< Yeremia 42 >

1 Kisha amri wote wa jeshi na Yonathan mwana wa Karea, Jezania mwana wa Hoshaia, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa walimkaribia Yeremia nabii.
And they approached all [the] commanders of the armies and Johanan [the] son of Kareah and Jezaniah [the] son of Hoshaiah and all the people from [the] small and unto [the] great.
2 Walisema naye, “Acha maombi yetu yaje mbele yako. Omba kwa ajili yetu kwa Yahwe Mungu wako kwa ajili ya watu hawa ambao wanabaki kwani tuko wachache katika idadi, kama unavyoona.
And they said to Jeremiah the prophet may it fall please supplication our before you and pray for us to Yahweh God your for all the remnant this for we are left a few from many just as eyes your [are] seeing us.
3 Muulize Yahwe Mungu wako atuambia sisi njia yakuendea na nini tufanye.”
So he may declare to us Yahweh God your the way which we will go in it and the thing which we will do.
4 Basi Yeremia nabii alisema nao, “Nimewasikia, Tazama, Nitaomba kwa Yahwe Mungu wenu kama mlivyoomba. Vyovyote Yahwe ananijibu, Nitawambia. Sitawaficha chochote ninyi.”
And he said to them Jeremiah the prophet I have heard here I [am] about to pray to Yahweh God your according to words your and it will be every word which he will answer Yahweh you I will tell to you not I will withhold from you a word.
5 Walisema na Yeremia, “Na Yawhe awe shahidi mkweli na mwaminifu dhidi yenu, kama hatutafanya kila kitu ambacho Yahwe Mungu wenu anatuambia kufanya.
And they they said to Jeremiah may he become Yahweh on us a witness of truth and faithful if not according to every word which he will send you Yahweh God your to us so we will do.
6 Hata kama ni vizuri au vibaya, tutatii sauti ya Yahwe Mungu wetu, ambaye tunawatuma ninyi, ili kwamba iwe vizuri pamoja nasi wakati tunatii sauti ya Yahwe Mungu wetu.”
Whether good and or bad to [the] voice of - Yahweh God our whom (we *Q(K)*) [are] sending you to him we will listen so that this it may go well for us for we will listen to [the] voice of Yahweh God our.
7 Basi ilitokea kwamba baada ya siku kumi, neno la Yahwe lilikuja kwa Yeremia.
And it was from [the] end of ten days and it came [the] word of Yahweh to Jeremiah.
8 Kwa hiyo Yeremia alimwita Yonathan mwana wa Karea na amri wote jeshi pamoja naye, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa.
And he summoned Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies who [were] with him and all the people from [the] small and unto [the] great.
9 Na alisema nao, “Yahwe, Mungu wa Israel, ambaye umenituma mimi ili niweze kuweka maombi yako mbele zake. Yahwe asema hivi,
And he said to them thus he says Yahweh [the] God of Israel whom you sent me to him to make fall supplication your before him.
10 Kama mtarudi na kuishi katika nchi hii, basi nitawajenga na sitawararua chini; Nitapanda na sitawangoa, kwa kuwa nitageuza maafa ambayo nimeleta juu yako.
Certainly [if] you will remain in the land this and I will build up you and not I will tear [you] down and I will plant you and not I will pluck [you] up for I am grieved concerning the harm which I have done to you.
11 Msimugope mfalme wa Babeli, ambaye mnamuogopa. Msimuogope-hili ni tamko la Yahwe kwani niko pamoja nanyi kuwahifadhi na kuwaokoa toka mkono wake.
May not you be afraid of [the] king of Babylon whom you [are] afraid of him may not you be afraid from him [the] utterance of Yahweh that [am] with you I to save you and to deliver you from hand his.
12 Kwa kuwa nitawapa rehema. Nitakuwa na huruma juu yenu, na nitawarudisha kwenye nchi yenu.
So I may give to you compassion and he will have compassion on you and he will restore you to land your.
13 Lakini tudhani kusema kwamba, “Hatutakaa katika nchi hii”- kama hamtasikiliza sauti yangu, sauti ya Yahwe Mungu wenu.
And if [are] saying you not we will remain in the land this to not to listen to [the] voice of Yahweh God your.
14 Tudhani kwamba mnasema, “Hapana! Tutaenda kwenye nchi ya Misri, ambayo hatutaona vita yoyote, ambayo hatutasikia sauti ya tarumbeta, na hatutaona njaa ya chakula. Tutaishi huko.”
Saying In-deed [the] land of Egypt we will go where not we will see warfare and [the] sound of a trumpet not we will hear and for bread not we will be hungry and there we will dwell.
15 Sasa sikiliza neno hili la Yahwe, wewe mabaki ya Yuda. Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, 'Kama kweli mtatoka kwenda Misri, kwenda na kuishi huko,
And now therefore hear [the] word of Yahweh O remnant of Judah thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel if you really you will set! faces your to go Egypt and you will go to sojourn there.
16 basi upanga ambao mnauogopa utawapita huko kwenye nchi ya Misri. Njaa ambayo mnawasiwasi nayo itawafatilia huko Misri. Na mtakufa huko.
And it will be the sword which you [are] afraid from it there it will overtake you in [the] land of Egypt and the famine which you - [are] anxious from it there it will pursue closely behind you Egypt and there you will die.
17 Basi itatokea kwamba wanaume wote waliondoka kwenda Misri kuishi huko watakufa kwa upanga, njaa, au pigo. Hapatakuwa na mwathirika wao, hakuna atakayetoroka maafa ambayo nitaleta juu yao.
And they may be all the people who they have set faces their to go Egypt to sojourn there they will die by the sword by famine and by pestilence and not he will belong to them a survivor and an escapee from before the calamity which I [will] bring on them.
18 Kwa kuwa Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Kama gadhabu yangu na hasira yangu imemwanga juu ya wakazi wa Yerusalem, kwa njia hiyo hasira yangu itamwangwa juu yenu kama mtaenda Misri. Mtakuwa sababu ya hasira na hofu, sababu la kuzungumza laana, na kitu kisichokuwa na heshima. Na hamtaona eneo hili tena.”
For thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel just as it was poured out anger my and rage my on [the] inhabitants of Jerusalem so it will pour out rage my on you when go you Egypt and you will become an curse and a horror and a curse and a reproach and not you will see again the place this.
19 Basi Yeremia alisema, “Yahwe amezungumza kuhusu ninyi - mabaki ya Yuda. Msiende Misri! Unajua kwa hakika kwamba nimekuwa shahidi dhidi yenu leo.
He has spoken Yahweh to you O remnant of Judah may not you go Egypt assuredly you will know that I have warned you this day.
20 Kwa kuwa mmejidanganya vibaya wenyewe wakati mliponituma mimi kwenda kwa Yahwe Mungu wenu na kusema, 'Omba kwa Yahwe Mungu wetu kwa ajili yetu. Kila kitu ambacho Yahwe Mungu wetu asema, tuambie, na tutaibeba.'
For (you caused to err *Q(K)*) selves your for you you sent me to Yahweh God your saying pray for us to Yahweh God our and according to all that he will say Yahweh God our so tell to us and we will do [it].
21 Kwa kuwa nimekwisha toa taarifa kwako leo, lakini hajusikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu au kwa chochote kuhusu ambacho alinituma mimi kwako.
And I have told to you this day and not you have listened to [the] voice of Yahweh God your and to all that he sent me to you.
22 Basi sasa, utajua kwa hakika kwamba utakufa kwa upanga, njaa, na pigo katika eneo ambalo ulitamani kwenda kuishi.”
And therefore assuredly you will know that by the sword by famine and by pestilence you will die in the place where you desire to go to sojourn there.

< Yeremia 42 >