< Yeremia 36 >

1 Ilikuja tokea katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosiah mfalme wa Yuda, kwamba neno hili lilikuja kwa Yeremiah kutoka kwa Yahwe, na alisema,
And it came to pass in the fourth year of Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah, that this word came to Jeremiah from Jehovah, saying:
2 “Chukua kitabu kwa ajili yako na uandike juu yake maneno yote ambayo nimekwisha kukuambia kuhusiana na Israel na Yuda, na kila taifa. Fanya hivi kwa kila kitu nilichokuambia tokea siku za Yosia mpaka siku ile.
Take thee a book-roll, and write upon it all the words which I have spoken to thee concerning Israel, and concerning Judah, and concerning all the nations, from the day when I began to speak to thee even to this day.
3 Huenda watu wa Yuda watasikiliza majanga yote ambayo ninakusudia kuleta juu yao. Huenda kila mmoja ataacha njia zake mbaya, ili kwamba niweze kuwasamehe maovu yao na dhambi zao.”
It may be that the house of Judah will hear all the evil which I purpose to do to them, and return every one from his evil way, so that I may forgive their iniquity and their sin.
4 Kisha Yeremia alimwita Baruku mwana wa Neria, na Baruku aliandika kwenye kitabu, kwa imla ya Yeremia, maneno yote ya Yahwe yalizunguzwa kwake.
Then Jeremiah called Baruch, the son of Neriah; and Baruch wrote from the mouth of Jeremiah all the words of Jehovah which he had spoken to him, upon a book-roll.
5 Kisha Yeremia alitoa amri kwa Baruku. Alisema, “Niko gerezani na siwezi kwenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And Jeremiah commanded Baruch and said: I am shut up; I cannot go into the house of Jehovah;
6 Kwa hiyo unapaswa uende na kusoma kutoka kwenye kitabu ulichoandika kwa imla yangu. Kwa siku ya kufunga, unapaswa usome maneno ya Yahwe kwenye masikio ya watu katika nyumba yake, na pia kwenye masikio ya Yuda yote waliokuja kutoka katika miji yao. Tangaza maneno haya kwao.
therefore, go thou, and read in the roll which thou hast written from my mouth the words of Jehovah, in the ears of the people, in the house of Jehovah, upon the fast-day; also in the ears of all Judah, that come out of their cities, shalt thou read them.
7 Huenda maombi yao ya rehema yatakuja mbele ya Yahwe. Huenda kila mtu ataacha njia mbaya, kwani gathabu na hasira ya Yahwe imetangazwa dhidi ya watu kwa ukali.”
It may be that they will prostrate themselves in supplication before Jehovah, and will return every one from his evil way. For great is the anger and the indignation which Jehovah hath denounced against this people.
8 Kwa hiyo Baruku mwana wa Neria alifanya kila kitu ambacho Yeremia nabii alimwamuru yeye kufanya. Alisoma kwa sauti maneno ya Yahwe ndani mwa nyumba ya Yahwe.
And Baruch, the son of Neriah, did according to all that Jeremiah the prophet commanded him, reading in the book the words of Jehovah in the house of Jehovah.
9 Ilikuja tokea katika mwaka wa tano na mwezi wa tisa kwa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, kwamba watu wote Yerusalemu na watu waliotoka Yerusalemu toka miji ya Yuda walitangaza kufunga kwa kumheshimu Yahwe.
And it came to pass in the fifth year of Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah, in the ninth month, that all the people in Jerusalem, and all the people that came out of the cities of Judah, proclaimed a fast before Jehovah, in Jerusalem.
10 Baruku alisoma kwa sauti maneno ya Yeremia katika nyumba ya Yahwe, kutoka kwenye chumba cha Gamaria mwana wa Shafani mwandishi, katika ua wa juu, kwa mlango wa kuingilia wa nyumba ya Yahwe. Alifanya hivi kwa masikio ya watu wote.
Then read Baruch in the book the words of Jeremiah in the house of Jehovah, in the chamber of Gemariah, the son of Shaphan the scribe, in the higher court, at the entrance of the new gate of the house of Jehovah, in the ears of all the people.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria alisikia maneno yote ya Yahwe kwenye kitabu.
And when Micah, the son of Gemariah, the son of Shaphan, had heard from the book all the words of Jehovah,
12 Alienda chini kwenye nyumba ya mfalme, kwenye chumba cha katibu. Tazama, maafisa wote walikuwa wamekaa hapo: Elishama mwandishi, Delaiah mwana wa Shemaiah, Elnathan mwana wa Achbor, Gemaria mwana wa Shefani, na Sedekia mwana wa Hananiah, na maafisa wote.
he went down to the king's house, into the scribe's chamber; and lo, all the princes were sitting there, Elishama the scribe, and Delaiah, the son of Shemaiah, and Elnathan, the son of Achbor, and Gemariah, the son of Shaphan, and Zedekiah, the son of Hananiah, and all the princes.
13 Kisha Mikaya alitoa taarifa ya maneno yote kwao ambayo alikuwa amesikia ambayo Baruku alisoma kwa sauti kwenye masikio ya watu.
Then Micah declared to them all the words which he had heard when Baruch read the book in the ears of the people.
14 Kwa hiyo maafisa wote walimtuma Jehudi mwana wa Nethania mwana wa Shelemiah mwana wa Kushi, kwa Baruku. Jehudi alisema kwa Baruku, “Chukua kitabu katika mkono wako, kitabu ambacho ulikuwa unakisoma kwa masikio ya watu and kuja.” Kwa hiyo Baruku mwana wa Neria alichukua kitabu katika mkono wake na alienda kwa maafisa.
Then all the princes sent Jehudi, the son of Nethaniah, the son of Shelemiah, the son of Cushi, to Baruch, and said, “Take in thy hand the roll wherein thou hast read in the ears of the people, and come.” So Baruch, the son of Neriah, took the roll in his hand, and came to them.
15 Kisha walisema naye,”Kaa chini na usome haya katika masikio yetu.” Kwa hiyo Baruku akasoma kitabu.
And they said to him, “Sit down now, and read it in our ears.” And Baruch read it in their ears.
16 Ilitokea wakati waliposikia haya maneno yote, kila mtu alipatwa na hofu kwa mtu aliye karibu naye na kusema kwa Baruku, “Kwa hakika tunapaswa kutoa taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
And when they had heard all the words, they looked with consternation upon one another, and they said to Baruch, “We must tell the king of all these things.”
17 Kisha walimuuliza Baruku, “Tuambie, ulipataje kuandika maneno yote haya kwa imla ya Yeremia?”
And they asked Baruch, saying, “Tell us now, how didst thou write all these words from his mouth?”
18 Baruku aliwaambia, “Alitoa imla ya maneno haya yote kwangu, na nikayaandika kwa wino kwenye kitabu hiki.”
And Baruch said to them, “With his mouth he pronounced to me all these words, and I wrote them on the book with ink.”
19 Kisha maafisa walisema kwa Baruku, “Nenda, jifiche mwenyewe, na Yeremiah, pia. Usipatikane mtu yeyote kujua uko wapi.”
Then said the princes to Baruch, “Go, hide thee, thou and Jeremiah, and let no man know where ye are.”
20 Kisha walienda kwa uwanja wa mfalme na wakatoa taarifa ya maneno haya kwake. Lakini kwanza walikihifadhi kitabu kwenye chumba cha katibu Elishama.
And they went in to the king into the court; but they laid up the roll in the chamber of Elishama the scribe, and they told all these things in the ears of the king.
21 Basi mfalme alimtuma Yehudi kuchukua kitabu. Yehudi alikichukua toka chumba cha Elishama katibu. Kisha alikisoma kwa sauti kwa mfalme na wote maafisa walikuwa wamesimama karibu naye.
Then the king sent Jehudi to fetch the roll, and he took it out of the chamber of Elishama the scribe; and Jehudi read it in the ears of the king, and in the ears of all the princes who stood beside the king.
22 Sasa mfalme alikuwa amesimama kwenye nyumba ya majira ya baridi katika mwezi wa tisa, na mkaa ulikuwa unawaka mbele yake.
And the king was sitting in the winter-house, in the ninth month, and a brasier was burning before him.
23 Ilitokea wakati Yehudi aliposoma kurusa tatu au nne, mfalme angeweza kuikata kwa kisu na kuitupa kwenye moto katika mkaa mpaka kitabu chote kiliteketea.
And when Jehudi had read three or four sections, he [[the king]] cut it with the penknife, and cast it into the fire, into the brasier, until the whole roll was consumed in the fire in the brasier.
24 Lakini wala mfalme wala yeyote wa mjakazi wake aliyesikia haya maneno yote aliogopa, wala hawakuchana nguo zao.
And they were not afraid, and rent not their garments, neither the king, nor any of his servants, who heard all these words;
25 Elnathani, Delaya, na Gemaria walikuwa wamemuomba mfalme asikichome kitabu, lakini hakuwasikiliza.
and although Elnathan and Delaiah and Gemariah interceded with the king not to burn the roll, yet he would not hearken to them.
26 Basi mfalme alimwamuru Yerameeli, ndugu, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kumfunga Baruku mwandishi na Yeremia nabii, lakini Yahwe alikuwa amewaficha.
And the king commanded Jerahmeel, the son of Hammelech, and Seraiah, the son of Azreel, and Shelemiah, the son of Abdeel, to seize Baruch the scribe, and Jeremiah the prophet; but Jehovah had hid them.
27 Kisha neno la Yahwe lilikuja kwa Yeremia baada ya mfalme kuwa amechoma kitabu na maneno ya Baruku yaliyokuwa yameandikwa kwa imla ya Yeremia, na alisema,
Then came the word of Jehovah to Jeremiah, after that the king had burned the roll, and the words which Baruch had written from the mouth of Jeremiah, saying:
28 “Rudi, chukua kitabu kingine kwa ajili yako, na uandike maneno haya yote ambayo yalikuwa kwenye kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikichoma.
Take thee another roll, and write in it all the former words that were in the first roll, which Jehoiakim, king of Judah, hath burned.
29 Kisha unapaswa kusema hivi kwa mfalme Yehoyakimu mfalme wa Yuda: 'Ulichoma hicho kitabu! Na ulisema: Kwanini umeandika juu yake, “Mfalme wa Babeli hakika atakuja na kuharibu nchi hii, kwa kuwa atawaangamiza wanaume wote na wanyama ndani yake?”
And concerning Jehoiakim, king of Judah, thou shalt say, Thou hast burned this roll, saying, “Why hast thou written therein and said, The king of Babylon shall surely come and shall destroy this land, and shall cause to cease from it man and beast?”
30 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi kuhusu wewe, Yehoyakimu mfalme wa Yuda: “Hakuna mzao wako atawahi kukaa kwenye kiti cha Daudi. Kama wewe, maiti yako itatupwa kwenye siku ya joto na usiku wa baridi.
Therefore thus saith Jehovah concerning Jehoiakim, king of Judah: He shall have not one to sit upon the throne of David; and his dead body shall be cast out in the day to the heat, and in the night to the frost.
31 Kwa kuwa nitakuadhibu, wazao wako, na wajakazi wako kwa maovu yenu yote. Nitaleta kwenu, kwa wakazi wote wa Yerusalemu, na kwa kila mtu Yuda majanga ambayo nimewatishia ninyi, lakini kwa hamkuwa makini.”
And I will punish him, and his offspring, and his servants, for their iniquity; and I will bring upon them, and upon the inhabitants of Jerusalem, and upon the men of Judah, all the evil which I have pronounced against them, and they have not hearkened.
32 Kwa hiyo Yeremia alichukua kitabu kingine na akampa Baruku mwana wa Neria mwandishi. Baruku aliandika juu yake kwa imla ya Yeremia maneno yote ambayo yalikuwa katika kitabu kilichochomwa moto na mfalme Yehoyakimu mfalme wa Yuda. Zaidi, maneno mengi ya kufanana yaliongezwa kwenye kitabu hiki.
Then Jeremiah took another roll, and gave it to Baruch the scribe, the son of Neriah, who wrote therein from the mouth of Jeremiah all the words of the book which Jehoiakim had burned in the fire; and there were added to them many words of the same kind.

< Yeremia 36 >