< Yeremia 49 >
1 Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
Concerning the children of Ammon. Thus saith Jehovah: Hath Israel no sons? Hath he not an heir? Why then doth Milcom inherit Gad, And his people dwell in his cities?
2 Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
Therefore, behold, the days come, saith Jehovah, That I will cause a cry of war to be heard against Rabbah of the sons of Ammon, And she shall become a ruinous heap, And her daughters shall be burned with fire; And Israel shall take possession of their land, who took possession of his.
3 Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
Howl, O Heshbon, for Ai is laid waste! Cry, ye daughters of Rabbah, Gird yourselves with sackcloth, lament, And run ye to and fro within the fences! For Milcom goeth into captivity, His priests and his princes together.
4 Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
Wherefore dost thou glory in the valleys? Thy valley shall flow [[with blood]], O perverse daughter, That gloriest in thy treasures, [[Saying, ]] “Who shall come against me?”
5 Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
Behold, I will bring a terror upon thee, saith Jehovah of hosts, From all those that are around thee, And ye shall be driven out, every one right forth, And there shall be none to gather up the fugitives.
6 Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
But after this will I bring back the captivity of the sons of Ammon, saith Jehovah.
7 Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
Concerning the Edomites. Thus saith Jehovah of hosts: Is wisdom no more in Teman? Is counsel passed away from the prudent? Is their wisdom vanished?
8 Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
Flee ye, turn ye back, Dwell in deep places, O ye inhabitants of Dedan! For the destruction of Esau do I bring, The time of his punishment upon him.
9 Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
If grape-gatherers had come upon thee, Would they not have left some gleanings? If thieves by night, They would have destroyed only till they had enough.
10 Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
But I will make Esau bare; I will uncover his hiding-places, So that he shall not be able to hide himself. His offspring shall be destroyed, and his brethren, and his neighbors, And he shall be no more.
11 Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
Leave thy fatherless children, I will preserve them alive, And thy widows, let them trust in me!
12 Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
For thus saith Jehovah: Behold, they who ought not to have drunk the cup have deeply drunken, And shalt thou go altogether unpunished? Thou shalt not go unpunished; Thou shalt surely drink.
13 Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
For by myself have I sworn, saith Jehovah, That Bozrah shall become an astonishment, A reproach, a desolation, and a curse; And all her cities shall be perpetual wastes.
14 Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
I have heard a proclamation from Jehovah, And an ambassador hath been sent among the nations, [[Saying, ]] “Assemble yourselves, and come against her, And arise to battle!”
15 “Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
For, behold, I will make thee small among the nations, Despised among men.
16 Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
Thy terribleness hath deceived thee, The pride of thy heart, Because thou dwellest in the recesses of the rock, And holdest the height of the hill. Though thou set thy nest on high, like the eagle, From thence will I bring thee down, saith Jehovah.
17 Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
And Edom shall be an astonishment: Every one that passeth by her shall be astonished, And shall hiss on account of all her plagues.
18 Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
As in the overthrow of Sodom and Gomorrah, And their neighboring cities, saith Jehovah, There shall not a man abide there, Nor a son of man dwell within her.
19 Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
Behold, he [[the enemy]] cometh up like a lion from the pride of Jordan against the habitation of the rock; Suddenly will I drive him [[Edom]] thence, And him who is chosen by me will I set over her. For who is like me, Or who will summon me to trial? Or who is the shepherd that will stand up against me?
20 Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Therefore, hear ye the purpose of Jehovah, Which he hath formed against Edom, And the designs which he meditateth against the inhabitants of Teman! Surely he [[the enemy]] shall drag them forth like feeble sheep; Surely he shall come upon them, And make their pastures desolate.
21 Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
At the noise of their fall the earth trembleth, Even to the Red Sea is their cry heard.
22 Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
Behold, like an eagle, he [[the enemy]] cometh up, And spreadeth his wings over Bozrah; And the hearts of the heroes of Edom, in that day, Shall be as the heart of a woman in her pangs.
23 Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
Concerning Damascus. Hamath and Arpad are confounded; They faint, because they have heard evil tidings. There is anxiety at the sea; It cannot be at rest.
24 Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
Damascus is faint-hearted; She turneth herself to flee; Trembling hath seized on her; Anguish and pangs have taken hold of her, as of a woman in travail.
25 Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
“Why is not the praised city left, The city of my joy?”
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
Yea, her young men shall fall in her streets, And all her men of war shall be cut off in that day, Saith Jehovah of hosts.
27 “Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
Yea, I will kindle a fire in the wall of Damascus, Which shall consume the palaces of Benhadad.
28 Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
Concerning Kedar, and concerning the kingdoms of Hazor, which Nebuchadnezzar, king of Babylon, smote. Thus saith Jehovah: Arise ye, go up against Kedar, And spoil the sons of the East!
29 Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
Their tents and their flocks shall they take away; They shall take to themselves their curtains, and all their furniture, and their camels, And men shall cry to them, “Terror is on every side.”
30 Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
Flee, get you far off, dwell in deep places, O ye inhabitants of Hazor, saith Jehovah. For Nebuchadnezzar, the king of Babylon, meditates a design against you, And has formed a purpose against you.
31 Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
Arise ye, go up against a nation at ease, That dwelleth securely, saith Jehovah; Which hath neither gates nor bars; Which dwelleth alone.
32 Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
And their camels shall be a booty, And the multitude of their cattle a spoil; And I will scatter to all the winds them that shave the cheeks, And from every side will I bring their calamity, saith Jehovah.
33 Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
And Hazor shall be a dwelling for jackals, A desolation forever. There shall not a man abide there, Nor any son of man dwell therein.
34 Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
The word of Jehovah which came to Jeremiah the prophet against Elam, in the beginning of the reign of Zedekiah, king of Judah, saying: —
35 “Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
Thus saith Jehovah of hosts: Behold, I break the bow of Elam, The chief part of their strength.
36 Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
And I will bring against Elam The four winds from the four extremities of the heavens, And I will scatter them to all these winds, And there shall be no nation To which the outcasts of Elam shall not come.
37 Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
For I will cause Elam to be dismayed before their enemies, And before them that seek their life. And I will bring evil upon them, The fierceness of my anger, saith Jehovah. And I will send after them the sword, Until I have consumed them.
38 Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
And I will set up my throne in Elam, And I will destroy from thence king and princes, saith Jehovah.
39 na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”
But it shall come to pass in future times, That I will bring back the captivity of Elam, saith Jehovah.