< Yeremia 32 >

1 Neno likaja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe katika mwaka wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.
After Zedekiah had been ruling Judah for almost ten years, Yahweh gave me another message, during the time that Nebuchadnezzar had been ruling [Babylonia] for almost 18 years.
2 Katika wakati huo, jeshsi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka Yerusalemu, na Nehemia nabii alikuwwa amefungwa katika uwanja wa walinzi katika nyumba ya mfalme wa Yuda.
His army was surrounding Jerusalem, and I was in a prison area in the courtyard where the guards of the king’s palace stayed.
3 Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga na kusema, “Kwa nini unatabiri na kusema, 'Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kuweka mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, na atauteka.
King Zedekiah had put me there. I continued to prophesy there [about what would happen]. I continued to say, “Yahweh says that he is about to allow [the army of] the king of Babylon to capture this city [DOU].
4 Sedekia mfalme wa Yuda hatapona kutoka kwenye mikono ya Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli. Mdomo wake utazumzia kwenye mdomo wa mfalme, na macho yake yatayaona macho ya mfalme.
And the soldiers of Babylonia will capture King Zedekiah and (take him to/put him in the hands of) the king of Babylon.
5 Atampeleka Sedekia Babeli, na atabaki huko hadi nimuadhibu—hili ni tangazo la Yahwe. Ingawa unapigana dhidi ya Wakaldayo, hautafanikiwa.”
Then his [soldiers] will take Zedekiah to Babylon, and he will remain there until I arrange for him to be punished. And if he tries to fight against the soldiers from Babylonia, he will not succeed.”
6 Yeremia akasema, “Neno la Yahwe likaja kwangu, likisema, Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako anakuja kwako na atasema,
[At that time], Yahweh gave me another message. He said,
7 “Linunue shamba langu ambalo liko katika Anathothi kwa ajili yako, kwa maana haki ya kununua ni yako.””
“[Your cousin] Hanamel, the son of Shallum [your uncle], will come to you. He will say to you, ‘Buy my field at Anathoth, [your hometown]. [Because you are my closest relative], [it is written in our laws that] you have the right to buy it [before I ask if anyone else wants to buy it].’”
8 Kisha, kama Yahwe alivyotangaza, Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akaja kwangu katika uwanja wa walinzi, na akasema kwangu, 'Linunue shamba langu kwa ajili yako ambalo liko Anathothi katika nchi ya Benyamini, kwa maana haki ya urithi ni ya kwako, na haki ya kulinunua ni yako. Linunue kwa ajili yako.' Kisha nilijua kuwa hili lilikuwa neno la Yahwe.
And just as Yahweh had predicted, my cousin Hanamel came to see me in the courtyard of the palace. He said, “[Please] buy my field at Anathoth in the area [where the descendants of] Benjamin live. It is written in our laws that you have the right to buy it [before I ask if anyone else wants to buy it.]” When he said that, I knew that the message that I had received was [truly] from Yahweh.
9 Kwa hiyo nililinua shamba katika Anathothi kutoka kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na nilipima fedha kwa ajili yake, shekeli kumi na saba katika uzito.
[So], I bought the field at Anathoth. I paid Hanamel 17 pieces of silver for it.
10 Kisha niliandika katika barua na kuitia muhuri, na kulikuwa na mashadi wakaishuhudia. Kisha nikampa fedha katika mizani.
I signed the paper/papyrus on which it was written that I was buying it, while others were watching/witnessing it. Then I weighed the silver [and gave it to him].
11 Kisha nikaichukua hati ya manunuzi ambayo ilikuwa imepigwa muhuri, kwa kuifuata amri na taratibu, na kama ilivyo ada.
Then I took two copies of the paper/papyrus. One was sealed and the other was not sealed. On both of them was written the price and conditions of the purchase. I took both copies
12 Ile barua nikampa Baruku mwana wa Neria wa Maaseya mbele ya Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mashahidi waliotia sahihi kwenye barua iliyopigwa muhuri, na mbele ya Wayahudi wote waliokaa katika uwanja wa walinzi.
and I gave them to Baruch, who was the son of Neraiah and the grandson of Mahseiah. I did this while my cousin Hanamel, the [other] witnesses who had signed the paper/papyrus, and other men of Judah who were there in the courtyard, were watching.
13 Kwa hiyo nikampa amri Baruku mbele yao. Nilisema,
[Then], while they were [all] listening, I said to Baruch,
14 Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Chukua nyaraka hizi, vyote hati hii ya manunuzi iliyopigwa muhuri na nakala zisizopigwa muhuri za manunuzi, na uziweke katika chungu cha udongo ili vidumu kwa muda mrefu.
“This is what the Commander of the armies of angels, the God whom [we] Israelis [worship], says: ‘Take both copies of this paper/papyrus and put them in a clay jar, to preserve them for a long time.
15 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nyumba, mashamba, na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika nchi hii.
[Do that] because this is what [I], the Commander of the armies of angels, the God whom [you] Israelis [worship], say: “[Some day people will again own property] in this land, and they will buy and sell houses and vineyards and fields.’”
16 Baada ya kumpa Baruki mwana wa Neria ile hati ya manunuzi, nikaomba kwa Yahwe nikasema,
After I had given the papers/papyri to Baruch, I prayed to Yahweh, saying this:
17 Ole, Bwana Yahwe! Angalia! Wewe peke yako umezitengeneza mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulioinuka. Hakuna kitu ambacho ukisema kwako ni kigumu sana kukifanya.
“Yahweh, [you are my] Lord! You made the sky and the earth by your very great power. [MTY, DOU] Nothing is too difficult for you [to do].
18 Wewe huonesha agano la uaminifu kwa maelfu na kumimina makosa ya wanadamu katika mapaja ya watoto wao baada yao. Wewe ni Mungu mkuu na mwenye nguvu.
You show thousands of people that you faithfully love them, but you punish people for the sins that their parents have committed. [You are the] great and powerful God, the Commander of the armies of angels.
19 Wewe ni mkuu katika hekima na una nguvu katika matendo, kwa maana macho yako yanaona njia zote za watu, ili kumlipa kila mtu stahiki ya matendo yake.
You make wise plans and you do mighty deeds. You see how all people behave [DOU], and you do to them what they deserve.
20 Ulifanya ishara na maajabu katika nchi ya Misiri. Hata leo hapa Israeli na kati ya wanadamu wengine wote, umelifanya jina lako kuwa maarufu.
You performed many miracles [DOU] in Egypt, and you continue [to perform miracles here] in Israel and everywhere else in the world. [Because of that], you have (become very famous/caused many people to know that you are very great/powerful).
21 Kwa maana uliwanunua watu wako Israeli kwa ishira na maajabu, kwa mkono hodari, kwa mkono ulioinuka, na kwa hofu kuu.
You brought our Israeli ancestors out of Egypt by performing many great miracles [DOU], using your very great power [DOU], causing [our enemies to be] terrified.
22 Kisha uliwapa nchi hii—ambayo uliapa kwa babu zao kwamba utawapa—nchi itiririkayo maziwa na asali.
You gave to us Israeli people this land that you solemnly promised to give to our ancestors, a land that is very fertile [IDM].
23 Hivyo walingia na kuimiliki. Lakini hawakuitii sauti yako wala kuishi kwa kuitii sheria yako. Hawakufanya chochote ulichowaamuru kufanya, kwa hiyo umeleta juu yao majanga haya yote.
Our ancestors came here and conquered this land and started to live in it, but they refused to obey you or to do what you commanded them to do. Because of that, you have caused us to experience all these disasters.
24 Angalia! Urefu wa maboma haya umefika hadi kwenye mji ili kuuteka. Kwa sababu ya upanga, njaa, na tauni, mji umetiwa kwenye mikono ya Wakaldayo wanaopigana dhidi yake. Kwa maana ulichosema kitatokea sasa kinatokea, na ona, unatazama.
And now, [the army] of Babylonia has built ramps up against our city [walls] in order to attack our city. Because of [our enemies’] swords and because of famines and diseases, they will be able to conquer it [easily]. The things that you said would happen have [now] happened.
25 Kisha wewe mwenyewe uliniambia, “Nunua shamba kwa fedha kwa ajili yako na mashahidi wameshuhudia, ingawa mji huu unatiwa mikononi mwa Wakaldayo.””
[And it is evident that] the Babylonian army will soon conquer this city. So now, Yahweh my Lord, [I do not understand] why you told me to buy this field with my silver, while others were watching. [It seems that I have just been wasting my money by doing that]!”
26 Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,
[Then] Yahweh gave me this message:
27 “Angalia! Mimi ni Yahwe, Mungu wa wanadamu wote. Kuna kitu cho chote kigumu sana kwangu kukifanya?
“I am Yahweh, the God [who rules] all the people [in the world]. There is absolutely nothing [RHQ] that is too difficult for me [to do].
28 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi, 'Ona, niko karibu kuutia mji huu kwenye mikono ya Wakaldayo na Nebukadreza, mfalme wa Babeli. Atauteka.
So, this is what I say: [It is true that] I will enable the Babylonian army and King Nebuchadnezzar to capture this city.
29 Wakaldayo wanaopigana dhidi ya mji huu watakuja na kuwasha moto kwenye mji huu na kuunguza, pamoja na nyumba juu ya paa la watu waliomwabudu Baali na kumimina dhabihu kwa miungu wengine ili kunikasirisha.
The soldiers of Babylonia who are [now outside the walls] around the city will enter and burn this city. They will burn down [all] the houses where people caused me to become angry by burning incense on [the tops of] their roofs to [honor] Baal and by pouring out offerings of wine to other gods.
30 Kwa maana watu wa Israeli na Yuda hakika wamekuwa watu wanaofanya maovu mbele ya macho yangu tangu ujana wao. Watu wa Israeli hakika wameniudhi kwa matendo ya mikono yao—hili ni tangazo la Yahwe.
The people of Israel and Judah have continually done only evil things from the time that they became a nation. They have caused me to become very angry by all their evil deeds.
31 Yahwe anatangaza kwamba mji huu umekuwa sababu ya hasira yangu na ghadhabu yangu tangu siku walipoujenga. Umekuwa hivyo hata leo. Kwa hiyo nitaundoa mbele ya uso wangu
From the time that this city was built until now, the people of this city have done [only] things that caused me to be very angry [DOU]. So [now] I will destroy it.
32 kwa sababu ya uovu wote wa watu wa Israeli na Yuda, mambo waliyofanya ili kunichukiza—wao, wafalme wao, wana wa wafalme, makuhani, manabii, na kila mtu katika Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.
The people of Israel and Judah, [including] their kings, their officials, the priests, the [false] prophets, and all the other people in Jerusalem have committed many sins that have caused me to become angry.
33 Wamenigeuzia migongo yao badala ya nyuso zao, ingawa niliwafundisha kwa furaha. Nilijitahidi kuwafundisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyenisikiliza ili kupokea marekebisho.
My people have turned away from me and have refused to return to me. Even though I taught them things many times, they would not pay attention to what I taught them, and they would not obey me.
34 Walisimamisha sanamu zao za ajabu katika nyumba inayoitwa kwa jina langu, ili kunitia unajisi.
They have set up their detestable idols [even] in my own [MTY] temple and (defiled it/caused it to become a place that is unacceptable for people to worship me).
35 Wakazijenga sehemu za juu katika Bonde la Beni Hinomu ili kuwatia katika moto wana wao na binti zao kwa ajili ya Moleki. Mimi sikuwaagiza. Sikuweka akilini mwangu kamwe kwamba watafanya mambo maovu na kwa hiyo kuwasabisha Yuda watende dhambi.
They have built shrines to [honor] Baal in Ben-Hinnom Valley [outside Jerusalem], and there they sacrifice their sons and daughters to [their god] Molech. I never commanded them to do such horrible things. I never even thought that anyone might do such a terrible thing. And by doing it they have caused [all the people of] Judah to [be guilty of having] sinned.”
36 Kwa hiyo sasa, Mimi, Yahwe, Mungu wa Israeli, kuhusu mji huu ninasema hivi, 'mji ambao mnasema, 'Umetiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli kwa upanga, njaa, na pigo.'
“But now [I will say something more] about this city. You [people of Jerusalem] have been saying, ‘[The army of] the King of Babylon will conquer it, either by their swords or because of famines or diseases.’ But this is what [I], Yahweh, the God whom you Israeli people [say you belong to], say:
37 Ona, niko karibu kuwakusanya kutoka kila nchi nilikowapeleka katika hasira yangu, ghadhabu, hasira kuu. Niko karibu kuwarudisha kwenye sehemu hii na kuwawezesha kuishi katika usalama.
‘I will certainly bring my people back here again, from all the countries to which I will force them to go because I am extremely angry [DOU] with them. I will bring them back to this city and allow them to live here safely.
38 Kisha watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
They will be my people, and I will be their God.
39 Nitawapa moyo mmjoa na na njia moja ya kuniheshimu kila siku ili kwamba yawepo mema kwa ajili yao na uzao wao baada yao.
I will cause them to have one way of thinking [IDM] and behaving, in order that they may revere me, for their good and for the good of their descendants.
40 Kisha nitafanya pamoja nao agano la milele, ili nisiache kufanya mema kwa ajili yao. nitajiwekea heshima katika mioyo yao, ili kwamba wasiniache.
I will make an agreement with them that will last forever: I will never stop doing good things for them, and I will encourage them to revere me and never turn away from me.
41 Kisha nitajifurahisha katika kufanya mema kwao. Kwa uaminifu nitawapanda katika anchi hii kwa moyo wangu wote na maisha yangu yoye.
I will be happy to do good things for them, and I will surely enable them to return to this land and remain here [MET]; I will do that with all my inner being and all my strength.’
42 Kwa amaana Yahwe anasema hivi, 'Kama tu nilivyoyaleta majanga haya makubwa yote juu ya watu hawa, hivyo hivyo nitaleta juu yao mambo mema niliyosema kwamba nitafanya kwa ajili yao.
And this is [also] what [I], Yahweh, say: ‘I have caused them to experience all these disasters. Similarly, [some day] I will do for them all the good things that I have promised.
43 Basi mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, ambayo mnaisema, “Hii ni nchi iliyoharibiwa, isiyo na mwanadamu wala mnyama. Imetiwa mikononi mwa Wakaldayo”
[By buying land you, Jeremiah, have predicted that some day] people will buy and sell fields in this land about which you [people of Jerusalem] now say, “The Babylonian soldiers have destroyed it. It is [now] desolate. [It is a land where] there are no longer any people or animals.”
44 Watanunua mashamba kwa fedha na kuandika katika barua zilizopigwa muhuri. Watawakusanya mashahidi katika nchi ya Benyamini, wote kuzunguka Yerusalemu na miji ya Yuda katika miji ya nchi yenye vilima, na katika nchi tambarare, na katika miji ya Negebu. Kwa maana nitawarejesha wafungwa wao—hili ni tangazo la Yahwe.”'
[But some day] people will [again] buy [and sell] fields here. People will sign documents [about buying those fields], and [other people] will witness them doing that. [That will happen] in the land where [the descendants of] Benjamin live and [here] in the villages near Jerusalem, in [other] towns in Judah, in the hilly areas and in the foothills [to the west], and in the southern desert area, [too. Some day] I will cause them to prosper again. [That will surely happen because I], Yahweh, have said it.’”

< Yeremia 32 >