< Yeremia 47 >

1 Hili ni neno la Yahwe lililokuja kwa Yeremia nabi juu ya Wafilisiti. Neno hili lilimjia kabla Farao hajaishambulia Gaza.
Слово Господне, еже бысть ко Иеремии пророку на иноплеменники, прежде нежели порази фараон Газу.
2 “Yahwe asema hivi: Tazama, mafuriko ya maji yanainuka huko kaskazini. Yatakuwa kama mto uliofurika! Kisha yataigharikisha nchi na kila kitu ndani yake, miji yake na watu wakaao ndani yake! Kila mtu atapiga kelele ya kuomba msaada, na wakaaji wote wa nchi wataomboleza.
Тако глаголет Господь: се, воды восходят от севера и будут яко поток наводняяй, и потопят землю и исполнение ея, град и живущыя в нем: и возопиют людие и восплачутся вси живущии на земли,
3 Kwa sauti ya kukanyaga kwa kwato za farasi wao wenye nguvu, kwa mwungurumo wa vibandawazi vyao na kelele za magurudumu yao, wazazi hawatawasaidia watoto wao kwa sababu ya udhaifu wao.
от шума устремления его, от оружия ног его и от гремения колесниц его и от звука колес его: не обратишася отцы ко сыном своим, опустивше руце свои,
4 Kwa maana siku inakuja itakayowaacha ukiwa Wafilisiti wote, kumwondoa kila mtu aliyesalia anayetaka kuwasaidia. Kwa maana Yahwe anawaangamiza Wafilisiti, waliosalia katika kisiwa cha Kaftori.
в день находящь, еже погубити вся иноплеменники: и разорю Тир и Сидон со всеми прочими помощники их, яко истребит Господь Филистины, останки островов Каппадокийских.
5 Maombolezo yatakuja juu ya Gaza. Hata kwa Ashikeloni, watu waliosalia bondeni watakuwa kimya. Ni kwa muda gani mtajiondoa katika maombolezo?
Прииде плешь на Газу, отвержен бысть Аскалон и останцы енакимли.
6 Ole, upanga wa Yahwe! itachukua muda gani hata unyamaze? Rudini alani mwenu! Acha na unyamaze.
Доколе сещи будеши, о, мечу Божий! Доколе не упокоишися? Вниди в ножны твоя, почий и вознесися.
7 Wawezaje kuwa kimya, maana Yahwe amekuagiza. Amekuamuru kumpiga Ashikeloni na dhidi ya nchi ya pwani ya bahari.
Како упокоится? Понеже Господь заповеда ему на Аскалона и на сущыя при мори, на прочыя востати.

< Yeremia 47 >