< Yeremia 33 >

1 Kisha neno la Yahwe likaja kwa Yeremia mara ya pili, alipokuwa bado amefungwa ndani ya uwanja wa walinzi, likisema,
And the word of the Lord came unto Jeremiah the second time, while he was yet shut up in the court of the prison, saying,
2 Yahwe muumbaji, anasema hivi—Yahwe, aumbaye ili athibitishishe—Yahwe ndilo jina lake,
Thus hath said the Lord who doth this, the Lord that formeth it, to establish it: the Eternal is his name;
3 'Niite, na nitakuitika, nitakuelezea mambo makuu, siri ambazo huzielewi.'
Call unto me, and I will answer thee, and I will tell thee great and unheard of things, which thou knowest not.
4 Kwa maana Yahwe, Mungu wa Israel, anasema hivi kuhusu nyumba zilizo katika mji huu na nyumba za wafalme wa Yuda zilizobomolewa kwa sababu ya maboma na upanga,
For thus hath said the Lord, the God of Israel, concerning the houses of this city, and concerning the houses of the kings of Judah, which are thrown down by means of the mounds, and by means of the sword;
5 Wakaldayao wanakuja kupigana na kuzijaza nyumba kwa hizi kwa majeshi ya watu ambao wataua katika hasira yangu na ghadhabu yangu, nitakapouficha mji huu uso wangu kwa sababu ya uovu wao wote.
As they come to fight with the Chaldeans, but only to fill those with the corpses of the men whom I slay in my anger and in my fury, and for all whose wickedness I have hidden my face from this city:
6 Lakini ona, niko karibu kuleta uponyaji na tiba, kwa maana nitawaponya na nitawapa wingi wa, amani na uamainifu.
Behold, I will bring it healing and cure, and I will cure them, and I will display unto them the abundance of peace and truth.
7 Kwa maana nitawarudhisha wafungwa wao wa Yuda na Israeli; nitawajenga tena kama ilivyokuw mwanzo.
And I will cause to return the captivity of Judah and the captivity of Israel, and I will build them up, as at the first.
8 Kisha nitawatakasa uovu wote walioufanya dhidi yangu. Nitasamehe makosa yote waliyonitenda, na na njia zote walizo asi dhidi yangu.
And I will cleanse them from all their guiltiness, whereby they have sinned against me; and I will pardon all their iniquities, whereby they have sinned toward me, and whereby they have transgressed against me.
9 Kwa maana mji huu kwa ajili yangu utakuwa chombo cha furaha, nyimbo, sifa na heshima kwa mataiafa yote ya dunia ambao watasikia mambo yote mema ninayokwenda kufanya kwa ajili ya huu mji. Kisha wataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mambo yote mema na amani nitayoupa mji huu.'
And it shall be to me for a name of gladness, a praise and an honor with all the nations of the earth, who will hear all the good that I am doing unto them: and they shall dread and tremble because of all the good and because of all the happiness that I prepare unto it.
10 Yahwe anasema hivi, 'Katika sehemu hii ambayo sasa mnaisema, “Imetengwa, sehemu isiyo na mwanadamu wala mnyama,” katika mji huu wa Yuda, na katika mitaa ya Yerusalemu ambayo imetengwa bila mwanadamu wala mnyama, zitasikika tena
Thus hath said the Lord, Yet again shall there be heard in this place, of which ye say, “It is ruined, without man and without beast” [[[even] in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, that are desolate, without man, and without inhabitant, and without beast, ]]
11 sauti za furaha na sauti za shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti za wale wasemao, wanapoleta shukrani katika nyumba ya Yahwe, “Mshukuruni Yahwe wa majeshi, kwa maana Yahwe ni mwema, na upendo wake usioshindwa wadumu milele!” Kwa maana nitawafanaya tena wafungwa wa nchi kuwa walivyokuwa mwanzo,' asema Yahwe.
The voice of gladness, and the voice of joy, the voice of the bridegroom, and the voice of the bride, the voice of those that say, “Give thanks unto the Lord of hosts; for the Lord is good; because to eternity endureth his kindness:” of those that bring thanksgiving-offering unto the house of the Lord. For I will cause to return the captivity of the land, as at the first, saith the Lord.
12 Yahwe wa majeshi asema hivi: Katika sehemu hii ya ukiwa, ambamo sasa hakuna mwanadamu wala mnyama—katika miji yake yote kutakuwepo tena malisho ambapo wachungaji wataweza kupumzisha makundi yao.
Thus hath said the Lord of hosts, Yet again shall there be in this place, which is ruined, without man and even without beast, and in all its cities, a habitation of shepherds who cause their flocks to lie down.
13 Katika miji hii katika nchi ya vilima, nchi tambarare, na Negevu katika nchi ya Benyamini na kuzunguka Yerusalemu yote, na katika miji ya Yuda, makundi yatapata njia chini ya mkono wa yule anayewahesabu,' asema Yahwe.
In the cities of the mountain, in the cities of the lowlands, and in the cities of the south, and in the land of Benjamin, and in the environs of Jerusalem, and in the cities of Judah, shall the flocks yet pass again under the hands of him that counteth them, saith the Lord.
14 Angalia! Siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—ambapo nitafanya niliyoahidi kwa nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
Behold, days are coming, saith the Lord, when I will fulfill that good word which I have spoken concerning the house of Israel and respecting the house of Judah.
15 Katika siku hizo na katika wakati huo nitachipua shina la haki kwa ajili ya Daudi, na litafanaya hukumu na haki katika nchi.
In those days, and at that time, will I cause to grow up unto David the sprout of righteousness: and he shall execute justice and righteousness in the land.
16 Katika siku hizo Yuda wataokolewa, na Yurusalemu utaishi katika usalama, kwa maana hivi ndivyo atakavyoitwa, “Yahwe ni haki ni haki yetu.”
In those days shall Judah be helped, and Jerusalem shall dwell in safety: and this is what she shall be called, The Lord is our righteousness.
17 Kwa maana Yahwe anasema hivi: 'Mwana kutoka ukoo wa Daudi hatakosa kuketi katika kiti cha nyumba ya Israeli,
For thus hath said the Lord, There shall never be wanting unto David a man to sit upon the throne of the house of Israel;
18 wala mtu kutoka ukuhani wa Kilawi hatakosa kutoa sadaka za kuteketezwa mbele zangu, kutoa sadaka za chakula, na kutoa sadaka za nafaka wakati wote.”'
And unto the priests the Levites there shall not be wanting a man before me, to offer burnt-offerings, and to burn meat-offerings, and to prepare sacrifices at all times.
19 Neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,
And the word of the Lord came unto Jeremiah, saying,
20 “Yahwe anasema hivi: 'Kama mkiweza kulivunja agano langu la mchana na usiku ili kwamba siku isikawie wala usiku usikawie kuja kwa wakati wake,
Thus hath said the Lord, If ye can break my covenant with the day, and my covenant with the night, and so, that there be not day and night in their season:
21 basi mtaweza u kulivunja agano langu na Daudi mtumishi wangu, ili kwamba aspate mwana wa kuketi juu ya kiti chake cha enzi, na gano langu na makuhuni wa Kilawi, watumishsi wangu.
Then also shall my covenant be broken with David my servant, that he should not have a son to reign upon his throne; and [that] with the Levites the priests, my ministers.
22 Kama vile majeshsi ya mbinguni yasivyoweza kuhesabika, na kama vile mchanga wa ufukwe wa bahari usivyoweza kupimwa, ndivyo nitakavyouongeza uzao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi watumikao mbele zangu.”
As the host of heaven cannot be numbered, and the sand of the sea not be measured: so will I multiply the seed of David my servant, and the Levites that minister unto me.
23 Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,
And the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
24 Hamkuzingatia walichotangaza watu hawa waliposema, 'Zile Familia mbili ambazo Yahwe alizichagua, sasa amezikataa'? Kwa jinsi hii hii waliwapuuza watu wangu, wakisema kwamba si taifa tena katika macho yao.
Hast thou not observed what this people have spoken, saying, The two families which the Lord hath made choice of, even these hath he rejected: and they [thus] have despised my people, that they should be no more a nation before them.
25 Mimi, Yahwe, nasema hivi, 'Kama sijalithibitisha agano la mchana na usiku, na kama sijaziweka sheria za mbingu na dunia,
Thus hath said the Lord, If my covenant be not with day and night, if I have not appointed the ordinances of heaven and earth:
26 basi nitawakataa uzao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na nisilete mtu kutoka kati yao wa kutawala juu ya uzao wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha wafubgwa wao na kuonesha huruma kwao.”'
Then also will I reject the seed of Jacob, and David my servant, so as not to take any of his seed to be rulers over the seed of Abraham, Isaac, and Jacob; for I will cause their captivity to return, and have mercy on them.

< Yeremia 33 >