< Yeremia 29 >

1 Haya ni maneno katika waraka ambao Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa wazee waliosalia miongoni mwa mateka na makuhuni, manabii, na watu wote ambao Nebukadreza aliwapeleka utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli.
این است سخنان رساله‌ای که ارمیانبی از اورشلیم نزد بقیه مشایخ اسیران وکاهنان و انبیا و تمامی قومی که نبوکدنصر ازاورشلیم به بابل به اسیری برده بود فرستاد.۱
2 Hii ilikuwa baada ya Yekonia mfalme, mama yake mfalme, na watumishi wakuu, viongozi wa Yuda na Yerusalemu, na wahunzi walikuwa wamepelekwa mbali na Yerusalemu.
بعداز آنکه یکنیا پادشاه و ملکه و خواجه‌سرایان وسروران یهودا و اورشلیم و صنعتگران و آهنگران از اورشلیم بیرون رفته بودند.۲
3 Aliutuma waraka huu kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani, Gemaria, mwana wa Hilkia, ambaye Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemtuma kwa Nebukadreza mfalme wa Babeli
(پس آن را) به‌دست العاسه بن شافان و جمریا ابن حلقیا که صدقیا پادشاه یهودا ایشان را نزد نبوکدنصرپادشاه بابل به بابل فرستاد (ارسال نموده )، گفت:۳
4 Waraka ulisema, Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kwa mateka ambao niliwasababisha kuwa mateka kutoka Yerusalemu hadi Babeli,
«یهوه صبایوت خدای اسرائیل به تمامی اسیرانی که من ایشان را از اورشلیم به بابل به اسیری فرستادم، چنین می‌گوید:۴
5 'Jengeni nyumba na muishi ndani yake. Pandeni bustani na mle matunda yake.
خانه‌ها ساخته در آنها ساکن شوید و باغها غرس نموده، میوه آنها را بخورید.۵
6 Chukueni wake na mzae wana na mabinti. Kisha Kisha chukueni wake kwa ajili ya wana wenu, na wapatieni waume binti zenu. Wazae wana na mabinti na waongezeke ili msiwe wachache sana.
زنان گرفته، پسران و دختران به هم رسانید و زنان برای پسران خود بگیرید ودختران خود را به شوهر بدهید تا پسران ودختران بزایند و در آنجا زیاد شوید و کم نگردید.۶
7 Itafuteni amani ya mji ambako nimewafanya kuwa watumwa, na mkauombee kwangu kwa niaba yake kwa kuwa kutakuwa na amani kwenu kama mji uko katika amani.'
و سلامتی آن شهر را که شما را به آن به اسیری فرستاده‌ام بطلبید و برایش نزد خداوند مسالت نمایید زیرا که در سلامتی آن شما را سلامتی خواهد بود.۷
8 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, 'Msiwaache manabii ambao wako katikati yenu na wabashiri wenu kuwadanganya, na msizisikilize ndoto ambazo ninyi wenyewe mnaota.
زیرا که یهوه صبایوت خدای اسرائیل چنین می‌گوید: مگذارید که انبیای شماکه در میان شمااند و فالگیران شما شما را فریب دهند و به خوابهایی که شما ایشان را وامی داریدکه آنها را ببینند، گوش مگیرید.۸
9 Kwa maana wanatabiri uongo kwenu katika jina langu. Mimi sikuwatuma—hili ni tangazo la Yahwe.'
زیرا خداوندمی گوید که ایشان برای شما به اسم من کاذبانه نبوت می‌کنند و من ایشان را نفرستاده‌ام.۹
10 Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Babeli atakapokuwa amewatawala kwa muda wa mika sabini, nitawasaidia ninyi na kulitimiza neno langu jema kwa ajili yenu ili kuwarudisha ninyi katika sehemu hii.
وخداوند می‌گوید: چون مدت هفتاد سال بابل سپری شود من از شما تفقد خواهم نمود وسخنان نیکو را که برای شما گفتم انجام خواهم داد؛ به اینکه شما را به این مکان باز خواهم آورد.۱۰
11 Kwa maana mimi mwenyewe naijua mipangao niliyonayo kwa ajili yenu—hili ni tangazo la Yahwe—mipango kwa ajili ya amani na siyo kwa ajili ya mabaya, ili kuwapa ninyi tumaini na siku zenu za mwisho.
زیرا خداوند می‌گوید: فکرهایی را که برای شما دارم می‌دانم که فکرهای سلامتی می‌باشد ونه بدی تا شما را در آخرت امید بخشم.۱۱
12 Kisha mtaniita, na kwenda na kuniomba mimi, na nitawasikiliza.
و مراخواهید خواند و آمده، نزد من تضرع خواهید کردو من شما را اجابت خواهم نمود.۱۲
13 Kwa maana mtanitafuta na kunipata, kwa kuwa mtanitafuta kwa moyo wenu wote.
و مراخواهید طلبید و چون مرا به تمامی دل خودجستجو نمایید، مرا خواهید یافت.۱۳
14 Kisha nitapatikana kwenu—hili ni tangazo la Yahwe—na nitawarudisha watu wenu waliofungwa; nitawakusanya kutoka mataifa yote na sehehemu zote ambako nimewatawanya—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitawarudisha kutoka sehemu ambako niliwasababisha kuwa mateka.
و خداوندمی گوید که مرا خواهید یافت و اسیران شما را بازخواهم آورد. و خداوند می‌گوید که شما را ازجمیع امت‌ها و از همه مکان هایی که شما را درآنها رانده‌ام، جمع خواهم نمود و شما را از جایی که به اسیری فرستاده‌ام، باز خواهم آورد.۱۴
15 Tangu mliposema kwamba Yahwe ameinua manabii kwa ajili yetu katika Babeli,
از آن رو که گفتید خداوند برای ما در بابل انبیا مبعوث نموده است.۱۵
16 Yahwe anasema hivi kwa mfalme aliyeketi katika kiti cha enzi cha Daudi na watu wote wakaao katika mji huo, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi utumwani—
«پس خداوند به پادشاهی که بر کرسی داودنشسته است و به تمامی قومی که در این شهرساکنند، یعنی برادران شما که همراه شما به اسیری نرفته‌اند، چنین می‌گوید:۱۶
17 Yahwe wa majeshi anasema hivi, ''Ona, niko karibu kutuma upanga, njaa, na ugonjwa juu yao. Kwa maana nitawafanya kuwa kama tini mbovu ambazo ni mbaya sana hazifai kuliwa.
بلی یهوه صبایوت چنین می‌گوید: اینک من شمشیر وقحط و وبا را بر ایشان خواهم فرستاد و ایشان رامثل انجیرهای بد که آنها را از بدی نتوان خورد، خواهم ساخت.۱۷
18 Kisha nitawafuata kwa upanga, njaa, na tauni na kuwafanya kuwa kitu cha kushangaza kwa falme zote juu ya dunia—kitu cha kuogofya, kitu cha kulaaniwa na kuzomewa, na kitu cha aibu miongoni mwa mataifa yote ambako nilimtawanya.
و ایشان را به شمشیر و قحط ووبا تعاقب خواهم نمود و در میان جمیع ممالک جهان مشوش خواهم ساخت تا برای همه امت هایی که ایشان را در میان آنها رانده‌ام، لعنت و دهشت و مسخره و عار باشند.۱۸
19 Hii ni kwa sababu hawakulisikiliza neno langu—hili ni tangazo la Yahwe—ambalo nililituma kwao kupitia watumishi wangu manabii. Niliwatuma tena na tena, lakini hamkusikiliza—hili ni tangazo la Yahwe. '
چونکه خداوند می‌گوید: کلام مرا که به واسطه بندگان خود انبیا نزد ایشان فرستادم نشنیدند با آنکه صبح زود برخاسته، آن را فرستادم اما خداوند می‌گویدکه شما نشنیدید.۱۹
20 Kwa hiyo ninyi wenyewe sikilizeni neno la Yahwe, ninyi mateka wote ambao amewatuma kutoka Yerusalemu hadi Babeli,
و شما‌ای جمیع اسیرانی که از اورشلیم به بابل فرستادم کلام خداوند رابشنوید.۲۰
21 'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya na Sedekia mwana wa Maaseya, watabirio uongo kwenu katika jina langu: Ona, niko karibu kuwaweka katika mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babeli. Atawaua mbele ya macho yenu.
یهوه صبایوت خدای اسرائیل درباره اخاب بن قولایا و درباره صدقیا ابن معسیا که برای شما به اسم من کاذبانه نبوت می‌کنند، چنین می‌گوید: اینک من ایشان را به‌دست نبوکدنصرپادشاه بابل تسلیم خواهم کرد و او ایشان را درحضور شما خواهد کشت.۲۱
22 Kisha laana itatamkwa na wafungwa wote wa Yuda katika Babeli kuhusu watu hawa. Laana itasema: Yahwe awafanye kuwa kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka kwenye moto.
و از ایشان برای تمامی اسیران یهودا که در بابل می‌باشند لعنت گرفته، خواهند گفت که خداوند تو را مثل صدقیاو اخاب که پادشاه بابل ایشان را در آتش سوزانید، بگرداند.۲۲
23 Hili litatokea kwa sababu ya mambo ya aibu waliyofanya katika Israeli walipofanya uzinzi na wake za majarani zao na kutangaza maneno ya uongo katika jina langu, mambo ambayo sikuwaamuru wayaseme. Kwa maana mimi ndiye nijuaye; mimi ni shahidi—hili ni tangazo la Yahwe.”'
چونکه ایشان در اسرائیل حماقت نمودند و با زنان همسایگان خود زنا کردند و به اسم من کلامی را که به ایشان امرنفرموده بودم کاذبانه گفتند و خداوند می‌گوید که من عارف و شاهد هستم.۲۳
24 Kuhusu Shemaya Mnehelami, sema hivi:
«و شمعیای نحلامی را خطاب کرده، بگو:۲۴
25 'Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu ulituma barua kwa jina lako kwa watu wote katika Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa Maaseya kuhani, na kwa makuhani wote, na ulisema,
یهوه صبایوت خدای اسرائیل تکلم نموده، چنین می‌گوید: از آنجایی که تو رسایل به اسم خود نزد تمامی قوم که در اورشلیم‌اند و نزدصفنیا ابن معسیا کاهن و نزد جمیع کاهنان فرستاده، گفتی:۲۵
26 “Yahwe aliwafanya ninyi kuwa makuhani badala ya Yehoyada kuhani, ili muwe wasimamizi wa nyumba ya Yahwe. Ninyi ni viongozi wa watu wote wajitiao wazimu na kujifanya wenyewe manabii. Mtawaweka katika mkatale na minyororo.
که خداوند تو را به‌جای یهویاداع کاهن به کهانت نصب نموده است تا برخانه خداوند وکلا باشید. برای هر شخص مجنون که خویشتن را نبی می‌نماید تا او را درکنده‌ها و زنجیرها ببندی.۲۶
27 Kwa hiyo sasa, kwa nini hamkumkemea Yeremia wa Anathothi, ambaye hujifanya mwenyewe nabii juu yenu?
پس الان چرا ارمیاعناتوتی را که خود را برای شما نبی می‌نمایدتوبیخ نمی کنی؟۲۷
28 Kwa maana ametutumia sisi katika Babeli, 'Itakuwa muda mrefu. Jengeni nyumba na muishi ndani yake, na pandeni busitani na mule matunda yake.””
زیرا که او نزد ما به بابل فرستاده، گفت که این اسیری بطول خواهدانجامید پس خانه‌ها بنا کرده، ساکن شوید و باغهاغرس نموده، میوه آنها را بخورید.»۲۸
29 Sefania kuhani akaisoma barua hii mbele ya Yeremia nabii.
و صفنیای کاهن این رساله را به گوش ارمیانبی خواند.۲۹
30 Kisha neno la Yahwe likaja kwa Yeremia, likisema,
پس کلام خداوند بر ارمیا نازل شده، گفت:۳۰
31 “tuma neno kwa mateka wote na sema, 'Yahwe anasema hivi kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi wakati mimi sikumtuma, na amewaongoza kuamini uongo,
«نزد جمیع اسیران فرستاده، بگوکه خداوند درباره شمعیای نحلامی چنین می‌گوید: چونکه شمعیا برای شما نبوت می‌کند ومن او را نفرستاده‌ام و او شما را وامیدارد که به دروغ اعتماد نمایید،۳۱
32 kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kumwadhibu Shemaya Mnehelami na uzao wake. Hapatakuwa na mtu wa kukaa miongoni mwa watu hawa kwa ajili yake. Hataona mema nitakayofanya kwa ajili ya watu wangu—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana ametangaza uasi dhidi ya Yahwe.””
بنابراین خداوند چنین می‌گوید: اینک من بر شمعیای نحلامی و ذریت وی عقوبت خواهم رسانید و برایش کسی‌که درمیان این قوم ساکن باشد، نخواهد ماند و خداوندمی گوید او آن احسانی را که من برای قوم خودمی کنم نخواهد دید، زیرا که درباره خداوند سخنان فتنه انگیز گفته است.»۳۲

< Yeremia 29 >