< Yeremia 5 >
1 Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
« Parcourez de long en large les rues de Jérusalem, et regardez maintenant, et sachez, et cherchez dans ses lieux écartés, si vous pouvez trouver un homme, s'il y a quelqu'un qui agisse avec justice, qui recherche la vérité, alors je lui pardonnerai.
2 Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
Même s'ils disent: « L'Éternel est vivant », ils jurent faussement. »
3 BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
O Yahvé, tes yeux ne regardent-ils pas la vérité? Tu les as frappés, mais ils n'ont pas été affligés. Tu les as consumés, mais ils ont refusé de se laisser corriger. Ils ont rendu leur visage plus dur que le roc. Ils ont refusé de revenir.
4 Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
Et je dis: « Ceux-là sont pauvres. Ils sont insensés, car ils ne connaissent pas la voie de l'Éternel, ni la loi de leur Dieu.
5 Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
Je vais aller vers les grands et je leur parlerai, car ils connaissent la voie de l'Éternel et la loi de leur Dieu. » Mais eux, d'un commun accord, ont brisé le joug, et rompu les liens.
6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
C'est pourquoi le lion de la forêt les tuera, le loup du soir les fera mourir. Le loup des soirs les détruira. Un léopard veillera sur leurs villes. Tous ceux qui sortent de là seront déchirés, parce que leurs transgressions sont nombreuses et que leur égarement s'est accru.
7 Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
« Comment pourrais-je te pardonner? Tes enfants m'ont abandonné, et ils ont juré par ce qui n'est pas un dieu. Après que je les ai rassasiés, ils ont commis l'adultère, et se sont rassemblés en troupes dans les maisons de prostitution.
8 Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
Ils étaient comme des chevaux nourris, errant en liberté. Chacun hennissait après la femme de son voisin.
9 Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
Ne devrais-je pas les punir pour ces choses? dit Yahvé. « Mon âme ne doit-elle pas se venger d'une telle nation?
10 Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
« Montez sur ses murs, détruisez, mais ne détruisez pas tout. Enlève ses branches, car elles ne sont pas à Yahvé.
11 Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
Car la maison d'Israël et la maison de Juda se sont montrées très perfides à mon égard, dit l'Éternel.
12 na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
Ils ont renié Yahvé, et ils ont dit: « Ce n'est pas lui. Le mal ne viendra pas sur nous. Nous ne verrons ni épée ni famine.
13 Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
Les prophètes seront du vent, et la parole n'est pas en eux. C'est ainsi qu'il leur sera fait. »
14 Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
C'est pourquoi Yahvé, le Dieu des armées, dit: « Parce que tu dis cela, voici, je ferai de mes paroles dans ta bouche du feu, et de ce peuple du bois, et il les dévorera.
15 Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
Voici, je vais faire venir sur vous une nation lointaine, maison d'Israël, dit l'Éternel. « C'est une nation puissante. C'est une nation ancienne, une nation dont vous ne connaissez pas la langue et dont vous ne comprenez pas ce qu'elle dit.
16 Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
Leur carquois est un tombeau ouvert. Ils sont tous des hommes puissants.
17 Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
Ils dévoreront ta moisson et ton pain, que tes fils et tes filles doivent manger. Ils dévoreront tes brebis et tes bœufs. Ils dévoreront tes vignes et tes figuiers. Ils abattront par l'épée tes villes fortifiées dans lesquelles tu te confies.
18 Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
« Mais même en ces jours-là, dit l'Éternel, je ne vous détruirai pas complètement.
19 Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
Quand vous direz: « Pourquoi Yahvé, notre Dieu, nous a-t-il fait toutes ces choses? Alors tu leur diras: « De même que vous m'avez abandonné pour servir des dieux étrangers dans votre pays, de même vous servirez des étrangers dans un pays qui n'est pas le vôtre ».
20 Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
Annoncez-le dans la maison de Jacob, et publiez-le en Juda, en disant:
21 'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
Écoutez ceci, peuple insensé et sans intelligence, qui avez des yeux et ne voyez pas, qui avez des oreilles et n'entendez pas.
22 Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
Ne me craignez-vous pas, dit l'Éternel, ne tremblez-vous pas devant moi, qui ai mis le sable à la limite de la mer, par un décret perpétuel, pour qu'elle ne la dépasse pas? Ses vagues ont beau s'agiter, elles ne peuvent l'emporter. Elles ont beau rugir, elles ne peuvent passer par-dessus.
23 Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
« Mais ce peuple a un cœur révolté et rebelle. Ils se sont révoltés et sont partis.
24 Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
Ils ne disent pas en leur cœur: « Craignons maintenant Yahvé, notre Dieu, qui donne la pluie, la première et l'arrière-saison, en son temps, qui nous réserve les semaines fixes de la moisson.
25 uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
« Vos iniquités ont détourné ces choses, et vos péchés ont retenu le bien.
26 Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
Car il se trouve des méchants parmi mon peuple. Ils guettent, comme les oiseleurs se tiennent aux aguets. Ils tendent un piège. Ils attrapent les hommes.
27 Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
Comme une cage est pleine d'oiseaux, ainsi leurs maisons sont pleines de tromperie. C`est pourquoi ils sont devenus grands, ils se sont enrichis.
28 Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
Ils se sont engraissés. Ils brillent; oui, ils excellent dans les actes de méchanceté. Ils ne plaident pas la cause, la cause de l'orphelin, pour prospérer, et ils ne défendent pas les droits des nécessiteux.
29 Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
« Ne devrais-je pas punir pour ces choses? » dit Yahvé. « Mon âme ne devrait-elle pas se venger d'une telle nation?
30 Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
« Une chose étonnante et horrible est arrivée dans le pays.
31 Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?
Les prophètes prophétisent faussement, et les prêtres gouvernent par leur propre autorité; et mon peuple aime qu'il en soit ainsi. Que ferez-vous à la fin de tout cela?