< Yeremia 32 >

1 Neno likaja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe katika mwaka wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.
Telle fut la parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahvé, la dixième année de Sédécias, roi de Juda, qui était la dix-huitième année de Nabuchodonosor.
2 Katika wakati huo, jeshsi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka Yerusalemu, na Nehemia nabii alikuwwa amefungwa katika uwanja wa walinzi katika nyumba ya mfalme wa Yuda.
En ce temps-là, l'armée du roi de Babylone assiégeait Jérusalem. Jérémie, le prophète, était enfermé dans la cour des gardes, qui était dans la maison du roi de Juda.
3 Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga na kusema, “Kwa nini unatabiri na kusema, 'Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kuweka mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, na atauteka.
Car Sédécias, roi de Juda, l'avait fait taire, en disant: Pourquoi prophétises-tu, en disant: Yahvé dit: Voici, je livre cette ville entre les mains du roi de Babylone, et il la prendra;
4 Sedekia mfalme wa Yuda hatapona kutoka kwenye mikono ya Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli. Mdomo wake utazumzia kwenye mdomo wa mfalme, na macho yake yatayaona macho ya mfalme.
et Sédécias, roi de Juda, n'échappera pas à la main des Chaldéens, mais il sera livré entre les mains du roi de Babylone, il parlera avec lui bouche à bouche, et ses yeux verront ses yeux;
5 Atampeleka Sedekia Babeli, na atabaki huko hadi nimuadhibu—hili ni tangazo la Yahwe. Ingawa unapigana dhidi ya Wakaldayo, hautafanikiwa.”
et il emmènera Sédécias à Babylone, et il y restera jusqu'à ce que je le visite, dit Yahvé, bien que tu combattes les Chaldéens, tu ne prospéreras pas? »'"
6 Yeremia akasema, “Neno la Yahwe likaja kwangu, likisema, Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako anakuja kwako na atasema,
Jérémie dit: « La parole de Yahvé m'a été adressée en ces termes:
7 “Linunue shamba langu ambalo liko katika Anathothi kwa ajili yako, kwa maana haki ya kununua ni yako.””
Voici que Hanamel, fils de Shallum, ton oncle, vient te voir et te dit: « Achète mon champ qui est à Anathoth, car le droit de rachat te revient pour l'acheter ».
8 Kisha, kama Yahwe alivyotangaza, Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akaja kwangu katika uwanja wa walinzi, na akasema kwangu, 'Linunue shamba langu kwa ajili yako ambalo liko Anathothi katika nchi ya Benyamini, kwa maana haki ya urithi ni ya kwako, na haki ya kulinunua ni yako. Linunue kwa ajili yako.' Kisha nilijua kuwa hili lilikuwa neno la Yahwe.
« Hanamel, fils de mon oncle, vint me voir dans la cour des gardes, selon la parole de Yahvé, et me dit: « Achète, je te prie, mon champ qui est à Anathoth, dans le pays de Benjamin, car le droit d'héritage est à toi, et le rachat est à toi. Achète-le pour toi-même. « Je sus alors que telle était la parole de Yahvé.
9 Kwa hiyo nililinua shamba katika Anathothi kutoka kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na nilipima fedha kwa ajili yake, shekeli kumi na saba katika uzito.
J'achetai le champ d'Anathoth au fils de Hanamel, mon oncle, et je lui pesai l'argent, dix-sept sicles d'argent.
10 Kisha niliandika katika barua na kuitia muhuri, na kulikuwa na mashadi wakaishuhudia. Kisha nikampa fedha katika mizani.
J'ai signé l'acte, je l'ai scellé, j'ai appelé des témoins et je lui ai pesé l'argent dans les balances.
11 Kisha nikaichukua hati ya manunuzi ambayo ilikuwa imepigwa muhuri, kwa kuifuata amri na taratibu, na kama ilivyo ada.
Je pris l'acte d'achat, celui qui était scellé, contenant les conditions, et celui qui était ouvert;
12 Ile barua nikampa Baruku mwana wa Neria wa Maaseya mbele ya Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mashahidi waliotia sahihi kwenye barua iliyopigwa muhuri, na mbele ya Wayahudi wote waliokaa katika uwanja wa walinzi.
et je remis l'acte d'achat à Baruch, fils de Neriah, fils de Mahséja, en présence de Hanamel, fils de mon oncle, et en présence des témoins qui avaient signé l'acte d'achat, devant tous les Juifs qui siégeaient dans la cour des gardes.
13 Kwa hiyo nikampa amri Baruku mbele yao. Nilisema,
J'ai donné cet ordre à Baruch en leur présence:
14 Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Chukua nyaraka hizi, vyote hati hii ya manunuzi iliyopigwa muhuri na nakala zisizopigwa muhuri za manunuzi, na uziweke katika chungu cha udongo ili vidumu kwa muda mrefu.
L'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Prends ces actes, cet acte d'achat scellé et cet acte ouvert, et mets-les dans un vase d'argile, pour qu'ils durent plusieurs jours.
15 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nyumba, mashamba, na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika nchi hii.
Car Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « On achètera encore dans ce pays des maisons, des champs et des vignes.
16 Baada ya kumpa Baruki mwana wa Neria ile hati ya manunuzi, nikaomba kwa Yahwe nikasema,
Après avoir remis l'acte d'achat à Baruch, fils de Neriah, j'ai prié l'Éternel, en disant,
17 Ole, Bwana Yahwe! Angalia! Wewe peke yako umezitengeneza mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulioinuka. Hakuna kitu ambacho ukisema kwako ni kigumu sana kukifanya.
« Ah Seigneur Yahvé! Voici que tu as fait les cieux et la terre par ta grande puissance et par ton bras étendu. Rien n'est trop dur pour toi.
18 Wewe huonesha agano la uaminifu kwa maelfu na kumimina makosa ya wanadamu katika mapaja ya watoto wao baada yao. Wewe ni Mungu mkuu na mwenye nguvu.
Tu fais preuve de bonté envers des milliers de personnes, et tu reverses l'iniquité des pères dans le sein de leurs enfants après eux. Ton nom est le Dieu grand et puissant, le Yahvé des armées:
19 Wewe ni mkuu katika hekima na una nguvu katika matendo, kwa maana macho yako yanaona njia zote za watu, ili kumlipa kila mtu stahiki ya matendo yake.
grand par ses conseils et puissant par ses œuvres, qui a les yeux ouverts sur toutes les voies des enfants des hommes, pour rendre à chacun selon ses voies et selon le fruit de ses œuvres;
20 Ulifanya ishara na maajabu katika nchi ya Misiri. Hata leo hapa Israeli na kati ya wanadamu wengine wote, umelifanya jina lako kuwa maarufu.
qui a opéré des signes et des prodiges au pays d'Égypte, jusqu'à ce jour, tant en Israël que parmi les autres hommes; et tu t'es fait un nom, comme il l'est aujourd'hui;
21 Kwa maana uliwanunua watu wako Israeli kwa ishira na maajabu, kwa mkono hodari, kwa mkono ulioinuka, na kwa hofu kuu.
et tu as fait sortir ton peuple Israël du pays d'Égypte avec des signes, avec des prodiges, avec une main forte, avec un bras étendu, et avec une grande terreur;
22 Kisha uliwapa nchi hii—ambayo uliapa kwa babu zao kwamba utawapa—nchi itiririkayo maziwa na asali.
et tu leur as donné ce pays, que tu avais juré à leurs pères de leur donner, un pays où coulent le lait et le miel.
23 Hivyo walingia na kuimiliki. Lakini hawakuitii sauti yako wala kuishi kwa kuitii sheria yako. Hawakufanya chochote ulichowaamuru kufanya, kwa hiyo umeleta juu yao majanga haya yote.
Ils y sont entrés et l'ont possédé, mais ils n'ont pas obéi à ta voix et n'ont pas suivi ta loi. Ils n'ont rien fait de tout ce que tu leur avais ordonné de faire. C'est pourquoi tu as fait venir sur eux tout ce malheur.
24 Angalia! Urefu wa maboma haya umefika hadi kwenye mji ili kuuteka. Kwa sababu ya upanga, njaa, na tauni, mji umetiwa kwenye mikono ya Wakaldayo wanaopigana dhidi yake. Kwa maana ulichosema kitatokea sasa kinatokea, na ona, unatazama.
« Voici, on a construit des rampes de siège contre la ville pour la prendre. La ville est livrée entre les mains des Chaldéens qui la combattent, à cause de l'épée, de la famine et de la peste. Ce que tu as dit est arrivé. Voici, tu le vois.
25 Kisha wewe mwenyewe uliniambia, “Nunua shamba kwa fedha kwa ajili yako na mashahidi wameshuhudia, ingawa mji huu unatiwa mikononi mwa Wakaldayo.””
Tu m'as dit, Seigneur Yahvé: « Achète le champ à prix d'argent, et appelle des témoins »; mais la ville a été livrée entre les mains des Chaldéens. »
26 Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,
Alors la parole de Yahvé fut adressée à Jérémie, en ces termes:
27 “Angalia! Mimi ni Yahwe, Mungu wa wanadamu wote. Kuna kitu cho chote kigumu sana kwangu kukifanya?
« Voici, je suis Yahvé, le Dieu de toute chair. Y a-t-il quelque chose de trop dur pour moi?
28 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi, 'Ona, niko karibu kuutia mji huu kwenye mikono ya Wakaldayo na Nebukadreza, mfalme wa Babeli. Atauteka.
C'est pourquoi Yahvé dit: Voici, je vais livrer cette ville entre les mains des Chaldéens, entre les mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et il la prendra.
29 Wakaldayo wanaopigana dhidi ya mji huu watakuja na kuwasha moto kwenye mji huu na kuunguza, pamoja na nyumba juu ya paa la watu waliomwabudu Baali na kumimina dhabihu kwa miungu wengine ili kunikasirisha.
Les Chaldéens, qui combattent cette ville, viendront et mettront le feu à cette ville, et ils la brûleront avec les maisons sur les toits desquelles ils ont offert de l'encens à Baal et versé des libations à d'autres dieux, pour m'irriter.
30 Kwa maana watu wa Israeli na Yuda hakika wamekuwa watu wanaofanya maovu mbele ya macho yangu tangu ujana wao. Watu wa Israeli hakika wameniudhi kwa matendo ya mikono yao—hili ni tangazo la Yahwe.
« Car les enfants d'Israël et les enfants de Juda n'ont fait que ce qui était mauvais à mes yeux dès leur jeunesse; car les enfants d'Israël n'ont fait que m'irriter par l'ouvrage de leurs mains, dit l'Éternel.
31 Yahwe anatangaza kwamba mji huu umekuwa sababu ya hasira yangu na ghadhabu yangu tangu siku walipoujenga. Umekuwa hivyo hata leo. Kwa hiyo nitaundoa mbele ya uso wangu
Car cette ville a été pour moi une provocation à ma colère et à ma fureur, depuis le jour où ils l'ont bâtie jusqu'à ce jour, pour que je l'enlève de devant ma face,
32 kwa sababu ya uovu wote wa watu wa Israeli na Yuda, mambo waliyofanya ili kunichukiza—wao, wafalme wao, wana wa wafalme, makuhani, manabii, na kila mtu katika Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.
à cause de tout le mal que les enfants d'Israël et les enfants de Juda ont fait pour m'irriter, eux, leurs rois, leurs princes, leurs prêtres, leurs prophètes, les hommes de Juda et les habitants de Jérusalem.
33 Wamenigeuzia migongo yao badala ya nyuso zao, ingawa niliwafundisha kwa furaha. Nilijitahidi kuwafundisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyenisikiliza ili kupokea marekebisho.
Ils m'ont tourné le dos, et non le visage. Bien que je les aie instruits, me levant de bonne heure et les instruisant, ils n'ont pas écouté pour recevoir l'instruction.
34 Walisimamisha sanamu zao za ajabu katika nyumba inayoitwa kwa jina langu, ili kunitia unajisi.
Mais ils ont placé leurs abominations dans la maison qui porte mon nom, pour la souiller.
35 Wakazijenga sehemu za juu katika Bonde la Beni Hinomu ili kuwatia katika moto wana wao na binti zao kwa ajili ya Moleki. Mimi sikuwaagiza. Sikuweka akilini mwangu kamwe kwamba watafanya mambo maovu na kwa hiyo kuwasabisha Yuda watende dhambi.
Ils ont bâti les hauts lieux de Baal, qui sont dans la vallée du fils de Hinnom, pour faire passer leurs fils et leurs filles par le feu à Moloch, ce que je ne leur ai pas commandé. Il ne m'est même pas venu à l'esprit qu'ils devaient faire cette abomination, pour faire pécher Juda. »
36 Kwa hiyo sasa, Mimi, Yahwe, Mungu wa Israeli, kuhusu mji huu ninasema hivi, 'mji ambao mnasema, 'Umetiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli kwa upanga, njaa, na pigo.'
Maintenant, Yahvé, le Dieu d'Israël, dit au sujet de cette ville dont vous dites: « Elle a été livrée entre les mains du roi de Babylone par l'épée, par la famine et par la peste »:
37 Ona, niko karibu kuwakusanya kutoka kila nchi nilikowapeleka katika hasira yangu, ghadhabu, hasira kuu. Niko karibu kuwarudisha kwenye sehemu hii na kuwawezesha kuishi katika usalama.
« Voici, je les rassemblerai de tous les pays où je les ai chassés dans ma colère, dans ma fureur et dans ma grande indignation, et je les ramènerai dans ce lieu. Je les ferai habiter en sécurité.
38 Kisha watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
Alors ils seront mon peuple, et je serai leur Dieu.
39 Nitawapa moyo mmjoa na na njia moja ya kuniheshimu kila siku ili kwamba yawepo mema kwa ajili yao na uzao wao baada yao.
Je leur donnerai un seul cœur et une seule voie, afin qu'ils me craignent toujours, pour leur bien et celui de leurs enfants après eux.
40 Kisha nitafanya pamoja nao agano la milele, ili nisiache kufanya mema kwa ajili yao. nitajiwekea heshima katika mioyo yao, ili kwamba wasiniache.
Je conclurai avec eux une alliance éternelle, et je ne me détournerai pas de les suivre pour leur faire du bien. Je mettrai ma crainte dans leur cœur, pour qu'ils ne s'éloignent pas de moi.
41 Kisha nitajifurahisha katika kufanya mema kwao. Kwa uaminifu nitawapanda katika anchi hii kwa moyo wangu wote na maisha yangu yoye.
Oui, je me réjouirai d'eux pour leur faire du bien, et je les planterai dans ce pays avec assurance, de tout mon cœur et de toute mon âme. »
42 Kwa amaana Yahwe anasema hivi, 'Kama tu nilivyoyaleta majanga haya makubwa yote juu ya watu hawa, hivyo hivyo nitaleta juu yao mambo mema niliyosema kwamba nitafanya kwa ajili yao.
Car Yahvé dit: « De même que j'ai fait venir sur ce peuple tout ce grand malheur, de même je ferai venir sur lui tout le bien que je lui ai promis.
43 Basi mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, ambayo mnaisema, “Hii ni nchi iliyoharibiwa, isiyo na mwanadamu wala mnyama. Imetiwa mikononi mwa Wakaldayo”
On achètera des champs dans ce pays dont vous dites: « Il est désert, sans homme ni bête. Il est livré entre les mains des Chaldéens ».
44 Watanunua mashamba kwa fedha na kuandika katika barua zilizopigwa muhuri. Watawakusanya mashahidi katika nchi ya Benyamini, wote kuzunguka Yerusalemu na miji ya Yuda katika miji ya nchi yenye vilima, na katika nchi tambarare, na katika miji ya Negebu. Kwa maana nitawarejesha wafungwa wao—hili ni tangazo la Yahwe.”'
Onachètera des champs à prix d'argent, on signera les actes, on les scellera, on appellera des témoins, dans le pays de Benjamin, dans les environs de Jérusalem, dans les villes de Juda, dans les villes de la montagne, dans les villes de la plaine, dans les villes du Midi, car je ferai revenir leur captivité, dit Yahvé.

< Yeremia 32 >