< Yeremia 49 >

1 Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
К сыном Аммоним тако глаголет Господь: еда не суть сынове Израилевы, или наследника несть им? Почто убо прия наследие Мелхом Гада, и людие его во градех его живяху?
2 Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
Сего ради, се, дние грядут, глаголет Господь, и оглашу на Равваф сынов Аммоних ратный звук, и будет в непроходная и в пагубу, и требища его огнем сожжена будут, и восприимет Израиль власть свою, глаголет Господь.
3 Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
Возопий, Есевоне, яко погибе Гай: возопийте, дщери Раввафски, препояшитеся вретищами, рыдайте и бегайте по забралом, яко Мелхом во плен отведется, священницы и князи его вкупе.
4 Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
Что хвалишися во удолиих? Стече удолие твое, дщи безстудная, уповающая на богатства своя, глаголющи: кто приидет на мя?
5 Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
Се, Аз наведу на тя страх, глаголет Господь Вседержитель, от всех сущих окрест тебе: и разсеетеся вси от лица его, и не будет собирающаго бежащих.
6 Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
И посем возвращу пленники сынов Аммоних, глаголет Господь.
7 Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
Ко Идумеи сия глаголет Господь Вседержитель: еда есть ктому мудрость во Фемане? Погибе совет от разумных, непотребна бысть мудрость их,
8 Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
попрано бысть место их: снидите в пропасть к седению, живущии во Дедане: яко жестокая сотвори: (погибель Исавлю) наведох нань во время, в неже посетих его.
9 Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
Яко оымателие вина приидоша на тя, не оставят тебе останков: аки татие в нощи возложат руки своя.
10 Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
Яко (Аз) обнажих Исава, открых тайная его, не возможет утаитися, погибе рукою брата своего и соседа своего,
11 Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
и несть остатися сироте твоей, да живет: Аз же сотворю жити, и вдовицы на Мя уповаша.
12 Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
Тако бо глаголет Господь: се, имже не бе закона пити чашу, пиюще испиют: и ты ли аки неповинный останешися? Не будеши неповинен, но пия испиеши.
13 Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
Собою бо кляхся, глаголет Господь, яко в пустыню и в поругание и в посмех и в проклятие будеши посреде его, и вси гради его будут в пустыню вечную.
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
Слух слышах от Господа, и послов во языки посла: соберитеся и идите противу ему и востаните на ополчение.
15 “Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
Се, мала дах тя во языцех и поругаема в людех.
16 Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
Играние твое прельсти тя, безстудие сердца твоего обиташе в разселинах каменных, похити крепость холма высокаго: егда вознесеши яко орел гнездо свое, оттоле свергу тя, глаголет Господь.
17 Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
И будет Идумеа в запустение, всяк ходяй чрез ню подивится и позвиждет над всякою язвою ея.
18 Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
Якоже превращена есть Содома и Гоморра и соседи ея, глаголет Господь, не поживет тамо муж, ниже пребудет тамо сын человечь.
19 Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
Се, якоже лев изыдет от среды Иордана на место сильнаго, яко скоро сотворю им бежати от него, и кто будет избран, егоже поставлю над ним? Кто бо подобен Мне? И кто противостанет Ми? И кто есть сей пастырь, иже сопротивится лицу Моему?
20 Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Сего ради слышите совет Господень, егоже совеща на Едома, и умышление Его, еже умысли на живущих во Фемане, не свергут ли их малая от стад, и не разметано ли будет на них жилище их?
21 Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
От гласа бо падения их потрясеся земля, и вопль на мори Чермнем слышася гласа их.
22 Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
Се, яко орел взыдет и возлетит и прострет криле свои над твердыньми его: и будет сердце сильных Идумейских в той день, яко сердце жены родящия.
23 Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
К Дамаску: посрамися Емаф и Арфаф, яко слух зол слышаша, ужасошася, возмутишася на мори, (за попечение) упокоитися не могут.
24 Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
Расторжеся Дамаск, обратися на бежание, трепет объят и, скорбь и болезнь одержаша его яко раждающую.
25 Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
Како не оставиша града славнаго, крепости любезныя?
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
Сего ради падут юноши на стогнах твоих, и вси мужие воинстии падут в той день, глаголет Господь Вседержитель.
27 “Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
И возжгу огнь на стене Дамаска, и пожжет стены сына Адерова.
28 Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
К Кидару, царице двора, егоже порази Навуходоносор царь Вавилонский, тако глаголет Господь: востаните и взыдите на Кидар и погубите сыны восточныя.
29 Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
Селения их и стада их возмут: одежды их и вся сосуды их и велблюды их возмут себе, и призовут на ня страх окрест.
30 Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
Бежите и отидите вскоре, в пропастех сядите, живущии во дворе, глаголет Господь: яко совеща на вы Навуходоносор царь Вавилонский совет и помысли на вас умышление.
31 Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
Востаните и внидите к людем упокоеным, живущым в прохладе, глаголет Господь: иже ни дверий, ниже заворов имут, едини обитают.
32 Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
И будут велблюды их в расхищение и множество скота их в разграбление, и развею я всяким ветром остриженых окрест, и от всех окрестных их приведу на ня погибель, глаголет Господь.
33 Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
И будет двор в жилище змием и пуст даже до века, не поживет тамо муж, ниже будет живяй в нем сын человечь.
34 Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
Слово Господне, еже бысть ко Иеремии пророку на Елам, в начале царства Седекии царя Иудина, глаголя:
35 “Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
тако глаголет Господь Вседержитель: се, Аз сокрушу лук Еламль, начало силы их,
36 Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
и наведу на Елам четыри ветры от четырех стран небесных и развею я во вся ветры тыя, и не будет языка, в оньже бы не пришли бежащии Еламитяне.
37 Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
И устрашу их пред враги их и пред лицем ищущих души их, и наведу на ня злая, по гневу ярости Моея, глаголет Господь: и послю вслед их мечь Мой, дондеже сотру их:
38 Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
и поставлю престол Мой во Еламе, и иждену оттуду царя и князи, глаголет Господь:
39 na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”
и будет в последния дни, возвращу плен Еламль, глаголет Господь.

< Yeremia 49 >