< Yeremia 50 >

1 Hili ni neno alilolisema Yahwe juu ya Babeli, nchi ya Wakalidayo, kwa mkono wa Yeremia nabii,
[the] word which to speak: speak LORD to(wards) Babylon to(wards) land: country/planet Chaldea in/on/with hand: by Jeremiah [the] prophet
2 “Wajulishe mataifa ili wasikie. Toa ishara ili wasikie. Usiiache. Sema, 'Babeli imetwaliwa. Beli ameaibika. Merodaki amefadhaika. Sanamu zake zimeaibishwa; vinyago vyake vimefadhaika
to tell in/on/with nation and to hear: proclaim and to lift: raise ensign to hear: proclaim not to hide to say to capture Babylon be ashamed Bel to to be dismayed Merodach be ashamed idol her to to be dismayed idol her
3 Taifa kutoka kaskazini litainuka kinyume chake, ili kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja, awe mtu au mnyama, atakayeishi ndani yake. Wataondoka.
for to ascend: rise upon her nation from north he/she/it to set: make [obj] land: country/planet her to/for horror: destroyed and not to be to dwell in/on/with her from man and till animal to wander to go: went
4 Katika siku hizo na wakati huo - hili ni tamko ya Yahwe - watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika ili kwenda kwa kulia na kumtafuta Yahwe Mungu wao.
in/on/with day [the] they(masc.) and in/on/with time [the] he/she/it utterance LORD to come (in): come son: descendant/people Israel they(masc.) and son: descendant/people Judah together to go: come and to weep to go: come and [obj] LORD God their to seek
5 Watauliza njia ya kwenda Sayuni nao watakwenda huko, wakisema, tutakwenda wenyewe ili kuungana na Yahwe katika agano la milele lisilosahaulikal
Zion to ask way: road here/thus face their to come (in): come and to join to(wards) LORD covenant forever: enduring not to forget
6 Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea. Wachungaji wao wamewapoteza milimani; wamewageuza kutoka mlima hata mlima. Walikwenda, wakasahau mahali walipokuwa wanaishi.
flock to perish (to be *Q(K)*) people my to pasture their to go astray them mountain: mount (turning back them *Q(K)*) from mountain: mount to(wards) hill to go: went to forget rest their
7 Kila awaendeaye anawararua. Washitaki wao walisema, 'Hatuna hatia, kwa sababu walimtenda dhambi Yahwe, nyumbani kwao halisi - Yahwe, tumaini la mababu zao.'
all to find them to eat them and enemy their to say not be guilty underneath: because of which to sin to/for LORD pasture righteousness and hope father their LORD
8 Tokeni kati ya Babeli; tokeni katika nchi ya Wakalidayo; iweni kama wafanyavyo mabeberu mbele ya kundi lote.
to wander from midst Babylon and from land: country/planet Chaldea (to come out: come *Q(K)*) and to be like/as goat to/for face: before flock
9 Maana tazama, ninaelekea kupeleka na kuinua kinyume cha Babeli kundi la mataifa makubwa kutoka kaskazini. Yatajipanga yenyewe kinyume chake. Kutoka hapo Babeli utatekwa. Mishale yao ni kama shujaa mzoefu asiyerudi mikono tupu.
for behold I to rouse and to ascend: establish upon Babylon assembly nation great: large from land: country/planet north and to arrange to/for her from there to capture arrow his like/as mighty man be prudent not to return: return emptily
10 Ukaldayo itakuwa mateka. Wate waitekao wataridhika - asema Yahwe.
and to be Chaldea to/for spoil all to loot her to satisfy utterance LORD
11 Mnafurahi, mnasherehekea kuteka urithi wangu; mnarukaruka kama ndama anayekanyaga katika malisho yake; mnalia kama farasi mwenye nguvu.
for (to rejoice *Q(K)*) for (to exult *Q(K)*) to plunder inheritance my for (to leap *Q(K)*) like/as heifer to tread (and to cry out *Q(K)*) like/as mighty: stallion
12 Hivyo mama yenu ataaibika sana; aliyewazaa atafadhaika. Tazama, atakuwa wa mwisho katika mataifa, nyika, nchi kame, na jangwa.
be ashamed mother your much be ashamed to beget you behold end nation wilderness dryness and plain
13 Kwa sababu ya hasira ya Yahwe, Babeli haitakaliwa, lakini itakuwa ukiwa mtupu. Kila apitaye kando ataogopa kwa sababu ya Babeli na atatoa sauti kwa sababu ya majeraha yake.
from wrath LORD not to dwell and to be devastation all her all to pass upon Babylon be desolate: appalled and to whistle upon all wound her
14 Jipangeni wenyewe kumzunguka Babeli kinyume chake. Kila apindaye upinde na ampige. Msizuie mshale wenu wowote, maana amemtenda dhambi Yahwe.
to arrange upon Babylon around all to tread bow to give thanks to(wards) her not to spare to(wards) arrow for to/for LORD to sin
15 Pigeni kelele za ushindi kinyume chake ninyi nyote mmzungukao. Amesalimu mamlaka yake; minara yake imeanguka. Kuta zake zimebomolewa, maana hiki ni kisasi cha Yahwe. Jilipizeni kisasi juu yake! Mtendeeni kama alivyoyatenda mataifa mengine.
to shout upon her around to give: give hand: power her to fall: fall (foundation her *Q(k)*) to overthrow wall her for vengeance LORD he/she/it to avenge in/on/with her like/as as which to make: do to make: do to/for her
16 Waaribuni wote mkulima apandaye mbegu naye atumiaye mundu wakati wa mavuno katika Babeli. Haya kila mtu na arudi kwa watu wake kutoka upanga wa mtesaji; na wakimbilie katika nchi yao wenyewe.
to cut: eliminate to sow from Babylon and to capture sickle in/on/with time harvest from face: before sword [the] to oppress man: anyone to(wards) people his to turn and man: anyone to/for land: country/planet his to flee
17 Israeli ni kondoo aliyetawanywa na kupelekwa na simba mbali. Kwanza mfalme wa Ashuru alimrarua; kisha baadaye, Nebukadneza mfalme wa Babeli akavunja mifupa yake.
sheep to scatter Israel lion to banish [the] first to eat him king Assyria and this [the] last be vast him Nebuchadnezzar king Babylon
18 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Tazama, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
to/for so thus to say LORD Hosts God Israel look! I to reckon: punish to(wards) king Babylon and to(wards) land: country/planet his like/as as which to reckon: punish to(wards) king Assyria
19 Nitamrudisha Israeli katika nchi yake; atajilisha katika Karmeli na Bashani. Kisha atajishibisha katika nchi ya kilima ya Efraimu na Gileadi.
and to return: rescue [obj] Israel to(wards) pasture his and to pasture [the] Carmel and [the] Bashan and in/on/with mountain: mount Ephraim and [the] Gilead to satisfy soul: appetite his
20 Siku hizo na wakati huo, asema Yahwe, uovu utatafutwa katika Israeli, lakini hautaonekana. Nitauliza kuhusu dhambi za Yuda, lakini hazitaonekana, maana nitawasamehe mabaki niliowaacha.”
in/on/with day [the] they(masc.) and in/on/with time [the] he/she/it utterance LORD to seek [obj] iniquity: crime Israel and nothing he and [obj] sin Judah and not to find for to forgive to/for which to remain
21 Inuka dhidi ya nchi ya Merathaimu, kinyume chake nao waishio Pekodi. Wapigeni kwa makali ya upanga na mwatenge kwa ajili ya maangamizo - asema Yahwe - fanyeni kila ninachowaamru.
upon [the] land: country/planet Merathaim to ascend: rise upon her and to(wards) to dwell Pekod to slay and to devote/destroy after them utterance LORD and to make: do like/as all which to command you
22 Sauti ya vita na maangamizi ya kustaajabisha yamo katika nchi.
voice: sound battle in/on/with land: country/planet and breaking great: large
23 Jinsi gani nyundo ya mataifa yote imekatiliwa mbali na kuharibiwa. Jinsi Babeli amekuwa kitu cha kushangaza kati ya mataifa.
how? to cut down/off and to break hammer all [the] land: country/planet how? to be to/for horror: appalled Babylon in/on/with nation
24 Nimetega mtego dhidi yako. Umenaswa, Babeli, nawe haukutambua! Ulionekana na kukamatwa, tangu uliponidhihaki, Yahwe.
to snare to/for you and also to capture Babylon and you(f. s.) not to know to find and also to capture for in/on/with LORD to stir up
25 Yahwe amefungua ghala lake la silaha na anachukua silaha kwa ajili ya kutekekeleza hasira yake. Kuna kazi kwa ajili ya Yahwe wa majeshi katika nchi ya Wakaldayo.
to open LORD [obj] treasure his and to come out: send [obj] article/utensil indignation his for work he/she/it to/for Lord YHWH/God Hosts in/on/with land: country/planet Chaldea
26 Mshambulie kutokea mbali. Fungua maghala yake ya chakula na kumrundika kama marundo ya nafaka. Mtenge mbali na maangamizi. Usimbakizie masalia.
to come (in): come to/for her from end to open granary her to build her like heap and to devote/destroy her not to be to/for her remnant
27 Ua madume wake wote wa ng'ombe. Washushe sehemu ya machinjio. Ole wao, maana siku yao imefika - wakati wa kuadhibiwa kwao.
to slay all bullock her to go down to/for slaughter woe! upon them for to come (in): come day their time punishment their
28 Kuna sauti ya wale wanaokimbia, walionusurika, katika nchi ya Babeli. Hawa watatoa taarifa ya kisasi cha Yahwe Mungu wetu kwa Sayuni, kisasi kwa hekalu lake.”
voice to flee and survivor from land: country/planet Babylon to/for to tell in/on/with Zion [obj] vengeance LORD God our vengeance temple his
29 Ita wapiga pinde dhidi ya Babeli - wale wote wapindao pinde zao. Piga kambi kinyume chake, na msimwache yeyote kutoroka. Mlipeni kwa kile alichofanya. Mfanyieni kwa kipimo alichotumia. Maana amemdharau Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
to hear: proclaim to(wards) Babylon archer all to tread bow to camp upon her around not (to be to/for her *Q(K)*) survivor to complete to/for her like/as work her like/as all which to make: do to make: do to/for her for to(wards) LORD to boil to(wards) holy Israel
30 Hivyo vijana wake wataanguka katika viwanja vya mji, na wapiganaji wake wote wataangamizwa siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe.”
to/for so to fall: kill youth her in/on/with street/plaza her and all human battle her to silence: silent in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD
31 Tazama, mimi ni kunyume chako, mwenye majivuno - hili ni tamko la Bwana Yahwe wa majeshi - maana siku yako imefika, mwenye kiburi, wakati nitakapokuadhibu.
look! I to(wards) you arrogance utterance Lord YHWH/God Hosts for to come (in): come day your time to reckon: punish you
32 Hivyo wenye kiburi watajikwaa na kuanguka. Hakuna atakaye wainua. Nitawasha moto katika miji yao; utateketeza kila kitu kati yake.
and to stumble arrogance and to fall: fall and nothing to/for him to arise: establish and to kindle fire in/on/with city his and to eat all around him
33 Yahwe wa majeshi asema hivi: watu wa Israeli wamenyanyaswa, pamoja na watu wa Yuda. Wate waliowateka bado wanawashikilia; wanakataa kuwaacha waondoke.
thus to say LORD Hosts to oppress son: descendant/people Israel and son: descendant/people Judah together and all to take captive them to strengthen: hold in/on/with them to refuse to send: let go them
34 Yeye awaokoaye ni mwenye nguvu. Yahwe wa majeshi ni jina lake. Kwa hakika atalitetea shitaka lao, ili kuleta pumziko katika nchi, na kuwapiga wakaao Babeli.
to redeem: redeem their strong LORD Hosts name his to contend to contend [obj] strife their because to rest [obj] [the] land: country/planet and to tremble to/for to dwell Babylon
35 Upanga u juu ya Wakalidayo - asema Yahwe - na juu ya wakaao Babeli, viongozi wake, na wenye hekima wake.
sword upon Chaldea utterance LORD and to(wards) to dwell Babylon and to(wards) ruler her and to(wards) wise her
36 Upanga unakuja juu ya waganga, ili wajione kuwa wajinga. Upanga utakuwa juu ya askari wake, hivyo watajaa hofu.
sword to(wards) [the] bluster and be foolish sword to(wards) mighty man her and to to be dismayed
37 Upanga utakuwa juu ya farasi wake, vibandawazi vyao na na watu wote waliomo Babeli, hivyo watakuwa kama wanawake. Upanga utakuwa juu ya ghala zake, nazo zitatekwa.
sword to(wards) horse his and to(wards) chariot his and to(wards) all [the] racial-mix which in/on/with midst her and to be to/for woman sword to(wards) treasure her and to plunder
38 Ukame unakuja juu ya maji yake, hivyo yatakauka. Maana ni nchi ya miungu wasiofaa, na wanafanya kama watu waliofanywa punguani kwa miungu yao isiyosaidia.
drought to(wards) water her and to wither for land: country/planet idol he/she/it and in/on/with terror to be foolish
39 Hivyo wanyama wa jangwani wakaishi na mbwea wataishi huko, na watoto wa mbuni wataishi ndani yake. Kwa muda wote, hatakaliwa tena. Kutoka kizazi hata kizazi, hatakaliwa tena na watu.
to/for so to dwell wild beast with wild beast and to dwell in/on/with her daughter ostrich and not to dwell still to/for perpetuity and not to dwell till generation and generation
40 Kama vile Mungu alivyoziangamiza Sodoma na Gomora na majirani zake - asema Yahwe - hakuna atakayeishi huko; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
like/as overthrow God [obj] Sodom and [obj] Gomorrah and [obj] neighboring her utterance LORD not to dwell there man: anyone and not to sojourn in/on/with her son: child man
41 “Tazama, watu wanakuja kutoka kaskazini, maana taifa kubwa na wafalme wengi wamemtikisa kutokea mbali.
behold people to come (in): come from north and nation great: large and king many to rouse from flank land: country/planet
42 Watachukua pinde na mishale. Ni wakatili na hawana huruma. Sauti yao ni kama mngurumo wa bahari, na wamepanda farasi katika mpangilio kama watu wapiganao, dhidi yako, bindi Babeli.
bow and javelin to strengthen: hold cruel they(masc.) and not to have compassion voice: sound their like/as sea to roar and upon horse to ride to arrange like/as man to/for battle upon you daughter Babylon
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari yao na mikono yake imelegea kwa huzuni. Mashaka yamemshika kama mwanamke katika utungu.
to hear: hear king Babylon [obj] report their and to slacken hand his distress to strengthen: hold him agony like/as to beget
44 Tazama! Anakwenda juu kama simba atokaye katika miinuko ya Yordani kuelekea katika eneo la malisho ya uvumilivu. Maana kwa haraka nitawafanya wakimbie kutoka humo, nami nitamweka mtu aliyechaguliwa kwa uangalizi wake. Maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayeniagiza? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
behold like/as lion to ascend: rise from pride [the] Jordan to(wards) pasture strong for to disturb (to run: run them *Q(K)*) from upon her and who? to choose to(wards) her to reckon: overseer for who? like me and who? to appoint me and who? this to pasture which to stand: stand to/for face: before my
45 Sikilizeni mipango ambayo Yahwe ameamua juu ya Babeli, mipango aliyonayo dhidi ya nchi ya Wakaldayo. Kwa hakika wataondolewa, hata kundi dogo zaidi. Eneo lao la malisho litageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
to/for so to hear: hear counsel LORD which to advise to(wards) Babylon and plot his which to devise: devise to(wards) land: country/planet Chaldea if: surely yes not to drag them little [the] flock if: surely yes not be desolate: appalled upon them pasture
46 Kwa sauti ya kuangushwa kwa Babeli nchi inatikisika, na sauti ya mateso yao inasikiwa kati ya mataifa.”
from voice: sound to capture Babylon to shake [the] land: country/planet and outcry in/on/with nation to hear: hear

< Yeremia 50 >