< Yeremia 37 >

1 Sasa Sedekia mwana wa Yosia alitawala kama mfalme badala ya Yehoyachin mwana wa Yehoyakimu. Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuwa amemfanya Sedekia mfalme juu ya nchi ya Yuda.
Now Zedekiah son of Josiah reigned as king instead of Jehoiachin son of Jehoiakim. Nebuchadnezzar king of Babylon had made Zedekiah king over the land of Judah.
2 Lakini Sedekia, wajakazi wake, na watu wa nchi hawakusikiliza maneno ya Yahwe ambayo alitangaza kwa mkono wa Yeremia nabii.
But Zedekiah, his servants, and the people of the land did not listen to the words of Yahweh that he proclaimed by the hand of Jeremiah the prophet.
3 Kwa hiyo Mfalme Sedekia, Yehukali mwana wa Shelemia, na Zefania mwana wa Maaseia kuhani alituma ujumbe kwa Yeremia nabii. Walisema, “Omba kwa niaba kwa Yahwe Mungu wetu.”
So King Zedekiah, Jehukal son of Shelemiah, and Zephaniah son of Maaseiah the priest sent a message to Jeremiah the prophet. They said, “Pray on our behalf to Yahweh our God.”
4 Sasa Yeremia alikuwa anakuja na kwenda miongoni mwa watu, kwa kuwa alikuwa bado hajawekwa ndani ya gereza.
Now Jeremiah was coming and going among the people, for he had not yet been put in prison.
5 Jeshi la Farao lilitoka Misri, na Wakaldayo waliozingira Yerusalem walisikia habari kuhusu wao na kuondoka Yerusalem.
Pharaoh's army came out from Egypt, and the Chaldeans who were besieging Jerusalem heard the news about them and left Jerusalem.
6 Kisha neno la Yahwe lilikuja kwa Yeremia nabii na kusema,
Then the word of Yahweh came to Jeremiah the prophet, saying,
7 “Yahwe, Mungu wa Israel, asema hivi: Hiki ndivyo utakavyosema kwa mfalme wa Yuda, kwa sababu amekutuma wewe kutafuta ushauri toka kwangu, 'Ona, jeshi la Farao, ambalo lilikuja kukusaidia, liko tayari kurudi Misri, kwenye nchi yao.
“Yahweh, God of Israel, says this: This is what you will say to the king of Judah, because he has sent you to seek advice from me, 'See, Pharaoh's army, which came to help you, is about to go back to Egypt, its own land.
8 Wakaldayo watarudi. Watapigana dhidi ya mji huu, kuuteka, na kuuchoma.'
The Chaldeans will return. They will fight against this city, capture it, and burn it.'
9 Yahwe asema hivi: Msidaganyane kwa kusema, “Hakika Wakaldayo wanatuacha sisi,' kwa kuwa hawatatuacha.
Yahweh says this: Do not deceive yourselves by saying, 'Surely the Chaldeans are leaving us,' for they will not leave.
10 Hata kama mmelishinda jeshi la Wakaldayo lote ambalo linapigana nanyi ili kwamba wanaume waliojeruhiwa walibakizwa katika mahema yao, wangeweza kunyanyuka na kuchoma mji huu.”
Even if you had defeated the entire Chaldean army that is fighting you so that only wounded men were left in their tents, they would get up and burn this city.”
11 Basi ilikuwa wakati jeshi la Wakaldayo lilipoondoka Yerusalem wakati jeshi la Farao lilikuwa linakuja,
So it was when the Chaldean army had left Jerusalem as Pharaoh's army was coming,
12 kisha Yeremia alienda toka Yerusalem kwenda nchi ya Benjamini. Alitaka kumiliki njia ya nchi huko miongoni mwa watu wake.
then Jeremiah went out from Jerusalem to go to the land of Benjamin. He wanted to take possession of a tract of land there among his people.
13 Kama alivyokuwa katika mlango wa Benjamini, mlinzi mkuu aliyekuwa hapo. Jina lake lilikuwa Yeria mwana wa Shelemia mwana wa Hanania. Alimshika kwa kumnyakua Yeremia nabii na kusema, “Mnatoka jangwani kwa Wakaldayo.”
As he was in the Benjamin Gate, a chief guard was there. His name was Irijah son of Shelemiah son of Hananiah. He grabbed hold of Jeremiah the prophet and said, “You are deserting to the Chaldeans.”
14 Lakini Yeremia alisema, “Hiyo si kweli. Siendi jangwani kwa Wakaldayo.” Lakini Yeria hakumsikiliza. Alimchukua Yeremia na kumleta kwa maafisa.
But Jeremiah said, “That is not true. I am not deserting to the Chaldeans.” But Irijah did not listen to him. He took Jeremiah and brought him to the officials.
15 Maafisa walikuwa wamemkasirikia Yeremia. Walimpiga na kumweka gerezani, ambayo ilikuwa nyumba ya Yonathani mwandishi, kwa kuwa waligeuza kuwa gereza.
The officials were angry with Jeremiah. They beat him and put him in prison, which had been the house of Jonathan the scribe, for they had turned it into a prison.
16 Kwa hiyo Yeremia alikuwa amewekwa kwenye kifungo cha chini, ambako alikuwa huko kwa siku nyingi.
So Jeremiah was put into an underground cell, where he stayed for many days.
17 Kisha mfalme Sedekia alimtuma mtu mmoja aliyemleta kwenye ikulu. Kwenye nyumba yake, mfalme alimuuliza binafsi, “Kuna neno: Utatiwa kwenye mkono wa mfalme wa Babeli.”
Then King Zedekiah sent someone who brought him to the palace. In his house, the king asked him privately, “Is there any word from Yahweh?” Jeremiah answered, “There is a word: You will be given into the hand of the king of Babylon.”
18 Kisha Yeremia alisema kwa mfalme Sedekia, “Kwa namna gani nimekutenda dhambi, mjakazi wako, au watu hawa kwamba umeniweke mimi kwenye gereza?
Then Jeremiah said to King Zedekiah, “How have I sinned against you, your servants, or this people so that you have placed me in prison?
19 Wako wapi nabii wako, wale waliotabiri kwa ajili yako na kusema mfalme wa Babeli hatakuja dhidi yako au dhidi ya nchi hii?
Where are your prophets, the ones who prophesied for you and said the king of Babylon will not come against you or against this land?
20 Lakini sasa sikiliza, bwana wangu mfalme! Acha ombi langu liwe mbele yako. Usinirudie mimi kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, au nitakufa huko.”
But now listen, my master the king! Let my pleas come before you. Do not return me to the house of Jonathan the scribe, or I will die there.”
21 Kwa hiyo mfalme Sedekia alitoa amri. Wajakazi wake walimwekea mipaka Yeremia katika uwanja wa walinzi. Alipewa mkate kila siku kutoka mtaa wa waokaji mkate, mpaka mkate wote mjini uliisha. Basi Yeremia alibaki kwenye uwanja walinzi.
So King Zedekiah gave an order. His servants confined Jeremiah in the courtyard of the guard. A loaf of bread was given him every day from the street of the bakers, until all the bread in the city was gone. So Jeremiah stayed in the courtyard of the guard.

< Yeremia 37 >