< Yeremia 5 >
1 Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
Run you to and fro through the streets of Jerusalem, and see now, and know, and seek in the broad places thereof, if you can find a man, if there be any that executes judgment, that seeks the truth; and I will pardon it.
2 Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
And though they say, The LORD lives; surely they swear falsely.
3 BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
O LORD, are not your eyes on the truth? you have stricken them, but they have not grieved; you have consumed them, but they have refused to receive correction: they have made their faces harder than a rock; they have refused to return.
4 Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
Therefore I said, Surely these are poor; they are foolish: for they know not the way of the LORD, nor the judgment of their God.
5 Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
I will get me to the great men, and will speak to them; for they have known the way of the LORD, and the judgment of their God: but these have altogether broken the yoke, and burst the bonds.
6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
Why a lion out of the forest shall slay them, and a wolf of the evenings shall spoil them, a leopard shall watch over their cities: every one that goes out there shall be torn in pieces: because their transgressions are many, and their backslidings are increased.
7 Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
How shall I pardon you for this? your children have forsaken me, and sworn by them that are no gods: when I had fed them to the full, they then committed adultery, and assembled themselves by troops in the harlots’ houses.
8 Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
They were as fed horses in the morning: every one neighed after his neighbor’s wife.
9 Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
Shall I not visit for these things? says the LORD: and shall not my soul be avenged on such a nation as this?
10 Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
Go you up on her walls, and destroy; but make not a full end: take away her battlements; for they are not the LORD’s.
11 Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
For the house of Israel and the house of Judah have dealt very treacherously against me, says the LORD.
12 na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
They have belied the LORD, and said, It is not he; neither shall evil come on us; neither shall we see sword nor famine:
13 Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
And the prophets shall become wind, and the word is not in them: thus shall it be done to them.
14 Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
Why thus says the LORD God of hosts, Because you speak this word, behold, I will make my words in your mouth fire, and this people wood, and it shall devour them.
15 Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
See, I will bring a nation on you from far, O house of Israel, says the LORD: it is a mighty nation, it is an ancient nation, a nation whose language you know not, neither understand what they say.
16 Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
Their quiver is as an open sepulcher, they are all mighty men.
17 Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
And they shall eat up your harvest, and your bread, which your sons and your daughters should eat: they shall eat up your flocks and your herds: they shall eat up your vines and your fig trees: they shall impoverish your fenced cities, wherein you trusted, with the sword.
18 Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
Nevertheless in those days, says the LORD, I will not make a full end with you.
19 Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
And it shall come to pass, when you shall say, Why does the LORD our God all these things to us? then shall you answer them, Like as you have forsaken me, and served strange gods in your land, so shall you serve strangers in a land that is not yours.
20 Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
Declare this in the house of Jacob, and publish it in Judah, saying,
21 'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
Hear now this, O foolish people, and without understanding; which have eyes, and see not; which have ears, and hear not:
22 Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
Fear you not me? says the LORD: will you not tremble at my presence, which have placed the sand for the bound of the sea by a perpetual decree, that it cannot pass it: and though the waves thereof toss themselves, yet can they not prevail; though they roar, yet can they not pass over it?
23 Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
But this people has a revolting and a rebellious heart; they are revolted and gone.
24 Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
Neither say they in their heart, Let us now fear the LORD our God, that gives rain, both the former and the latter, in his season: he reserves to us the appointed weeks of the harvest.
25 uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
Your iniquities have turned away these things, and your sins have withheld good things from you.
26 Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
For among my people are found wicked men: they lay wait, as he that sets snares; they set a trap, they catch men.
27 Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
As a cage is full of birds, so are their houses full of deceit: therefore they are become great, and waxen rich.
28 Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
They are waxen fat, they shine: yes, they overpass the deeds of the wicked: they judge not the cause, the cause of the fatherless, yet they prosper; and the right of the needy do they not judge.
29 Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
Shall I not visit for these things? says the LORD: shall not my soul be avenged on such a nation as this?
30 Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
A wonderful and horrible thing is committed in the land;
31 Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?
The prophets prophesy falsely, and the priests bear rule by their means; and my people love to have it so: and what will you do in the end thereof?