< Yeremia 34 >
1 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yahwe, wakati Nebukadreza mfalme wa Babeli, majeshi yake yote, pamoja na falme zote za dunia, maeneo yote yaliyo chini ya mamlaka yake, na watu wake wote walikuwa wanapigana vita dhidi ya Yerusalemu na miji yake yote, kusema:
La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahvé, lorsque Nebucadnetsar, roi de Babylone, avec toute son armée, tous les royaumes de la terre qui étaient sous sa domination, et tous les peuples, combattaient contre Jérusalem et contre toutes ses villes, en disant:
2 'Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nenda na uzungumze kwa Sedekia mfalme wa Yuda na useme kwake, 'Yahwe asema hivi: Angalia, niko karibu kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli. Atauchoma moto.
Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: « Va, parle à Sédécias, roi de Juda, et dis-lui: Yahvé dit: « Voici, je livre cette ville entre les mains du roi de Babylone et il la brûlera par le feu.
3 Hautapona kutoka mkono wake, kwa maana kwa hakika utakamatwa na kutiwa mkononi mwake. Macho yako yatayaangalia macho ya mfalme wa Babeli; atazungumza kwako moja kwa moja ukiwa unaenda Babeli.'
Tu n'échapperas pas à sa main, mais tu seras certainement pris et livré entre ses mains. Tes yeux verront les yeux du roi de Babylone, et il te parlera bouche à bouche. Tu iras à Babylone. »'
4 Sedekia mfalme wa Yuda, sikiliza neno la Yahwe! Yahwe anasema hivi kuhusu wewe, 'Hautakufa kwa upanga.
« Mais écoute la parole de Yahvé, Sédécias, roi de Juda. Yahvé dit à ton sujet: 'Tu ne mourras pas par l'épée'.
5 Utakufa katika amani. Kama kwenye mafukizo ya babu zako, wafalme waliokuwepo kabla yako, watauchoma mwili wako. Watasema, 'Ole, bwana!” Watakuomboleza. Sasa nimesema—hili ni tangazo la Yahwe.”
Tu mourras dans la paix; et avec les brûlures de tes pères, les anciens rois qui t'ont précédé, ils feront une brûlure pour toi. Ils te pleureront en disant: « Ah Seigneur! » car j'ai dit la parole, dit Yahvé. »
6 Kwa hiyo Yeremia nabii akatangaza kwa Sedekia mfalme wa Yuda maneno haya yote katika Yerusalemu.
Jérémie, le prophète, adressa toutes ces paroles à Sédécias, roi de Juda, à Jérusalem,
7 Jeshi la mfalme wa Babeli likafanya dhidi ya Yerusalemu na miji yote ya Yuda iliyobaki: Lakishi, na Azeka. Miji hii ya yuda ilisalia kama miji yenye maboma.
au moment où l'armée du roi de Babylone combattait contre Jérusalem et contre toutes les villes de Juda qui restaient, contre Lakis et contre Azéka, car ce sont les seules villes de Juda qui restaient comme villes fortes.
8 Neno lilomjia Yeremia kutoka kwa Yahwe baada ya mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote katika Yurusalemu, ili kuwatanagazia uhuru
La parole fut adressée à Jérémie de la part de Yahvé, après que le roi Sédécias eut fait alliance avec tout le peuple qui était à Jérusalem, pour lui annoncer la liberté,
9 ya kwamba kila mtu lazima amwachie huru mtumwa wake wa Kiebrania, wote wa kiume na wa kike, kwa hiyo mtu alipaswa kutomtumikisha Myahudi, ambaye alikuwa ndugu yake.
que chacun laisserait aller en liberté son serviteur et sa servante, hébreu ou hébreu, afin que personne ne les asservisse plus, d'un Juif à son frère.
10 Kwa hiyo watu wote na viongozi wakaingia katika agano kwamba kila mtu amwachie huru mtumwa wake wa kiume na waikke ili asiwe mtumwa tena. Walitii na kuwaweka huru.
Tous les princes et tout le peuple obéirent à ceux qui avaient conclu l'alliance, pour que chacun libère son serviteur et chacune de ses servantes, et que personne ne les asservisse plus. Ils obéirent et les laissèrent aller,
11 Lakini baada ya hapo walibadili akili zao. Wakawarudisha watumwa ambao walikuwa wamewaachia huru. Wakawalazimisha kuwa wataumwa tena.
mais ensuite ils se retournèrent, firent revenir les serviteurs et les servantes qu'ils avaient laissés aller en liberté, et les soumirent comme serviteurs et comme servantes.
12 Kwa hiyo neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,
La parole de Yahvé fut adressée à Jérémie de la part de Yahvé, en ces termes:
13 “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi, 'Mimi mwenyewe nilifanya agano na babu zenu katika siku ambayo niliwatoa nje ya nchi ya Misiri, nje ya nyumba ya utumwa. Hapo ndipo niliposema,
« Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: 'J'ai fait une alliance avec vos pères, le jour où je les ai fait sortir du pays d'Égypte, de la maison de servitude, en disant:
14 Katika mwisho wa mwaka wa saba, kila mtu lazima amwachie ndugu yake, Mwebrania mwenzake aliyejiuza mwenyewe kwako ili kukutumikia kwa miaka sita. Mwagize aende kwa uhuru.” Lakini babu zenu hawakunisikiliza wala kutega masikio yao kwangu.
Au bout de sept ans, chacun de vous relâchera son frère hébreu qui vous a été vendu et qui vous a servi pendant six ans. Tu le laisseras partir libre de chez toi. Mais vos pères ne m'ont pas écouté, et n'ont pas prêté l'oreille.
15 Sasa ninyi wenyewe mlitubu na kuanza yaliyomema katika macho yangu. Mlitangaza uhuru, kila mtu kwa jirani yake, na mlifanya agano mbele zangu kwenye nyumba iitwayo kwa jina langu.
Vous vous étiez maintenant retournés, et vous aviez fait ce qui est juste à mes yeux, en proclamant chacun la liberté de son prochain. Vous aviez fait une alliance devant moi, dans la maison qui porte mon nom;
16 Lakini tena mmegeuka na kulichafua jina langu; mmemsababisha kila mtu kumleta tena mtumwa wake wa kiume na wa kike, wale mliowachie kwenda walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa tena.'
mais vous vous êtes détournés et vous avez profané mon nom, et chacun a fait revenir son esclave et sa servante, que vous aviez laissés libres à leur gré. Vous les avez soumis, pour qu'ils soient pour vous des serviteurs et des servantes.'"
17 Kwa hiyo Yahwe asema hivi, 'Ninyi wenyewe hamkunisikiliza. Mlipaswa kuwa mmetangaza uhuru, kila mmoja wenu, kwa ndugu zenu na Waisraeli wenzenu. Kwa hiyo angalia! Niko karibu kutangaza uhuru kwenu—hili ni tangazo la Yahwe—uhuru wa upanga, tauni, na njaa, kwa maana naenda kuwafanya kitu cha ajabu katika macho aya kila ufalme juu ya dunia.
C'est pourquoi Yahvé dit: « Vous ne m'avez pas écouté, pour proclamer la liberté, chacun pour son frère, chacun pour son prochain. Voici, je vous proclame la liberté, dit Yahvé, devant l'épée, la peste et la famine. Je vous ferai aller et venir parmi tous les royaumes de la terre.
18 Kisha nitashughulika na watu waliolivuja agano langu, ambao hawakuyashika maneno ya agano ambalo walilithibitisha mbele zangu walipomkata ng'ombe dume katika vipande viwili na kutembea katika vipande vyake,
Je livrerai les hommes qui ont transgressé mon alliance, qui n'ont pas accompli les paroles de l'alliance qu'ils ont conclue devant moi quand ils ont coupé le veau en deux et sont passés entre ses parties:
19 na kisha viongozi wa Yuda na Yerusalemu, matowashi na makuhani, na watu wote wa nchi wakatembea katika vipande vya yule ng'ombe dume.
les princes de Juda, les princes de Jérusalem, les eunuques, les prêtres et tout le peuple du pays, qui sont passés entre les parties du veau.
20 Nitawatia katika mikono ya adui zao na katika mikono ya hao wanaoutafuta uhai wao. Miili yao itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama juu ya dunia.
Je les livrerai entre les mains de leurs ennemis et entre les mains de ceux qui en veulent à leur vie. Leurs cadavres serviront de nourriture aux oiseaux du ciel et aux animaux de la terre.
21 Kwa hiyo nitawatia Sedekia mfalme wa Yuda na viongozi wake kwenye mikono ya adui zao na kwenye miko ya wale wanaoutafuta uhai wao na katika mikono ya majeshi ya mfalme wa Babeli ambayo yameinuka dhidi yenu.
« Je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses princes entre les mains de leurs ennemis, entre les mains de ceux qui en veulent à leur vie et entre les mains de l'armée du roi de Babylone, qui s'est éloignée de vous.
22 Angalia, niko karibu kutoa amari—hili ni tangazo la Yahwe—na nitawaleta tena kwenye mji huu ili wapigane dhidi yake, na kuunguza kwa moto. Kwa maana nitaigeuza miji ya Yuda kuwa sehemu za ukiwa ambamo hapatakuwa na wakaaji.”
Voici que j'ordonne, dit Yahvé, et que je les fais revenir dans cette ville. Ils la combattront, la prendront et la brûleront par le feu. Je ferai des villes de Juda une désolation, sans habitant. »