< Yeremia 50 >

1 Hili ni neno alilolisema Yahwe juu ya Babeli, nchi ya Wakalidayo, kwa mkono wa Yeremia nabii,
The word that the Lord spoke concerning Babylon, concerning the land of the Chaldeans, by means of Jeremiah the prophet.
2 “Wajulishe mataifa ili wasikie. Toa ishara ili wasikie. Usiiache. Sema, 'Babeli imetwaliwa. Beli ameaibika. Merodaki amefadhaika. Sanamu zake zimeaibishwa; vinyago vyake vimefadhaika
Announce ye among the nations, and publish, and lift up a standard; publish, conceal not; say, Babylon is captured, Bel is put to shame, Merodach is broken in pieces; put to shame are her idols; broken in pieces are her images.
3 Taifa kutoka kaskazini litainuka kinyume chake, ili kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja, awe mtu au mnyama, atakayeishi ndani yake. Wataondoka.
For there is come up against her a nation out of the north, which will change her land into a desert, so that there shall not be any one dwelling therein: both man and beast are fled away, they are departed.
4 Katika siku hizo na wakati huo - hili ni tamko ya Yahwe - watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika ili kwenda kwa kulia na kumtafuta Yahwe Mungu wao.
In those days, and at that time, saith the Lord, shall the children of Israel come, they and the children of Judah together, going and weeping shall they go, and the Lord their God shall they seek.
5 Watauliza njia ya kwenda Sayuni nao watakwenda huko, wakisema, tutakwenda wenyewe ili kuungana na Yahwe katika agano la milele lisilosahaulikal
After Zion shall they ask, with their faces on the way thitherward, [saying, ] Come: and they will join themselves to the Lord in a perpetual covenant that shall not be forgotten.
6 Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea. Wachungaji wao wamewapoteza milimani; wamewageuza kutoka mlima hata mlima. Walikwenda, wakasahau mahali walipokuwa wanaishi.
Lost sheep were my people; their shepherds had caused them to go astray, they had let them roam wildly on the mountains: from mountain to hill did they go, they forgot their resting-place.
7 Kila awaendeaye anawararua. Washitaki wao walisema, 'Hatuna hatia, kwa sababu walimtenda dhambi Yahwe, nyumbani kwao halisi - Yahwe, tumaini la mababu zao.'
All that found them devoured them; and their adversaries said, We offend not, because they have sinned against the Lord, the habitation of righteousness, and the hope of their fathers, the Lord.
8 Tokeni kati ya Babeli; tokeni katika nchi ya Wakalidayo; iweni kama wafanyavyo mabeberu mbele ya kundi lote.
Fly away out of the midst of Babylon, and go forth out of the land of the Chaldeans, and be ye as the he-goats before the flocks.
9 Maana tazama, ninaelekea kupeleka na kuinua kinyume cha Babeli kundi la mataifa makubwa kutoka kaskazini. Yatajipanga yenyewe kinyume chake. Kutoka hapo Babeli utatekwa. Mishale yao ni kama shujaa mzoefu asiyerudi mikono tupu.
For, lo, I will awaken and cause to come up against Babylon an assemblage of great nations from the north country; and they shall set themselves in battle-array against her; from there shall she be captured: their arrows are as those of a skilful mighty one, none of which ever returneth in vain.
10 Ukaldayo itakuwa mateka. Wate waitekao wataridhika - asema Yahwe.
And Chaldea shall be given up to spoil: all that spoil her shall be satisfied, saith the Lord.
11 Mnafurahi, mnasherehekea kuteka urithi wangu; mnarukaruka kama ndama anayekanyaga katika malisho yake; mnalia kama farasi mwenye nguvu.
Though ye rejoice, though ye be glad, O ye plunderers of my heritage, though ye be grown fat as the heifer at grass, and neigh as stud-horses:
12 Hivyo mama yenu ataaibika sana; aliyewazaa atafadhaika. Tazama, atakuwa wa mwisho katika mataifa, nyika, nchi kame, na jangwa.
Your mother is made greatly ashamed; she that bore you is put to the blush; behold, the end of nations shall be wilderness, dry land, and desert.
13 Kwa sababu ya hasira ya Yahwe, Babeli haitakaliwa, lakini itakuwa ukiwa mtupu. Kila apitaye kando ataogopa kwa sababu ya Babeli na atatoa sauti kwa sababu ya majeraha yake.
Because of the wrath of the Lord shall it not be inhabited, and it shall be wholly desolate: every one that passeth by Babylon shall be astonished, and hiss over all her wounds.
14 Jipangeni wenyewe kumzunguka Babeli kinyume chake. Kila apindaye upinde na ampige. Msizuie mshale wenu wowote, maana amemtenda dhambi Yahwe.
Put yourselves in battle-array against Babylon round about, all ye that bend the bow, shoot at her, spare not the arrows: for against the Lord hath she sinned.
15 Pigeni kelele za ushindi kinyume chake ninyi nyote mmzungukao. Amesalimu mamlaka yake; minara yake imeanguka. Kuta zake zimebomolewa, maana hiki ni kisasi cha Yahwe. Jilipizeni kisasi juu yake! Mtendeeni kama alivyoyatenda mataifa mengine.
Shout against her round about; she hath stretched out her hand: fallen are her foundations, thrown down are her walls; for it is the vengeance of the Lord; take vengeance upon her; as she hath done, so do unto her.
16 Waaribuni wote mkulima apandaye mbegu naye atumiaye mundu wakati wa mavuno katika Babeli. Haya kila mtu na arudi kwa watu wake kutoka upanga wa mtesaji; na wakimbilie katika nchi yao wenyewe.
Cut off the sower from Babylon, and him that handleth the sickle in the time of harvest; because of the wasting sword shall they turn about every one to his people, and every one to his own land shall they flee.
17 Israeli ni kondoo aliyetawanywa na kupelekwa na simba mbali. Kwanza mfalme wa Ashuru alimrarua; kisha baadaye, Nebukadneza mfalme wa Babeli akavunja mifupa yake.
A scattered lamb is Israel; the lions have driven him away: first the king of Assyria devoured him; and this last one broke his bones, [even] Nebuchadrezzar the king of Babylon.
18 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Tazama, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
Therefore thus hath said the Lord of hosts, the God of Israel, Behold, I will inflict punishment on the king of Babylon and on his land, as I have punished the king of Assyria.
19 Nitamrudisha Israeli katika nchi yake; atajilisha katika Karmeli na Bashani. Kisha atajishibisha katika nchi ya kilima ya Efraimu na Gileadi.
And I will bring Israel back again to his habitation, and he shall feed on Carmel and Bashan: and upon the mountain of Ephraim and Gil'ad shall his soul be satisfied.
20 Siku hizo na wakati huo, asema Yahwe, uovu utatafutwa katika Israeli, lakini hautaonekana. Nitauliza kuhusu dhambi za Yuda, lakini hazitaonekana, maana nitawasamehe mabaki niliowaacha.”
In those days, and at that time, saith the Lord, shall the iniquity of Israel be sought for, and it shall not be there; and the sins of Judah, and they shall not be found; for I will pardon those whom I will leave remaining.
21 Inuka dhidi ya nchi ya Merathaimu, kinyume chake nao waishio Pekodi. Wapigeni kwa makali ya upanga na mwatenge kwa ajili ya maangamizo - asema Yahwe - fanyeni kila ninachowaamru.
Against the land of twofold rebellion—even against it go thou up, and against the inhabitants of the country of punishment: lay in ruins and utterly destroy their offspring, saith the Lord, and do in accordance with all that I have commanded thee.
22 Sauti ya vita na maangamizi ya kustaajabisha yamo katika nchi.
A sound of battle [is heard] in the land, and of great destruction.
23 Jinsi gani nyundo ya mataifa yote imekatiliwa mbali na kuharibiwa. Jinsi Babeli amekuwa kitu cha kushangaza kati ya mataifa.
How is cut asunder and broken the hammer of all the earth! how is Babylon become an astonishment among the nations!
24 Nimetega mtego dhidi yako. Umenaswa, Babeli, nawe haukutambua! Ulionekana na kukamatwa, tangu uliponidhihaki, Yahwe.
I have laid a snare for thee, and thou art also captured, O Babylon, while thou wast not aware: thou art found, and also caught, because thou hadst entered into a contest against the Lord.
25 Yahwe amefungua ghala lake la silaha na anachukua silaha kwa ajili ya kutekekeleza hasira yake. Kuna kazi kwa ajili ya Yahwe wa majeshi katika nchi ya Wakaldayo.
The Lord hath opened his treasury, and hath brought forth the weapons of his indignation; for it is a work for the Lord, the Eternal of hosts, in the land of the Chaldeans.
26 Mshambulie kutokea mbali. Fungua maghala yake ya chakula na kumrundika kama marundo ya nafaka. Mtenge mbali na maangamizi. Usimbakizie masalia.
Come against her from the end of the earth, open her garners; tread her down as sheaves of corn, and destroy her utterly: let there not be left of her a remnant even.
27 Ua madume wake wote wa ng'ombe. Washushe sehemu ya machinjio. Ole wao, maana siku yao imefika - wakati wa kuadhibiwa kwao.
Destroy all her bullocks; let them go down to the slaughter: Woe unto them! for their day is come, the time of their visitation.
28 Kuna sauti ya wale wanaokimbia, walionusurika, katika nchi ya Babeli. Hawa watatoa taarifa ya kisasi cha Yahwe Mungu wetu kwa Sayuni, kisasi kwa hekalu lake.”
There is the voice of those that flee and escape out of the land of Babylon, to tell in Zion the vengeance of the Lord our God, the vengeance for his temple.
29 Ita wapiga pinde dhidi ya Babeli - wale wote wapindao pinde zao. Piga kambi kinyume chake, na msimwache yeyote kutoroka. Mlipeni kwa kile alichofanya. Mfanyieni kwa kipimo alichotumia. Maana amemdharau Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
Call together the archers against Babylon; all ye that bend the bow, encamp against her round about; let there be no escape for her: recompense her according to her work; in accordance with all that she hath done, do unto her; for against the Lord hath she acted presumptuously, against the Holy One of Israel.
30 Hivyo vijana wake wataanguka katika viwanja vya mji, na wapiganaji wake wote wataangamizwa siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe.”
therefore shall her young men fall in her streets, and all her men of war shall perish on that day, saith the Lord.
31 Tazama, mimi ni kunyume chako, mwenye majivuno - hili ni tamko la Bwana Yahwe wa majeshi - maana siku yako imefika, mwenye kiburi, wakati nitakapokuadhibu.
Behold, I am against thee, O presumptuous one! saith the Lord, the Eternal of hosts; for thy day is come, the time that I will visit thee [with punishment].
32 Hivyo wenye kiburi watajikwaa na kuanguka. Hakuna atakaye wainua. Nitawasha moto katika miji yao; utateketeza kila kitu kati yake.
And the presumptuous shall stumble and fall, with none to raise him up: and I will kindle a fire in his cities, and it shall devour all his environs.
33 Yahwe wa majeshi asema hivi: watu wa Israeli wamenyanyaswa, pamoja na watu wa Yuda. Wate waliowateka bado wanawashikilia; wanakataa kuwaacha waondoke.
Thus hath said the Lord of hosts, The children of Israel and the children of Judah are oppressed together: and all that took them captive hold them fast; they refuse to dismiss them.
34 Yeye awaokoaye ni mwenye nguvu. Yahwe wa majeshi ni jina lake. Kwa hakika atalitetea shitaka lao, ili kuleta pumziko katika nchi, na kuwapiga wakaao Babeli.
Their Redeemer is strong; The Lord of hosts is his name: he will surely contend in their cause, in order that he may give rest to the land, and make the inhabitants of Babylon tremble.
35 Upanga u juu ya Wakalidayo - asema Yahwe - na juu ya wakaao Babeli, viongozi wake, na wenye hekima wake.
The sword is upon the Chaldeans, saith the Lord, and against the inhabitants of Babylon, and against her princes, and against her wise men.
36 Upanga unakuja juu ya waganga, ili wajione kuwa wajinga. Upanga utakuwa juu ya askari wake, hivyo watajaa hofu.
The sword is against the lying soothsayers, and they shall be made foolish: the sword is against her mighty men, and they shall be dismayed.
37 Upanga utakuwa juu ya farasi wake, vibandawazi vyao na na watu wote waliomo Babeli, hivyo watakuwa kama wanawake. Upanga utakuwa juu ya ghala zake, nazo zitatekwa.
The sword is against their horses, and against their chariots, and against all the confederates that are in the midst of her, and they shall become as women: the sword is against her treasures, and they shall be plundered.
38 Ukame unakuja juu ya maji yake, hivyo yatakauka. Maana ni nchi ya miungu wasiofaa, na wanafanya kama watu waliofanywa punguani kwa miungu yao isiyosaidia.
The drought is against her waters, and they shall be dried up; for it is the land of graven images, and with their horrid idols do they play the madman.
39 Hivyo wanyama wa jangwani wakaishi na mbwea wataishi huko, na watoto wa mbuni wataishi ndani yake. Kwa muda wote, hatakaliwa tena. Kutoka kizazi hata kizazi, hatakaliwa tena na watu.
Therefore shall martens dwell [there] with jackals, and the ostriches shall dwell therein: and it shall be not inhabited any more for ever; and it shall not be dwelt in from generation to generation.
40 Kama vile Mungu alivyoziangamiza Sodoma na Gomora na majirani zake - asema Yahwe - hakuna atakayeishi huko; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Like the overthrow by God of Sodom and Gomorrah and their neighbors, saith the Lord, so shall no man dwell there, nor shall any son of man sojourn therein.
41 “Tazama, watu wanakuja kutoka kaskazini, maana taifa kubwa na wafalme wengi wamemtikisa kutokea mbali.
Behold, a people cometh from the north, and a great nation, and many kings shall be awakened from the farthest ends of the earth.
42 Watachukua pinde na mishale. Ni wakatili na hawana huruma. Sauti yao ni kama mngurumo wa bahari, na wamepanda farasi katika mpangilio kama watu wapiganao, dhidi yako, bindi Babeli.
Bow and lance do they firmly grasp; they are cruel, and show not any mercy; their voice roareth like the sea, and upon horses do they ride, placed in array, like one man, for the battle, against thee, O daughter of Babylon.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari yao na mikono yake imelegea kwa huzuni. Mashaka yamemshika kama mwanamke katika utungu.
The king of Babylon hath heard the report of them, and his hands are grown feeble: anguish hath taken fast hold of him, pangs as of a woman in travail.
44 Tazama! Anakwenda juu kama simba atokaye katika miinuko ya Yordani kuelekea katika eneo la malisho ya uvumilivu. Maana kwa haraka nitawafanya wakimbie kutoka humo, nami nitamweka mtu aliyechaguliwa kwa uangalizi wake. Maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayeniagiza? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
Behold, like a lion shall he come up from the overflow of the Jordan unto the strong habitation; for I will hasten them [and] make them suddenly prevail over her, and him who is chosen will I array against her; for who like me? and who will challenge me to battle? and who is that shepherd that can stand before me?
45 Sikilizeni mipango ambayo Yahwe ameamua juu ya Babeli, mipango aliyonayo dhidi ya nchi ya Wakaldayo. Kwa hakika wataondolewa, hata kundi dogo zaidi. Eneo lao la malisho litageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Therefore hear ye the counsel of the Lord, that he hath resolved against Babylon; and his purposes, that he hath devised against the land of the Chaldeans: Surely the least of the flock shall drag them away; surely he will devastate over them their habitation.
46 Kwa sauti ya kuangushwa kwa Babeli nchi inatikisika, na sauti ya mateso yao inasikiwa kati ya mataifa.”
At the noise of the conquest of Babylon the earth quaketh, and the outcry is heard among the nations.

< Yeremia 50 >