< Yeremia 42 >

1 Kisha amri wote wa jeshi na Yonathan mwana wa Karea, Jezania mwana wa Hoshaia, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa walimkaribia Yeremia nabii.
And all the captains of the forces, and Johanan, the son of Kareah, and Jezaniah, the son of Hoshaiah, and all the people, from the least even to the greatest, came near,
2 Walisema naye, “Acha maombi yetu yaje mbele yako. Omba kwa ajili yetu kwa Yahwe Mungu wako kwa ajili ya watu hawa ambao wanabaki kwani tuko wachache katika idadi, kama unavyoona.
and said to Jeremiah the prophet: “Let, we beseech thee, our supplication be accepted before thee, and pray for us to Jehovah, thy God, for all this remnant; (for we are left a few out of many, as thine eyes do behold us; )
3 Muulize Yahwe Mungu wako atuambia sisi njia yakuendea na nini tufanye.”
that Jehovah, thy God, may show us the way wherein we shall walk, and the thing which we shall do.”
4 Basi Yeremia nabii alisema nao, “Nimewasikia, Tazama, Nitaomba kwa Yahwe Mungu wenu kama mlivyoomba. Vyovyote Yahwe ananijibu, Nitawambia. Sitawaficha chochote ninyi.”
And Jeremiah the prophet said to them: “I have heard; behold, I will pray to Jehovah your God, according to your words, and all which Jehovah shall answer you I will declare to you; I will keep back nothing from you.”
5 Walisema na Yeremia, “Na Yawhe awe shahidi mkweli na mwaminifu dhidi yenu, kama hatutafanya kila kitu ambacho Yahwe Mungu wenu anatuambia kufanya.
Then they said to Jeremiah: “May Jehovah be our witness, a faithful and true witness! According to all for which Jehovah our God shall send thee to us, so will we do.
6 Hata kama ni vizuri au vibaya, tutatii sauti ya Yahwe Mungu wetu, ambaye tunawatuma ninyi, ili kwamba iwe vizuri pamoja nasi wakati tunatii sauti ya Yahwe Mungu wetu.”
Whether it be good, or whether it be evil, we will obey the voice of Jehovah our God, to whom we send thee, that it may be well with us when we shall have obeyed the voice of Jehovah our God.”
7 Basi ilitokea kwamba baada ya siku kumi, neno la Yahwe lilikuja kwa Yeremia.
And it came to pass after ten days, that the word of Jehovah came to Jeremiah.
8 Kwa hiyo Yeremia alimwita Yonathan mwana wa Karea na amri wote jeshi pamoja naye, na watu wote kutoka mdogo kwa mkubwa.
And he called Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces which were with him, and all the people, from the least even to the greatest,
9 Na alisema nao, “Yahwe, Mungu wa Israel, ambaye umenituma mimi ili niweze kuweka maombi yako mbele zake. Yahwe asema hivi,
and said to them: “Thus saith Jehovah, the God of Israel, to whom ye sent me to present your supplication before him:
10 Kama mtarudi na kuishi katika nchi hii, basi nitawajenga na sitawararua chini; Nitapanda na sitawangoa, kwa kuwa nitageuza maafa ambayo nimeleta juu yako.
If ye will still abide in this land, then will I build you, and not pull you down, and I will plant you, and not pluck you up; for I repent me of the evil which I have done to you.
11 Msimugope mfalme wa Babeli, ambaye mnamuogopa. Msimuogope-hili ni tamko la Yahwe kwani niko pamoja nanyi kuwahifadhi na kuwaokoa toka mkono wake.
Be not afraid of the king of Babylon, of whom ye are afraid; be not afraid of him, saith Jehovah; for I will be with you to save you, and to deliver you from his hand.
12 Kwa kuwa nitawapa rehema. Nitakuwa na huruma juu yenu, na nitawarudisha kwenye nchi yenu.
And I will show mercies to you, that he may have compassion upon you, and cause you to return to your own land.
13 Lakini tudhani kusema kwamba, “Hatutakaa katika nchi hii”- kama hamtasikiliza sauti yangu, sauti ya Yahwe Mungu wenu.
But if ye say, 'We will not dwell in this land,' so as not to hearken to the voice of Jehovah your God,
14 Tudhani kwamba mnasema, “Hapana! Tutaenda kwenye nchi ya Misri, ambayo hatutaona vita yoyote, ambayo hatutasikia sauti ya tarumbeta, na hatutaona njaa ya chakula. Tutaishi huko.”
saying, 'No! but we will go into the land of Egypt, where we shall see no war, nor hear the sound of the trumpet, nor be hungry for bread, and there will we dwell, —
15 Sasa sikiliza neno hili la Yahwe, wewe mabaki ya Yuda. Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, 'Kama kweli mtatoka kwenda Misri, kwenda na kuishi huko,
now, therefore, hear the word of Jehovah, ye remnant of Judah! Thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: If ye set your faces to enter into Egypt, and go to sojourn there,
16 basi upanga ambao mnauogopa utawapita huko kwenye nchi ya Misri. Njaa ambayo mnawasiwasi nayo itawafatilia huko Misri. Na mtakufa huko.
then it shall come to pass that the sword, which ye feared, shall overtake you there in the land of Egypt, and the famine, of which ye were afraid, shall follow close after you into Egypt, and there shall ye die.
17 Basi itatokea kwamba wanaume wote waliondoka kwenda Misri kuishi huko watakufa kwa upanga, njaa, au pigo. Hapatakuwa na mwathirika wao, hakuna atakayetoroka maafa ambayo nitaleta juu yao.
So shall it be with all the men that set their faces to go into Egypt to sojourn there. They shall die by the sword, and by famine, and by pestilence, and not one of them shall remain, or escape from the evil which I bring upon them.
18 Kwa kuwa Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Kama gadhabu yangu na hasira yangu imemwanga juu ya wakazi wa Yerusalem, kwa njia hiyo hasira yangu itamwangwa juu yenu kama mtaenda Misri. Mtakuwa sababu ya hasira na hofu, sababu la kuzungumza laana, na kitu kisichokuwa na heshima. Na hamtaona eneo hili tena.”
For thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: As my anger and my wrath have been poured forth upon the inhabitants of Jerusalem, so shall my wrath be poured forth upon you, when ye shall enter into Egypt; and ye shall be an execration, and an astonishment, and a curse, and a reproach; and ye shall see this place no more.
19 Basi Yeremia alisema, “Yahwe amezungumza kuhusu ninyi - mabaki ya Yuda. Msiende Misri! Unajua kwa hakika kwamba nimekuwa shahidi dhidi yenu leo.
This is the word of Jehovah to you, ye remnant of Judah! Go ye not into Egypt; ye shall surely know that I have warned you this day.
20 Kwa kuwa mmejidanganya vibaya wenyewe wakati mliponituma mimi kwenda kwa Yahwe Mungu wenu na kusema, 'Omba kwa Yahwe Mungu wetu kwa ajili yetu. Kila kitu ambacho Yahwe Mungu wetu asema, tuambie, na tutaibeba.'
Ye err to your own ruin; for ye sent me to Jehovah your God, saying, 'Pray for us to Jehovah our God, and according to all that Jehovah our God shall say, so declare to us, and we will do it';
21 Kwa kuwa nimekwisha toa taarifa kwako leo, lakini hajusikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu au kwa chochote kuhusu ambacho alinituma mimi kwako.
and now I have this day declared it to you, but ye have not hearkened to the voice of Jehovah your God, nor to anything for which he sent me to you.
22 Basi sasa, utajua kwa hakika kwamba utakufa kwa upanga, njaa, na pigo katika eneo ambalo ulitamani kwenda kuishi.”
Now, therefore, ye shall know assuredly, that by the sword, by famine, and by pestilence ye shall die, in the place whither ye have chosen to go and to sojourn.”

< Yeremia 42 >