< Yeremia 49 >

1 Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
Esto es lo que dice el Señor sobre los amonitas: ¿Acaso los israelitas no tienen hijos? ¿No tienen herederos que hereden sus bienes? Entonces, ¿por qué Milcom se apoderó del territorio perteneciente a la tribu de Gad? ¿Por qué su gente vive en sus ciudades?
2 Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
¡Cuidado! Se acerca el momento, declara el Señor, en que señalaré el ataque a la ciudad amonita de Rabá. Se convertirá en un montón de ruinas, y sus pueblos serán incendiados. Entonces los israelitas expulsarán a los pueblos que se apoderaron de su tierra, dice el Señor.
3 Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
Lloren, pueblos de Hesbón, porque la ciudad de Hai ha sido destruida. Clamen por ayuda, pueblo de Rabá. Pónganse ropas de cilicio y comiencen a llorar; corran de un lado a otro dentro de los muros de su ciudad, porque su dios Milcom irá al exilio junto con sus sacerdotes y líderes.
4 Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
¿Por qué te jactas de que tus valles son tan productivos, pueblo infiel? Confían en sus riquezas, diciendo: “¿Quién se atreverá a atacarnos?”.
5 Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
¡Cuidado! Voy a traer a las naciones de alrededor para aterrorizarlos, declara el Señor Dios Todopoderoso. Todos ustedes serán expulsados y dispersados, y nadie podrá volver a reunir a los refugiados.
6 Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
Sin embargo, más adelante los haré volver del exilio a los amonitas, declara el Señor.
7 Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
Esto es lo que dice el Señor Todopoderoso sobre Edom: ¿No queda ninguna persona sabia en Temán? ¿No hay ningún buen consejo de los que tienen visión? ¿Se ha podrido su sabiduría?
8 Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
¡Vuelvan y huyan! Busquen un lugar donde esconderse, pueblo de Dedán, porque voy a hacer caer el desastre sobre ustedes, descendientes de Esaú, cuando los castigue.
9 Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
Si viniera gente a cosechar uvas, dejaría algunas, ¿no es así? Si vinieran ladrones durante la noche, sólo robarían lo que quisieran, ¿no es así?
10 Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
Pero yo voy a desnudar todo el país, dejando a su gente sin ningún lugar donde esconderse. Todos los descendientes de Esaú serán destruidos, junto con sus parientes y amigos; todos desaparecerán.
11 Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
Sin embargo, puedes dejarme a tus huérfanos porque yo los protegeré. Haz que tus viudas pongan su confianza en mí.
12 Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
Esto es lo que dice el Señor: Si los que no tuvieron que beber de la copa del juicio tuvieron que hacerlo, ¿cómo no van a ser castigados ustedes? No se quedarán impunes, porque también tienen que beberla.
13 Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
Me hice la solemne promesa, declara el Señor, de que la ciudad de Bosra se convertirá en un lugar que horrorice a la gente, en una completa humillación, en un montón de ruinas y en un nombre que se use como palabra de maldición. Todos sus pueblos circundantes también quedarán en ruinas para siempre.
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
He recibido este mensaje del Señor. Ha enviado un mensajero a las naciones: ¡Prepárense para atacar a Edom! ¡Prepárense para la batalla!
15 “Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
Vean cómo los haré insignificantes en comparación con otras naciones; todos los mirarán con desprecio.
16 Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
El miedo que una vez causaron en los demás, y el orgullo que llevan por dentro los ha engañado, dándoles un exceso de confianza, ustedes que viven en las cimas de las montañas rocosas. Aunque hagan sus casas en lo alto, fuera de su propio alcance, como un nido de águilas, incluso de allí los derribaré, declara el Señor.
17 Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
La gente se horrorizará de lo que le ha ocurrido a Edom. Todos los que pasen por allí se escandalizarán y se burlarán de todo su daño.
18 Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
Así como Sodoma y Gomorra fueron destruidas, junto con sus ciudades vecinas, dice el Señor, nadie vivirá allí; quedarán deshabitadas.
19 Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
¡Cuidado! Voy a salir como un león de la maleza junto al Jordán para atacar a los animales que pastan los verdes pastos. De hecho, voy a expulsar a los edomitas de su tierra muy rápidamente. ¿A quién elegiré para conquistarlos? ¿Quién es como yo? ¿Quién puede desafiarme? ¿Qué líder ¿podría oponerse a mí?
20 Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Así que escucha lo que el Señor ha planeado hacer a Edom y al pueblo de Temán: Sus hijos serán arrastrados como corderos del rebaño, y por su culpa sus pastos se convertirán en un páramo.
21 Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
Cuando caigan, el ruido que hagan hará temblar la tierra; sus gritos se oirán hasta el Mar Rojo.
22 Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
Mira como un enemigo como un águila vuela alto, y luego se abalanza, extendiendo sus alas mientras ataca a Bosra. En ese momento los guerreros de Edom estarán tan asustados como una mujer de parto.
23 Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
Una profecía sobre Damasco: Las ciudades de Hamat y Arpad están perturbados, porque han recibido malas noticias. Están temerosos, inquietos como el mar. Nada puede calmar sus preocupaciones.
24 Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
Los habitantes de Damasco están desmoralizados; se vuelven y huyen despavoridos, invadidos por el dolor y la angustia como una parturienta.
25 Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
¿Por qué la ciudad alabada no está desierta, la ciudad que me hizo feliz?
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
Porque ese día sus jóvenes morirán en sus calles, todos sus defensores serán asesinados, declara el Señor de los Ejércitos.
27 “Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
Voy a prender fuego a las murallas de Damasco; eso quemará las fortalezas de Ben-Hadad.
28 Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
Profecía sobre la tierra de Cedar y los reinos de Hazor que fueron atacados por Nabucodonosor, rey de Babilonia. Esto es lo que dice el Señor: Ve y ataca a Cedar; ¡destruye a los pueblos del oriente!
29 Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
¡Toma sus tiendas y sus rebaños! Llévense las cortinas de sus tiendas y todas sus posesiones. Tomen sus camellos para ustedes. Gritadles: “¡El terror está en todas partes!”
30 Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
Corran! ¡Aléjense lo más que puedan! Busquen un lugar donde esconderse, pueblo de Hazor, declara el Señor. Porque Nabucodonosor, rey de Babilonia, ha hecho planes para atacarlos y destruirlos.
31 Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
Vayan y ataquen esa nación autocomplaciente que se cree segura, declara el Señor. No tienen puertas cerradas y no tienen aliados.
32 Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
Sus camellos y grandes rebaños serán un botín para ti. Los dispersaré por todas partes, a este pueblo del desierto que se recorta el pelo a los lados de la cabeza. Haré descender sobre ellos un desastre desde todas las direcciones, declara el Señor.
33 Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
Hazor se convertirá en un lugar donde viven chacales, un lugar abandonado para siempre. Nadie vivirá allí; quedará deshabitado.
34 Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
Este es el mensaje del Señor que llegó al profeta Jeremías sobre Elam. Esto fue al comienzo del reinado de Sedequías, rey de Judá.
35 “Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
Esto es lo que dice el Señor Todopoderoso: Mira, voy a destrozar los arcos de los elamitas, el arma en la que confían para su poder.
36 Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
Traeré vientos de todas las direcciones para atacar a Elam, y los dispersaré en todas direcciones. No habrá nación que no tenga algunos exiliados de Elam.
37 Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
Aplastaré a los elamitas frente a sus enemigos, ante los que quieren matarlos. En mi furioso enojo haré caer el desastre sobre ellos, declara el Señor. Los perseguiré con la espada hasta destruirlos.
38 Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
En Elam instalaré mi trono y destruiré a su rey y a sus funcionarios, declara el Señor.
39 na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”
Sin embargo, más adelante haré volver a los elamitas del exilio, declara el Señor.

< Yeremia 49 >