< Yeremia 49 >
1 Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
Of the sons of Ammon-Thus saith Yahweh: Hath Israel no, sons? Hath he no, heir? Why hath, Malkam, taken possession of Gad, Or have, his people, in the cities thereof, made their dwelling?
2 Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
Therefore, lo! days are coming, Declareth Yahweh When I will cause to be heard against Rabbah of the sons of Ammon, an alarm of war, So shall she become a mound of desolation, And, her villages, with fire, shall blaze, —Then shall Israel, inherit them who inherited him, Saith Yahweh.
3 Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
Howl, O Heshbon, for Ai is spoiled Make outcry, ye daughters of Rabbah, Gird you with sackcloth, Lament ye and run to and fro among the fences, —For, Malkam, into captivity, shall go, His priests and his princes, together.
4 Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
Why shouldst thou glory in the vales, The flowing of thy vale O apostate daughter? She who is trusting in her treasures, [saying, ] Who shall invade, me?
5 Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
Behold me! bringing upon thee, terror Declareth My Lord, Yahweh of hosts, From all who are round about thee, —And ye shall be driven out every man before it, And there shall be none to bring home the wanderer;
6 Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
But afterwards, will I bring back the captivity of the sons of Ammon, Declareth Yahweh.
7 Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
Of Edom—Thus, saith Yahweh of hosts, Is there no longer wisdom in Teman? Hath counsel perished from the discerning? Is their wisdom corrupt?
8 Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
Flee ye turn go down deep to dwell, O inhabitant of Dedan, —For the doom of Esau, have I brought in upon him The time of his visitation.
9 Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
If, grape-gatherers, came to thee, Would they not leave, gleanings? If, thieves in the night, Would they not have taken away what sufficed them?
10 Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
But, I, have stripped Esau bare, I have uncovered his secret places, And to conceal himself, shall he not be able! Spoiled, are his seed, and his brethren, and his neighbours, and he is not.
11 Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
Leave thy fatherless children I, will preserve them alive, —And thy widows, In me, let them trust.
12 Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
For, thus saith Yahweh—Lo! they who had not been adjudged to drink the cup, shall surely drink, And art thou, the one to go unpunished? Thou shalt not go unpunished, but shalt surely drink.
13 Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
For by myself, have I sworn, Declareth Yahweh, That, Bozrah shall become, an astonishment: a reproach and a desolation, and a contempt, —And all her cities shall become age-abiding desolations.
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
A report, have I heard from Yahweh, Yea, an envoy, throughout the nations, hath been sent, —Gather yourselves together and come against her, And arise to the battle.
15 “Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
For lo! Small, have I made thee among the nations, —Despised among men!
16 Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
Thy monstrous thing, hath deceived thee, The insolence of thy heart, O thou that inhabitest the hidden recesses of the cliff, That holdest fast the height of the hill, —Though thou set high as an eagle, thy nest, From thence, will I bring thee down, Declareth Yahweh;
17 Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
So shall, Edom, become an astonishment, —Every one passing by her, will be astonished and hiss, over all her plagues:
18 Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
Like the overthrow of Sodom and Gomorrah and her neighbours, Saith Yahweh, —There shall not dwell there—a man, Nor sojourn therein—any son of the earth-born.
19 Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
Lo! like a lion, will he come up from the majesty of the Jordan, unto the pasture perennial, But I will wink—I will make him run away therefrom, Who then shall be the Chosen One whom over it, I may set in charge? For who shall be like unto, me? And who shall appoint me, a time? And who is the Shepherd that shall stand before, me?
20 Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Wherefore, hear ye The counsel of Yahweh which he hath counseled against Edom, And his devices which he hath devised against the inhabitants of Teman, —Surely the little ones of the flock shall drag them away, Surely he will cause their fold to be astounded over them.
21 Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
At the noise of their fall, hath trembled the earth, At the outcry, in the Red Sea, was heard its noise.
22 Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
Lo! as an eagle, he shall mount and dart, and spread his wings over Bozrah, —So shall the heart of the heroes of Edom, in that day, become as the heart of a woman in her pain.
23 Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
Of Damascus. Turned pale have Hamath and Arpad, For, a calamitous report, have they heard—they tremble, —In the sea, is anxiety, it cannot, rest.
24 Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
Enfeebled is Damascus She hath turned to flee But terror, hath seized her, —Anguish and pangs, have seized her as a woman in childbirth.
25 Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
Alas! is she not forsaken—The city so praised! The citadel I rejoiced in!
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
Therefore shall her young men fall in her broadways, —And, all her men of war, shall be silent in that day, Declareth Yahweh of hosts;
27 “Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
Then will I kindle a fire in the walls of Damascus, —And it shall devour the palaces of Ben-hadad.
28 Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
Of Kedar. And of the kingdoms of Hazor Which Nebuchadrezzar king of Babylon smote—Thus, saith Yahweh, —Arise ye go up against Kedar, So shall they spoil the sons of the East:
29 Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
Their tents and their flocks, shall they take, And their curtains and all their baggage and their camels, shall they carry off for themselves, —And shall cry out unto them, Terror round about!
30 Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
Flee remove far away, go deep to dwell, Ye inhabitants of Hazor, Urgeth Yahweh; For Nebuchadrezzar king of Babylon—hath counseled against you, a counsel, And devised against you a device.
31 Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
Arise ye, go up against a nation at ease—dwelling securely, Commandeth Yahweh, —Having neither doors nor bars, Alone, do they dwell:
32 Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
So shall their camels, become, a prey, And the throng of their cattle, a spoil, Then will I scatter them to every wind even the clipt-beards, —And from all sides of him, will I bring in their doom Declareth Yahweh.
33 Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
So shall Hazor become A habitation of jackals An astonishment unto times age-abiding: There shall not dwell there—a man, Nor sojourn therein—a son of the earth-born.
34 Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
So much of the word of Yahweh as came unto Jeremiah the prophet, Against Elam, —in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah saying: —
35 “Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
Thus, saith Yahweh of hosts, Behold me! breaking the bow of Elam, —The beginning of their might;
36 Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
Then will I bring in against Elam four winds from the four quarters of the heavens, And will scatter them to all these winds, —And there shall be no nation whither the outcasts of Elam, shall not come;
37 Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
And I will cause Elam to be dismayed Before their enemies Even before them who are seeking their life, So will I bring upon them calamity, Even the glow of mine anger Declareth Yahweh, —And will send after them the sword, until I have made an end of them;
38 Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
And I will set my throne in Elam, —And will destroy, from thence king and princes, Declareth Yahweh;
39 na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”
But it shall come to pass In the afterpart of the days, That I will bring back the captivity of Elam, Declareth Yahweh.