< Yeremia 39 >
1 Katika mwaka wa tisa na mwezi wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote dhidi ya Yerusalem na kuizingira.
La neuvième année de Sédécias, roi de Juda, au dixième mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint et toute son armée devant Jérusalem, et ils en faisaient le siège.
2 Katika mwaka wa kumi na moja na mwezi wa nne wa Sekeia, siku ya tisa ya mwezi, mji uliharibiwa.
Mais la onzième année de Sédécias, au quatrième mois, le cinquième jour, la cité fut ouverte.
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli walikuja na kukaa kwenye lango la katikati: Nergali Sharezeri, Samgari Nebo, na Sarsechimu, afisa muhimu. Nerga Sharezeri alikuwa afisa mkuu na wote waliobaki maafisa wa mfalme wa Babeli.
Et tous les princes du roi de Babylone entrèrent, et se postèrent à la porte du milieu: Nérégel, Séréser, Sémégarnabu, Sarsachim, Rabsarès, Nérégel, Séréser, Rebmag, et tous les autres princes du roi de Babylone.
4 Ilitokea kwamba wakati Sedekia, mfalme wa Yuda, na wanaume wapiganaji wake wote walipowaona, walikimbia. Walitoka nje usiku toka kwenye mji kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango la kati la kuta mbili. Mfalme alitoka nje katika mwelekeo wa Arabah.
Et lorsque Sédécias, roi de Juda, et tous les hommes de guerre les eurent aperçus, ils s’enfuirent; et ils sortirent la nuit de la cité par la voie du jardin du roi, et par la porte qui était entre les deux murs, et ils se dirigèrent vers la voie du désert.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo walimfatilia na kumpata Sedekia kwenye tambarare za mto Yordani karibu na Yeriko. Kisha walimshika na kumleta kwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Riblah kwenye nchi ya Hamath, ambapo Nebukadreza alipitisha sentensi juu yake.
Mais l’armée des Chaldéens les poursuivit; et ils prirent Sédécias dans les champs de la solitude de Jéricho, et ils l’amenèrent prisonnier à Nabuchodonosor, roi de Babylone, à Réblatha qui est en la terre d’Emath; et Nabuchodonosor lui prononça son arrêt.
6 Mfalme wa Babeli alimchinja binti wa Sedekia mbele ya macho yake huko Ribla. Pia aliwachinja wanaume wote wa heshima wa Yuda.
Et le roi de Babylone fit mourir les deux fils de Sédécias à Réblatha, sous ses yeux, et tous les nobles de Juda, le roi de Babylone les fit mourir.
7 Kisha alingoa macho ya Sedekia na kumfunga mnyororo wa shaba ili kusudi kumpeleka Babeli.
Il arracha aussi les yeux à Sédécias, et le chargea de fers aux pieds, afin qu’il fût emmené à Babylone.
8 Kisha Wakaldayo walichoma nyumba ya mfalme na nyumba za watu. Pia walivunja kuta za Yerusalem.
Les Chaldéens mirent aussi le feu à la maison du roi et aux maisons du peuple, et ils renversèrent le mur de Jérusalem.
9 Nebukadreza, nahodha wa walinzi wa mfalme, waliwachukua katika mateka watu wengine waliobaki katika mji. Hii ilijumuisha watu waliotoka jangwa kwenda Wakaldayo na watu wengine walioachwa katika mji.
Et les restes du peuple qui étaient demeurés dans Jérusalem, et les transfuges qui s’étaient réfugiés auprès de lui, et les restants du peuple qui étaient demeurés, Nabuzardan, chef de la milice, les transféra à Babylone.
10 Lakini Nebukadreza nahodha wa walinzi wa mfalme aliwaruhusu watu maskini ambayo hawakuwa na chochote wao kubaki katika chi ya Yuda. Aliwapa mashamba ya mizabibu na maeneo katika siku ile.
Et quant à la foule des pauvres qui ne possédaient absolument rien, Nabuzardan, chef de la milice, la laissa dans la terre de Juda et lui donna des vignes et des citernes en ce jour-là.
11 Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa amri kuhusu Yeremia kwa Nebuzaradani nahodha wa walinzi wa mfalme. Alikuwa amesema,
Mais Nabuchodonosor, roi de Babylone, avait donné à Nabuzardan, chef de la milice, cet ordre touchant Jérémie, disant:
12 “Mchukue na umjali. Usimdhuru. Fanya kwa ajili yake chochote anachokuambia.”
Prends-le et tiens sur lui tes yeux, et ne lui fais aucun mal: mais comme il voudra, ainsi tu lui feras.
13 Basi Nebuzaradani nahodha wa walinzi wa mfalme, Nebushazbani mkuu wa matoashi, Nergali Sharezeri afisa mkuu, na wote maafisa wa muhimu wa mfalme wa Babeli walituma watu nje.
Nabuzardan donc, chef de la milice, envoya, et Nabusezban, et Rabsarès, et Nérégel, et Séréser, et Rebmag, et tous les autres grands du roi de Babylone,
14 Watu wao walimchukua Yeremia kutoka uwanja wa mlinzi na kumkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikami mwana wa Shafani, kumchua nyumbani, basi Yeremia alibaki miongoni mwa watu.
Envoyèrent et firent sortir Jérémie du vestibule de la prison, et ils le remirent à Godolias, fils d’Ahicam, fils de Saphan, afin qu’il entrât dans une maison et qu’il habitât au milieu du peuple.
15 Sasa neno la Yahwe lilikuwa limekuja kwa Yeremia wakati alipokuwa chini ya kifungo kwenye uwanja wa mlinzi, na alisema,
Mais à Jérémie avait été adressée la parole du Seigneur, lorsqu’il était enfermé dans le vestibule de la prison, disant:
16 “Zungumza kwa Ebedi Meleki Mkushi na sema, 'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Ona, Nimekaribia kubeba maneno yangu dhidi ya mji huu kwa ajili ya janga na si kwa uzuri. Kwa kuwa yatakuwa kweli mbele yako katika siku hiyo.
Va, et parle à Abdémélech l’Ethiopien, disant: Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Voilà que j’amènerai mes paroles sur cette cité, pour son mal, et non pour son bien: elles auront lieu en ce jour-là devant tes yeux.
17 Lakini nitakuokoa katika siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe - na hautatiwa katika mkono wa wanaume ambayo unawaogopa.
Et je te délivrerai, en ce jour-là, dit le Seigneur; et tu ne seras pas livré aux mains des hommes que tu redoutes;
18 Kwa kuwa nitakuokoa hakika. Hautaanguka kwa upanga. Utatoroka pamoja na maisha yako, kwani unanitumaini - hili lilikuwa tamko la Yahwe.”
Mais, t’en retirant, je te délivrerai, et tu ne tomberas pas sous le glaive; mais ta vie te sera sauvée, parce que tu as eu confiance en moi, dit le Seigneur.