< Yeremia 5 >

1 Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
“Rush about through the streets of Jerusalem; search in her city squares, too. Then look and think about this: If you can find a man or anyone who is acting justly and trying to act faithfully, then I will forgive Jerusalem.
2 Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
Although they say, 'As Yahweh lives,' yet they are swearing falsely.”
3 BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
Yahweh, do your eyes not look for faithfulness? You struck the people, but they do not feel pain. You have completely defeated them, but they still refuse to receive discipline. They make their faces harder than rock, for they refuse to repent.
4 Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
So I said, “Surely these are only poor people. They are foolish, for they do not know Yahweh's ways, nor their God's decrees.
5 Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
I will go to the important people and declare God's messages to them, for they at least know Yahweh's ways, the decrees of their God.” But they all broke their yoke together; they all tore apart the chains that bound them to God.
6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
So a lion from a thicket will attack them. A wolf from the Arabah will ruin them. A lurking panther will come against their cities. Anyone who goes outside his city will be torn apart. For their transgressions increase. Their acts of faithlessness are unlimited.
7 Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
Why should I pardon these people? Your sons have abandoned me and have made oaths by what are not gods. I fed them fully, but they committed adultery and walked in great numbers to the houses of prostitutes.
8 Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
They were horses in heat. They roamed about wanting to mate. Each man neighed to his neighbor's wife.
9 Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
So should I not punish them—this is Yahweh's declaration— and should I not avenge myself on a nation that is like this?
10 Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
Go up onto her vineyards' terraces and destroy. But do not bring complete destruction to them. Trim their vines, since those vines do not come from Yahweh.
11 Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
For the houses of Israel and Judah have completely betrayed me—this is Yahweh's declaration.
12 na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
They have spoken falsely about Yahweh and they said, “He will do nothing; no harm will come upon us, and we will not see sword or famine.
13 Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
The prophets will become wind, the word is not in them, so let what they say be done to them.”
14 Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
So Yahweh, the God of hosts says this, “Because you have said this, see, I am about to place my word in your mouth. It will be like a fire, and this people will be like wood! For it will consume them.
15 Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
Behold! I am about to bring a nation against you from far away, house of Israel—this is Yahweh's declaration— it is a lasting nation, an ancient nation! It is a nation whose language you do not know, nor will you understand what they say.
16 Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
Its quiver is like an open tomb. They are all soldiers.
17 Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
So your harvest will be consumed, your sons and daughters also, and your food. They will eat your flocks and cattle; they will eat the fruit from your vines and fig trees. They will beat down with a sword your fortified cities that you trusted in.
18 Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
But even in those days—this is Yahweh's declaration—I do not intend to destroy you completely.
19 Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
When you, Israel and Judah, say, 'Why has Yahweh our God done all these things to us?' then you, Jeremiah, will say to them, 'Just as you abandoned Yahweh and served foreign gods in your land, so you must also serve strangers in a land that is not your own.'
20 Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
Report this to the house of Jacob and let it be heard in Judah. Say,
21 'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
'Hear this, you foolish people who have no understanding; who have eyes but you cannot see, and you have ears but you cannot hear.
22 Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
Do you not fear me—this is Yahweh's declaration—or tremble before my face? I have placed a border of sand against the sea, an ongoing decree that it does not violate— even though the sea rises and falls, still it does not violate it. Even though its waves roar, they do not cross it.
23 Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
But this people has a stubborn heart. It turns away in rebellion and goes away.
24 Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
For they do not say in their hearts, “Let us fear Yahweh our God, the one who brings the rain —the early rain and the late rains—in their right time, keeping the fixed weeks of the harvest for us.”
25 uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
Your iniquities kept these things from happening. Your sins have stopped good from coming to you.
26 Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
For wicked men are found with my people. They watch as someone crouches to capture birds; they set a trap and catch people.
27 Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
Like a cage full of birds, their houses are full of deceit. So they grow large and become rich.
28 Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
They have become fat; they shine with well-being. They crossed over all bounds of wickedness. They do not plead the cause of the people, or the cause of the orphan. They prosper even though they have not given justice to the needy.
29 Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
Should I not punish them for these things—this is Yahweh's declaration— and will I not take vengeance for myself on a nation like this?
30 Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
Atrocities and horrors have occurred in the land.
31 Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?
The prophets prophesy with deceit, and the priests rule with their own power. My people love it this way, but what will happen in the end?'”

< Yeremia 5 >