates burned. All that the people worked for will be for nothing; other nations who came to help will wear themselves out, only to see what they've done go up in flames.
59 Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
This is the message that Jeremiah the prophet gave to Seraiah son of Neriah, son of Mahseiah, when he accompanied King Zedekiah of Judah to Babylon in the fourth year of Zedekiah's reign. Seraiah was the king's personal assistant.
60 Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
Jeremiah had written on a scroll a description of all the disasters that would come to Babylon—all these words written here about Babylon.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
Jeremiah told Seraiah, “When you arrive in Babylon, make sure you read out loud everything written here,
62 Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
and announce, ‘Lord, you have promised to destroy this place so that none will be left—no people or animals. In fact it will be deserted forever.’
63 Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
After you finish reading this scroll out loud, tie a stone to it and throw it into the Euphrates.
64 Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Then say, ‘This is how Babylon will sink and won't ever rise again, because of the disaster I'm bringing down on her. Her people will grow tired.’” This is the end of Jeremiah's messages.