< Yeremia 32 >

1 Neno likaja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe katika mwaka wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.
The word which it came to Jeremiah from with Yahweh (in the year *Q(K)*) tenth of Zedekiah [the] king of Judah that [was] the year eight-teen year of Nebuchadnezzar.
2 Katika wakati huo, jeshsi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka Yerusalemu, na Nehemia nabii alikuwwa amefungwa katika uwanja wa walinzi katika nyumba ya mfalme wa Yuda.
And then [the] army of [the] king of Babylon [were] laying siege on Jerusalem and Jeremiah the prophet he was shut up in [the] courtyard of the guard which [was] [the] house of [the] king of Judah.
3 Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga na kusema, “Kwa nini unatabiri na kusema, 'Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kuweka mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, na atauteka.
Where he had shut up him Zedekiah [the] king of Judah saying why? [are] you prophesying saying thus he says Yahweh here I [am] about to give the city this in [the] hand of [the] king of Babylon and he will capture it.
4 Sedekia mfalme wa Yuda hatapona kutoka kwenye mikono ya Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli. Mdomo wake utazumzia kwenye mdomo wa mfalme, na macho yake yatayaona macho ya mfalme.
And Zedekiah [the] king of Judah not he will escape from [the] hand of the Chaldeans for certainly he will be given in [the] hand of [the] king of Babylon and it will speak mouth his with mouth his and eyes his (eyes his *Q(K)*) they will see.
5 Atampeleka Sedekia Babeli, na atabaki huko hadi nimuadhibu—hili ni tangazo la Yahwe. Ingawa unapigana dhidi ya Wakaldayo, hautafanikiwa.”
And Babylon he will take Zedekiah and there he will be until give attention to I him [the] utterance of Yahweh if you will fight with the Chaldeans not you will succeed.
6 Yeremia akasema, “Neno la Yahwe likaja kwangu, likisema, Angalia, Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako anakuja kwako na atasema,
And he said Jeremiah it came [the] word of Yahweh to me saying.
7 “Linunue shamba langu ambalo liko katika Anathothi kwa ajili yako, kwa maana haki ya kununua ni yako.””
Here! Hanamel [the] son of Shallum uncle your [is] about to come to you saying buy for yourself field my which [is] at Anathoth for [belongs] to you [the] right of redemption to buy [it].
8 Kisha, kama Yahwe alivyotangaza, Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akaja kwangu katika uwanja wa walinzi, na akasema kwangu, 'Linunue shamba langu kwa ajili yako ambalo liko Anathothi katika nchi ya Benyamini, kwa maana haki ya urithi ni ya kwako, na haki ya kulinunua ni yako. Linunue kwa ajili yako.' Kisha nilijua kuwa hili lilikuwa neno la Yahwe.
And he came to me Hanamel [the] son of uncle my according to [the] word of Yahweh to [the] courtyard of the guard and he said to me buy please field my which [is] at Anathoth which - [is] in [the] land of Benjamin for [belongs] to you [the] right of possession and [belongs] to you the redemption buy [it] for yourself and I knew that [was] [the] word of Yahweh it.
9 Kwa hiyo nililinua shamba katika Anathothi kutoka kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na nilipima fedha kwa ajili yake, shekeli kumi na saba katika uzito.
And I bought the field from with Hanamel [the] son of uncle my which [was] at Anathoth and I weighed out! for him the silver [was] seven shekels and ten the silver.
10 Kisha niliandika katika barua na kuitia muhuri, na kulikuwa na mashadi wakaishuhudia. Kisha nikampa fedha katika mizani.
And I wrote on the document and I sealed [it] and I caused to witness [it] witnesses and I weighed out the silver on scales.
11 Kisha nikaichukua hati ya manunuzi ambayo ilikuwa imepigwa muhuri, kwa kuifuata amri na taratibu, na kama ilivyo ada.
And I took [the] document of the purchase the sealed [one] the order and the conditions and the uncovered [one].
12 Ile barua nikampa Baruku mwana wa Neria wa Maaseya mbele ya Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mashahidi waliotia sahihi kwenye barua iliyopigwa muhuri, na mbele ya Wayahudi wote waliokaa katika uwanja wa walinzi.
And I gave the document the purchase to Baruch [the] son of Neriah [the] son of Mahseiah to [the] eyes of Hanamel uncle my and to [the] eyes of the witnesses who wrote on [the] document of the purchase to [the] eyes of all the Jews who were sitting in [the] courtyard of the guard.
13 Kwa hiyo nikampa amri Baruku mbele yao. Nilisema,
And I commanded Baruch to eyes their saying.
14 Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Chukua nyaraka hizi, vyote hati hii ya manunuzi iliyopigwa muhuri na nakala zisizopigwa muhuri za manunuzi, na uziweke katika chungu cha udongo ili vidumu kwa muda mrefu.
Thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel take the documents these [the] document of the purchase this and the sealed [one] and [the] document uncovered this and you will put them in a vessel of earthenware so that they may remain days many.
15 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nyumba, mashamba, na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika nchi hii.
For thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel again they will be bought houses and fields and vineyards in the land this.
16 Baada ya kumpa Baruki mwana wa Neria ile hati ya manunuzi, nikaomba kwa Yahwe nikasema,
And I prayed to Yahweh after gave I [the] document of the purchase to Baruch [the] son of Neriah saying.
17 Ole, Bwana Yahwe! Angalia! Wewe peke yako umezitengeneza mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulioinuka. Hakuna kitu ambacho ukisema kwako ni kigumu sana kukifanya.
Alas! O Lord Yahweh there! - you you made the heavens and the earth by strength your great and by arm your outstretched not it is [too] difficult for you any thing.
18 Wewe huonesha agano la uaminifu kwa maelfu na kumimina makosa ya wanadamu katika mapaja ya watoto wao baada yao. Wewe ni Mungu mkuu na mwenye nguvu.
[who] does Covenant loyalty to thousands and [who] pays back [the] iniquity of fathers into [the] bosom of children their after them God great mighty [is] Yahweh of hosts name his.
19 Wewe ni mkuu katika hekima na una nguvu katika matendo, kwa maana macho yako yanaona njia zote za watu, ili kumlipa kila mtu stahiki ya matendo yake.
great of Counsel and [the] great of deed[s] who eyes your [are] opened on all [the] ways of [the] children of humankind to give to everyone according to ways his and according to [the] fruit of deeds his.
20 Ulifanya ishara na maajabu katika nchi ya Misiri. Hata leo hapa Israeli na kati ya wanadamu wengine wote, umelifanya jina lako kuwa maarufu.
Who you performed signs and wonders in [the] land of Egypt until the day this and in Israel and among humankind and you have made for yourself a name as the day this.
21 Kwa maana uliwanunua watu wako Israeli kwa ishira na maajabu, kwa mkono hodari, kwa mkono ulioinuka, na kwa hofu kuu.
And you brought out people your Israel from [the] land of Egypt by signs and by wonders and by a hand strong and by an arm outstretched and with terror great.
22 Kisha uliwapa nchi hii—ambayo uliapa kwa babu zao kwamba utawapa—nchi itiririkayo maziwa na asali.
And you gave to them the land this which you had sworn to ancestors their to give to them a land flowing of milk and honey.
23 Hivyo walingia na kuimiliki. Lakini hawakuitii sauti yako wala kuishi kwa kuitii sheria yako. Hawakufanya chochote ulichowaamuru kufanya, kwa hiyo umeleta juu yao majanga haya yote.
And they came and they took possession of it and not they listened to voice your (and in law your *Q(K)*) not they walked all that you had commanded to them to do not they did and you have caused to happen to them all the calamity this.
24 Angalia! Urefu wa maboma haya umefika hadi kwenye mji ili kuuteka. Kwa sababu ya upanga, njaa, na tauni, mji umetiwa kwenye mikono ya Wakaldayo wanaopigana dhidi yake. Kwa maana ulichosema kitatokea sasa kinatokea, na ona, unatazama.
There! the mounds they have come the city to capture it and the city it has been given in [the] hand of the Chaldeans who are fighting on it because of the sword and the famine and the pestilence and [that] which you spoke it has happened and there you [are] seeing [it].
25 Kisha wewe mwenyewe uliniambia, “Nunua shamba kwa fedha kwa ajili yako na mashahidi wameshuhudia, ingawa mji huu unatiwa mikononi mwa Wakaldayo.””
And you you have said to me O Lord Yahweh buy for yourself the field with silver and cause to witness [it] witnesses and the city it has been given in [the] hand of the Chaldeans.
26 Neno la Mungu likaja kwa Yeremia, likisema,
And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah saying.
27 “Angalia! Mimi ni Yahwe, Mungu wa wanadamu wote. Kuna kitu cho chote kigumu sana kwangu kukifanya?
Here! I [am] Yahweh [the] God of all flesh ¿ for me is it [too] difficult any thing.
28 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi, 'Ona, niko karibu kuutia mji huu kwenye mikono ya Wakaldayo na Nebukadreza, mfalme wa Babeli. Atauteka.
Therefore thus he says Yahweh here I [am] about to give the city this in [the] hand of the Chaldeans and in [the] hand of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and he will capture it.
29 Wakaldayo wanaopigana dhidi ya mji huu watakuja na kuwasha moto kwenye mji huu na kuunguza, pamoja na nyumba juu ya paa la watu waliomwabudu Baali na kumimina dhabihu kwa miungu wengine ili kunikasirisha.
And they will come the Chaldeans who are fighting on the city this and they will set on fire the city this with fire and they will burn it and the houses which people made smoke on roofs their to Baal and they poured out drink offerings to gods other so as to provoke to anger me.
30 Kwa maana watu wa Israeli na Yuda hakika wamekuwa watu wanaofanya maovu mbele ya macho yangu tangu ujana wao. Watu wa Israeli hakika wameniudhi kwa matendo ya mikono yao—hili ni tangazo la Yahwe.
For they have been [the] people of Israel and [the] people of Judah only doing the evil in view my since youth their for [the] people of Israel only [are] provoking to anger me by [the] work of hands their [the] utterance of Yahweh.
31 Yahwe anatangaza kwamba mji huu umekuwa sababu ya hasira yangu na ghadhabu yangu tangu siku walipoujenga. Umekuwa hivyo hata leo. Kwa hiyo nitaundoa mbele ya uso wangu
That on anger my and on rage my it has been to me the city this from the day when they built it and until the day this to remove it from on face my.
32 kwa sababu ya uovu wote wa watu wa Israeli na Yuda, mambo waliyofanya ili kunichukiza—wao, wafalme wao, wana wa wafalme, makuhani, manabii, na kila mtu katika Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.
On all [the] evil of [the] people of Israel and [the] people of Judah which they have done to provoke to anger me they kings their officials their priests their and prophets their and everyone of Judah and [the] inhabitants of Jerusalem.
33 Wamenigeuzia migongo yao badala ya nyuso zao, ingawa niliwafundisha kwa furaha. Nilijitahidi kuwafundisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyenisikiliza ili kupokea marekebisho.
And they turned to me a back and not a face and I taught them rising early and teaching and not they [were] listening to accept correction.
34 Walisimamisha sanamu zao za ajabu katika nyumba inayoitwa kwa jina langu, ili kunitia unajisi.
And they put detestable things their in the house which it was called name my on it to make unclean it.
35 Wakazijenga sehemu za juu katika Bonde la Beni Hinomu ili kuwatia katika moto wana wao na binti zao kwa ajili ya Moleki. Mimi sikuwaagiza. Sikuweka akilini mwangu kamwe kwamba watafanya mambo maovu na kwa hiyo kuwasabisha Yuda watende dhambi.
And they built [the] high places of Baal which - [are] in [the] valley of Ben Hinnom to make pass through sons their and daughters their to Molech which not I had commanded them and not it had come up on heart my to do the abomination this so as (to cause to sin *Q(k)*) Judah.
36 Kwa hiyo sasa, Mimi, Yahwe, Mungu wa Israeli, kuhusu mji huu ninasema hivi, 'mji ambao mnasema, 'Umetiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli kwa upanga, njaa, na pigo.'
And now therefore thus he says Yahweh [the] God of Israel concerning the city this which - you [are] saying it has been given in [the] hand of [the] king of Babylon by the sword and by famine and by pestilence.
37 Ona, niko karibu kuwakusanya kutoka kila nchi nilikowapeleka katika hasira yangu, ghadhabu, hasira kuu. Niko karibu kuwarudisha kwenye sehemu hii na kuwawezesha kuishi katika usalama.
Here I [will be] gathering them from all the lands where I have banished them there in anger my and in rage my and in wrath great and I will bring back them to the place this and I will cause to dwell them to security.
38 Kisha watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
And they will become for me a people and I I will become for them God.
39 Nitawapa moyo mmjoa na na njia moja ya kuniheshimu kila siku ili kwamba yawepo mema kwa ajili yao na uzao wao baada yao.
And I will give to them a heart one and a way one to fear me all the days for good for them and for children their after them.
40 Kisha nitafanya pamoja nao agano la milele, ili nisiache kufanya mema kwa ajili yao. nitajiwekea heshima katika mioyo yao, ili kwamba wasiniache.
And I will make to them a covenant of perpetuity which not I will turn back from after them to do good to I them and fear my I will put in heart their to not to turn aside from with me.
41 Kisha nitajifurahisha katika kufanya mema kwao. Kwa uaminifu nitawapanda katika anchi hii kwa moyo wangu wote na maisha yangu yoye.
And I will rejoice on them to do good to them and I will plant them in the land this in faithfulness with all heart my and with all being my.
42 Kwa amaana Yahwe anasema hivi, 'Kama tu nilivyoyaleta majanga haya makubwa yote juu ya watu hawa, hivyo hivyo nitaleta juu yao mambo mema niliyosema kwamba nitafanya kwa ajili yao.
For thus he says Yahweh just as I have brought to the people this all the calamity great this so I [will] bring on them all the good which I [am] speaking to them.
43 Basi mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, ambayo mnaisema, “Hii ni nchi iliyoharibiwa, isiyo na mwanadamu wala mnyama. Imetiwa mikononi mwa Wakaldayo”
And it will be bought the field in the land this which - you [are] saying [is] a desolation it from not human being and an animal it has been given in [the] hand of the Chaldeans.
44 Watanunua mashamba kwa fedha na kuandika katika barua zilizopigwa muhuri. Watawakusanya mashahidi katika nchi ya Benyamini, wote kuzunguka Yerusalemu na miji ya Yuda katika miji ya nchi yenye vilima, na katika nchi tambarare, na katika miji ya Negebu. Kwa maana nitawarejesha wafungwa wao—hili ni tangazo la Yahwe.”'
Fields for silver people will buy and they will write on the document - and they will seal [it] and cause to witness [it] witnesses in [the] land of Benjamin and in [the] surroundings of Jerusalem and in [the] cities of Judah and in [the] cities of the hill country and in [the] cities of the Shephelah and in [the] cities of the Negev for I will turn back captivity their [the] utterance of Yahweh.

< Yeremia 32 >